Free talk: Mwanamke shtuka!

Free talk: Mwanamke shtuka!

Umeongea point, hakuna kitu kizuri kwa mwanamke kama kuwa na akili ya kujiongeza kujituma na kuwa mtafutaji kabla hata hujaolewa, sio unataka kuolewa hata kishughuli kidogo cha kukufanya ulete kitu mezani huna. Maisha yamebadilika wanaume nao siku hizi wanaangalia una nini na wewe, sio akubebe tuu ukawe wa kuomba tu kila siku, vinginevyo hela utapewa, mechi utachezeshwa na mwisho wa siku unashangaa umeachwa kaolewa Mwajuma unabaki kutafuta mchawi.
Na mara nyingi ukikuta mwanamke wa aina hiyo huwa ni wale wasio jielewa by nature, na hana akili ya kujiongeza, ndo hao wa kujaza viatu na mapochi ukimuambia kuhusu kuwekeza ndo kwanza unaonekana mshamba wewe unaongea nini. Hata akikaa na mwanaume hana cha maana cha kuongea utakuta ni pumba tu mpaka mwanaume anajiuliza hivi huyu kichwani kuna kitu kinachoitwa maendeleo anakijua kweli? tujielewe.
Kila mwanamke nikidate nae ni wa aina hii. Mungu nilikukosea nini.!
 
Kuhusu kuomba fedha, kwanza namuona kila Mara yuko busy na familia yake, muda wote utasikia wanampigia simu za wagonjwa, misiba, ada za shule etc. Hill si tatizo kwangu. Zikitulia simu za ndugu ataanza kudeal na ujenzi, simu za mafundi zinapishana, bado service za magari, utasikia kununua viwanja au mashamba...... Hela yake yote ni kama ni ya maendeleo yake, sasa ukisikia analalamika kaelemewa, utapata nguvu ya kumuomba? Nikikasirika anavurugwa, hapo napo kuna mawili, ataniomba niongee naye private, akiona sijisikii,atatafuta namna tuonane akiwa na rafiki zake, huwa siwezi kuonesha hasira mbele za watu. Tukitoka hapo,ataomba kuongea na Mimi!
Miaka yote nimekuwa kwenye distant relationship, ila muda huu nikaamua niwe na mahusiano ya karibu labda ntaona tofauti, kinacho niboa hata akija kwangu akaona hela anachukua! Mwanzoni nilikuwa nachukulia poa, ila muda huu akijichanganya achukue huwa anapata habari yake,nilisha acha hata kupika akija kunitembelea. Nilikuwa nafanya kwa kupenda lakini nikaona inakuwa kama sheria huku hela yake siijui. Nikijisikia kwenda kwake sijusumbui tena na kazi za nyumbani kama mwanzo. Yaani natafuta stability tu ya moyo wangu then niondoke. Msiseme ni Mario, hapana. Ni MTU mwenye kazi yake, na sikujipeleka, ilimchukua muda kunitafuta na kunipata, na mwanzo alikuwa akifanya kila kitu mpaka nalia!
Alipo kuja kugundua kuwa Nina vimifereji vya hela, nikawa nimejiroga. Na sikuwa na namna maana kama ni safari atajua kuwa nimesafiri nk!
Sina cha kuongeza, haya mambo kila mtu ana experience yake.I pray that upate mtakayefurahiana... #mutualfeelings
 
Kuna vitu unafanyiwa na mpenzi wako kama favour kwa kuwa wewe ni mwanaume au mwanamke wake....... Naweza kuwa Nina uwezo wa kujilipia saloon, lkn ukinilipia kama mpenzi wako, hiyo ni favour, najisikia kuwa kuna MTU ananijali...... I don't see a lady in me, thou I did everything to make him feel like my lovely man!
Damn!

Nimekuhurumia.
 
Nikiwa binti, mara nyingi ijumaa tulikuwa na mikesha ya vijana, sio tu kuombeana ila nakukumbushana vitu mbalimbali. Namshukuru Mungu kwa ajili ya Pastor wetu, kuna muda alikuwa anatupa makavu hadi kanisani unapaona pachungu, Ila alitutengeneza tukawa watu fulani amazing sana.

He used to tell us young ladies; muda ambao hujaolewa ndo muda wa kufulfil your dreams; making an identity of your own. Once ukiolewa mara nyingi sana utatimiza ndoto/kutembea na vision ya mumeo. Majority tunaua ndoto zetu tukiingia ndoani (sad). So alitutaka tufanye kazi kwa bidii, adding values to our lives, sio tuspend kwenye unnecessary starehe kujifanya slay queens; waiting to get married and chop our hubby's money. Kuna wakati anamsimamisha kijana mdogo yupo high school (inspiration) ila tu ni anachakarika akikutajia assets zake, mimi limama lizima naona aibu na kupata tabu sana. Hakutaka kusikia kitu "I'm doing nothing". Kuna maisha zaidi ya kuolewa, what if usipoolewa, ndo utaishi ukiinvest kwenye kujiremba milele?

Hujapanga, unakaa home, make sure una vitu/assets zako. Sio kusubiri zawadi na vyombo vya send off ndo ukaanzie maisha, wewe binafsi unabeba nguo na viatu na mapochi.
Na alikuwa anatuambia kabisa, tusiende tukawe mizigo kwa waume zetu, hata chumvi ikiisha unasubiri baba atoke kazini. Wengine wanalia mume wangu ananinyanyasa sana, Ila wakati mwingine ni kwa sababu huna mchango wowote financially nyumbani, anakuchokaa. Afu pamoja na kuzaa, bado tuna wajibu wa kutimiza ndoto za watoto wetu. Watoto wako wasishindwe kutimiza ndoto zao kisa baba amekataa kuwahudumia au hayupo au tukasema ni kazi ya baba yao tu. Though sio kama kila mtu atafanikiwa kuinvest as we wish, ila kuwa na ile spirit ya kuthubutu/ kutaka kufika mahala fulani ni jambo zuri sana. Kwa sababu hata usipofanikiwa leo, you won't rest till you make it happen.

