Forojo Ganze (Master), mchawi maarufu aliyeanzisha Mwenge wa Uhuru

kwa maana nyingine unamaanisha kuwa neno 'harambee' ni mantra? (mantra ni neno maalum lenye energy ambalo likirudiwa mara nyingi lina produce a certain effect}.
ujue hata wayahudi kina ben Gurion mwaka 1948 nchi yao waliamua waiitie ISRAEL ikiwa ni muunganiko wa majina ya miungu wao watatu ISIS, RA, na ELOHIM. Isije ikawa huyu HAR ikawa ni corruption ya jina RA au RAMA wa mahabarata.
raa na mwanae isis ni miungu ya egypt sio israel
 
Kwa hiyo TZ ilikabidhiwa mikononi mwa shetani.Any way nashukuru kwa kufahamu chanzo cha huu mwenge sikiwahi kupata jibu la kuridhisha
Ahsante JF
 
Enhee nambie habali ya lindi na zindiko
Limefanyika eneo gani
Mwaka gani
Na nani walihusika....?
Na kwanini waliichagua lindi na si mkoa mwingine
 
"Baba, sisi tunataka kuwasha mwenge na kuuweka juu ya mlima kilimanjaro, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini mahala pasipo na tumaini, faraja palipo na huzuni, tumaini pasipo na tumaini, upendo penye chuki na heshima palipo na dharau"

Baada ya kutamka hayo mbele ya Mwl.Nyerere, Ganze alikata roho na ndipo ukaanzishwa Mwenge wa Uhuru. Kinachonishangaza hapa ni kile kipengele kisemacho"UMULIKE NJE YA MIPAKA YETU"..... Inamaana ndani ya nchi tubaki gizani kama tulivyo sasa? Na kwann Forojo Ganze hakutangazwa kama mwanzilishi wa Mwenge?
Umeandika " UMULIKE HATA NJEE YA MIPAKA YETU." sasa mbona unajitega mwenyewe
 
Ndiomaana wapinzani kipindi frani wali chachamaa mwenge ufutwe coz wanajua ukiondoa labda ccm yaweza toka madarakan sina uhakika lakin
 
Kuna haja ya Watanzania kuwa na utamaduni wa kuweka Mapito yetu kwenya maandishi ili hata vizazi vijavyo isije kufika wakati vikawa vinabishana juu ya kule taifa limetoka. Mfn leo tuko wenye miaka ya 2000's ikijakufika miaka ya 3000's mtoto atakaye zaliwa let's say 3018 atakuwa anasimuliwa kuwa kuna watu waliwahi kuishi bila kuwa na UMEME au BARABARA au SIMU lakini atabishi na atahitaji ushahidi na atahitaji hata picha ili kudhibitisha....lakini ushahid hautapatikana na ataonekana mshindi........na yule aliyesimulia ataonekana muongo maana amekosa ushahidi. Wazungu ni watunzaji wazuri wa kumbukumbu na historia zao hata sisi tunaweza kujifunza....
 
V
"Baba, sisi tunataka kuwasha mwenge na kuuweka juu ya mlima kilimanjaro, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini mahala pasipo na tumaini, faraja palipo na huzuni, tumaini pasipo na tumaini, upendo penye chuki na heshima palipo na dharau"

Baada ya kutamka hayo mbele ya Mwl.Nyerere, Ganze alikata roho na ndipo ukaanzishwa Mwenge wa Uhuru. Kinachonishangaza hapa ni kile kipengele kisemacho"UMULIKE NJE YA MIPAKA YETU"..... Inamaana ndani ya nchi tubaki gizani kama tulivyo sasa? Na kwann Forojo Ganze hakutangazwa kama mwanzilishi wa Mwenge?
Viongozi wetu mpo?Jamani hatuutaki huu mwenge unatufanya tuwe mazezeta!
 
Kijue kiswahili vizuri umulike hata nje ya mip.................. maana yake unaanzia ndani hadi nje,pia Juu ya Mlima Kilimanjaro ni ndani ya Tanzania siyo Kenya hivyo unamulika ndani na nje ya nchi,pili huyo mchawi unayedai alianzisha mwenge ni ndugu yako nini? au fundi aliyeutengeneza mbona hatumjui angeweka patent right kama alivyofanya Wheel barrow kule ujerumani kwenye toroli tungemuelewa tena tafadhali usituchafulie jina la mwenge wetu wa uhuru na wachawi hiyo ni kufuru,hiyo ndiyo alama pekee inayowaunganisha watanzania iliyobaki na hakuna nyingine zilizobaki zote za kikabila,kikanda,kisiasa na kidini,hata bendera zanzibar wana yao hivi sasa.
Kwani Rais wa Tanzania, hatoshi kuwaunga watanzania?
 
