Frank na Mkewe

Frank na Mkewe

Ndallo

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2010
Posts
7,621
Reaction score
4,311
Mke wa Frank anajivunia mume mtulivu, hashindi baa na hatongozi videmu.

Akitoka kazini huenda kucheza basketball na hurudi nyakati za dinner. Siku
moja mkewe akamhurumia. Anachoka na kazi. Mtu gani asiyependa starehe japo
kidogo?

... Mke akamlazimisha outing, Frank akabisha lakini taxi ikafika. kituo cha
kwanza ilikuwa ni Kaizari Bar & G.house.

Walipofika mlangoni tu, mlinzi akaita, "Mambo Frank!" "Poa"
"Nilidhani huwa hutaweza kija club, kwa vile ulichoka sana kwa ile mizigo ya
jana!

Inakuwaje mlinzi anakufahamu?" mke akauliza
"Yule mgambo, mchana analinda ofisini kwetu, usiku anapiga part time hapa"
akajibu Frank

Wakachagua meza. Kukaa tu tayari mhudumu ameshaleta castle lager.

Akamuuliza mama anakunywa nini. Mhudumu alipoondoka mama akauliza,

"amejuaje unakunywa castle kama
hakufahamu?"

Wakati Frank anajikanyaga aanze vipi kujitetea, mhudumu wa vyumba akawa
amefika na kuuliza.

"Mkuu kama kawaida bila zana au? nimekuandalia namba tano, nendeni tu
vinywaji nitawaletea huko huko"

Kufikia hapo mama akawa hana simile tena, akanyanyuka akitukana kama chizi.
Akatoka nje mbio na kuingia katika taxi iliyokuwepo pale.

Wakati anapatana bei na dereva, Frank naye akaingia. Mama yakamporomoka
matusi kibao na kilio juu. Alipovuta kamasi na kupiga kwikwi akamsikia
dereve anasema.

"Duh, eee bwana Frank huyu malaya uliyeokota leo balaaaaaaaaaaaaaaa kuliko
wa jana!!!!!!"

Mamaa akazimiaaaa.........zzzzzzzzzzzzzzzzzzzz
 
Mhhh kamkuta jamaa anafahamika kuliko alivyodhani
Alijua jamaa mtu wa mazoezi tuu na kazi kumbe yako yaliyojificha
 
iweke ktk vitanu km shigongo unaweza ukatoka.
 
hayo yanatojea sana,cha msingi ni kuomba Mungu hata usijue mwenzio anafanyaga kitu gani akiwa mbali nawe vinginevyo waweza kufa kabisa achilia mbali kuzimia.Ila du.............yataka moyo nayo hayo khaaaaaaaa!!!
 
Pale sasa wadada tunapojishaua ati baby wangu hatomboki kwingine,..teh teh
 
kama nilishaga iona hivi, ila ni nzuriiiiiiii
 
Ni vema kama wanaume kukumbushana uaminifu kwa wenzi wetu.
 
duh hata ningekua mimi ningezimia au ningekufa kabisa
 
Back
Top Bottom