Na maisha yana ups and downs, hata ukiolewa na bilionea possibly kuna siku maisha yatashake kidogo, sasa ukiwa slay queen, hicho kipindi cha mpito kitapita salama? Usije ukamuua kwa presha mumeo kwa kutaka aendelee kukuhudumia as it was before, au utakimbia nyumba? au utatafuta sponsors ili uendelee kumaintain status?. Make your own identity lady. Mwanamke ana nguvu ya kumultiply, chochote kidogo kitakachopandwa kwake/kufanywa na yeye, atakitunza hadi kiongeze na vingine. (I missed magazeti mweeh)
wanawake " wenye" mawazo kama haya ya kwako" walishakufa wote kwenye vita ya kagera" ...but umeongea kitu kikubwa sana'' Mwenye macho aone" na mwenye masikio asikie
 
Jamani sasa mbona me bado nipo hai (kidding). Wenye mawazo hayo bado wapo; wengi tu
wanawake " wenye" mawazo kama haya ya kwako" walishakufa wote kwenye vita ya kagera" ...but umeongea kitu kikubwa sana'' Mwenye macho aone" na mwenye masikio asikie
 
Hivi kumbe kuna wanawake bado wanajielewa?? Mbona sikutani nao asee
 
Logic....
Habari wana MMU.

Kuna hili jambo ningependa tujadiliane ama tushirikishane kidogo.

Hakuna asiejua kuwa kila mwanamke kabla hatujavurugwa na dunia huwa matamanio yetu ni siku moja kuolewa na kutengeneza familia na mwanaume fulani hivi amazing(fantancy vs reality).

Sasa tatizo linakuja kuwa huwa wanawake wengi wana mentality kuwa maandalizi ya familia ya baadae haswa kwa mambo yanayohusu assets na gharama zingine ni majukumu ya mwanaume na sio mwanamke.
Hivyo unaweza kukuta binti ana kazi nzuri tu ila hata kujiwekeza kununua hata kiwanja walaaa hawazi au hata kufungua biashara. Anawekeza kwenye mikoba,mawigi,simu za bei ghali,viatu nk. Vitu ambavyo ukivipigia mahesabu unakuta ana viwanja vitano vikubwa tu huku kijijini kwetu.

Hebu fikiria unaolewa ukiwa angalau umejiwekeza kiasi fulani hivyo mkiunganisha nguvu na mwenza wako angalau mnapiga hatua kadhaa kwa haraka kuliko kusubiria mwanaume afanye kila kitu.

Wakati mwingine unakuta binti anadate mwanaume mwenye expossure ya kutosha na mfanyabiashara mzuri, hata kuomba basi hata aelekezwe abc's za biashara, hata kuunganishwa kibiashara nehiiii.

Au unadate mwanaume mwenye uwezo mkubwa kifedha hivyo kazi yake ni kuomba kununuliwa simu ya milioni 2 nk, vitu vya anasa ambavyo kwa kiasi kikubwa havikuongezei lolote la maana zaidi ya sifa za kijinga. Ni kwanini usimuombe mtu wa aina hiyo hata business idea, au angalau uanze jambo lako ie biashara,ujenzi nk kisha umuombe akuongezee kiasi fulani cha pesa? Kwa mwanaume mwenye upeo atakuona una akili na anaweza kukusogeza mahali pazuri.

Mwingine unakuta ni mama kabisa ila hata haiwazii kesho ya mtoto wake ambae anamlea peke yake, yuko busy na starehe na kutumbua pesa za child support, kesho na keshokutwa baba hayupo mtu anaanza kuhaha wakati nafasi ilikuwepo akaichezea

Maisha yamebadilika sana jamani basi nasi wanawake tubadilike in a positive way, tuyaishi maisha halisi na sio ya kuigiza ili angalau tunapoingia kwenye maisha ya ndoa angalau tuwe na cha kuongeza sio ndio ukiolewa umtwishe mwanaume majukumu ya familia mnayoijenga,familia ya kwao na ya kwenu pia. No wonder wanakufa mapema hawa watu.

Tuzitumie fursa vizuri pale zinapopatikana kabla haijawa too late.

Jamani hapa simchagulii mtu maisha ila hakikisha hautokuwa na majuto baadae kuwa "laiti ningejua"!!! Maana hakuna anaependa kesho yake iwe ya kuunga unga.

Nawasilisha.
 
Have ma" like babe-girlunajua nini umesema maneno maziiito mno mwenye kusikia na asikie,.japo KUPANGA NI KUCHAGUA hatuingiliani lifestyles lakini penye ukweli lazima tukumbushane...

Wadada tupunguze luxuries tofauti na vipato vyetu,.tuwe na kiasi na kuridhika..tukipata wenzetu hebu tupeane support sio kisa ni mbebe wako basi ndio akome kila dhiki unambebesha kaka wa watu looh tena ujue kwao wana japo mbuzi wa maziwa basi hali akashiba.,.ndio maana wengine miti mikavu hawanenepagi kwa kufyonzwa....tujue kufanya kazi zetu na kusave pia kwa ajili ya baadae,.kumtegemea mtu sana kwanza dhambi...

Yeremia 17:5-8 ukisoma utaona mtu anaye mtegemea mwanadamu anakuwaje...

Mungu akatubariki sawasawa na utajiri wake,kusukwa-sukwa hata kumwagika...!!!!
.
IMG_20200904_165349.jpg
 
Back
Top Bottom