Samahani kwa kwenda off topic kidogo. Ila mimi huwa nina amini kuwa kukosa "mawendeleo" kwetu wa Afrika kunatokana sana na kukana Mungu/miungu wetu na kupapatikia ya wenzetu.
Nchi zote zilizoendelea na zinazoendelea kwa kasi zina Miungu yao. Angalia, Americans, Europeans, Arabs, Chinese and Indians wote wana Miungu yao na wameendelea kuliko Wa Africa na wa Latino ambao kwa aslimia kubwa wameiga Miungu ya wenzao!

Turudi kwenye topic ya Mwenge! Japo sijawahi shiriki maandamano pia sijawahi tafakari sana undani wake. Hoja humu za leo zimenifanya nipate hamu ya kujua zaidi! JF 4 life. Ndio mana niko since 2006!
Ila kiuhalisia, Hizo nchi kama China na India zimekua baada ya population ya Wakristo (Mungu wa Wazungu) kuongezeka.

Na nchi za kiarabu pia wamestick na Mungu wao. Nchi kama Israel ina watu wasiomwamini Yesu Kristo bali wanamkubali Mungu.

Kuna nchi zingine zina maendeleo na zinakuwa kila siku na ni nchi zenye population kubwa ya atheists.

Point yangu ni nini?
Maendeleo ya kidunia, ya kiuchumi nakadhalika; hayana uhusiano wowote aina ya Imani nchi husika inayo.

Nchi zilizoendelea zina idadi kubwa ya watu wanao-invest muda na pesa katika maendeleo. Narudia tena, sio 'wote', bali 'idadi kubwa'. Hawajaridhika na maisha. Bas!
Huo ndo uchawi wa maendeleo.
Enlightenment!




Sent using LF Electromagnetic Waves
 
unavyosema ni kweli haya matukio yapo orally hayajaandikwa bado,na mtu ambaye angekua ametufanyia haki kuiandika hii historia ni mwl .Nyerere kwan alishiriki katika mambo yote na alikua pia ni mwandishi wa vitabu sasa sielewi kwa nini hakutaka kuandika historia iliyotokea na hakuwahi kuandika harakati zake hata mpaka anakufa?

na alikua mwazi kuyasema hadharani,jaribu kufuatilia hotuba zake anasimulia kuhusu mambo aliyofanya wakati wa kuusaka uhuru

kuhusu wazee wa dar kumshauri raisi ni kitu cha kawaida tu kama wazee wenye busara na wanaoijua hii nchi kwani dar ndio kitovu cha harakat zote za uhuru ulipoanzia na kusambazwa mikoani halaf ukarudi tena dar na wanachomshauri siomambo ya economics of country kwani raisi ana washauri wake kwa mambo hayo

tafsiri unavyotaka kama nchi imekabidhiwa mashetan au mungu, ila kwa wazawa wa kweli na wenye kuujua utanzania na uafrika na watanzania wakweli kutoka rohoni na wanaoheshimu mababu zetu waliotuleta hapa dunian,wakatulisha,wakatuvisha wakatulinda na hatari zote kupitia kumuomba huyo mungu ambae watu wanasema ni shetani na kufanikiwa kuhimili maisha kwa kuomba kwa mungu ambaye alikua anatuletea mvua,anatuonesha siri zilizofichika machon,anatufunulia tiba za magonjwa mbalimbali kupitia njozi au njia zingine mpaka ukawepo leo hii. tunasema nchi imekabidhiwa kwa mungu wetu na sio mungu wa kigeni ambae babu zetu hata hawakumjua na aliyekuja akatupeleka utumwani,akatugeuza makoloni yake, huyo kwetu sio mungu ni shetani

na kuna maeneo matakatifu ndani ya hii nchi ambamo tunaenda kusali na tunafanikiwa

hujawahi kujiuliza kwanini viongozi wanakimbilia mlingotin

tafakari na uikimbie mental slavery
 
Back
Top Bottom