Form 4 na wengine, angalieni hapa!

Form 4 na wengine, angalieni hapa!

Yaani huu utaratibu mpya mi sijaufuatilia sana ufaulu wake na qualification zake, lakini ninavyojua kwa Div. 4 ualimu sahau...hata kusomea sheria pia ni ngumu, ushauri wangu tafuta kozi itayokufaa uanze n ngazi ya cheti then ukifaulu vizuri ndo matokeo yako ya cheti somea mambo mengine. Vyuo vya utumishi wa umma ka Public Service College unaweza kusoma pia kozi za Reording Managements au Human Resources certificate na ukaunganisha Diploma

nashukuru sana kwa jibu lako zuri. sasa ni wakati wangu kufanyia kazi.
 
mwenye 3 ya 26
civ c
bios b
chem c
geog c
hist c
engl b
math d
kisw c
je anaweza kuchaguliwa govment wakuu nisaidieni.
 
haya matokeo ndiyo hayo yametoka!! Kila kitu hadharani, sasa ukiwa hapa jf ndo mpango nzima!! Manake watu washaanza kuhoji, mi nina hiki au kile nitafanyaje, haya ngoja nitajaribu kuweka mwongozo na alternatively nyingine due to spme perfomances kwa wote, manake naona huku kitaa watu wanadanganyana sana!!

Hii ni kwa kadri ninavyofahamu mimi, kama kuna marekebisho basi yafuatie:

=> credit qualification kwa hali ya kawaaida ni 'c'-na ili uende form 5 unahitaji uwe na c 3, hapa ni either umebalance combination(comb) au hujabalance. Sasa kama una c 3 na comb hujabalance, hautachaguliwa serikalini bali shule binafsi utaenda kusoma mchepuo utakaofanana na masomo yako.
[ mfano: Civ-c, kisw-c, geo-c...unaweza fanya hgk ama hgl ama kozi nyingine hata kama english na history una d].

=>ukiwa na c 2 na d kadhaa(lets say 4 ya 26), hapa utaweza kwenda form 5 shule za private lakini utatakiwa utafute c ya 3 kw kureset wakati upo form 5. Same na c 1 you need to re-sit.

=> hapa sasa ndipo kwenye utata. Ukiwa na d 3, kiukweli sahau form 5 kama hauhitaji kurisit, sasa qualification hizi zina option zifuatazo:
1. Unahitaji kupiga long pass kwa kwenda chuo kwa ngazi ya certificates. Duraation ya hii kozi ni 1 year certificate. Sasa hapa kuna vyuo kadhaa vinavyotoa certificates. Hapa ni d za masomo yoyote yale basic(sina uhakika kama b/knwoledge na islam zinazingatiwa na ndio maana nasema d za basic subjects)
mfano: Unaweza kufanya certicates vyuo vya cbe-mambo ya biashara, ifm, tia, utumishi wa umma(public service) vyuo vya kilimo na ualimunk.
Nakozi nyingi tu wanatoa kwa certificates..mfano procurement, accounts, public admistration, recording, clearing and forwarding, social development, secretarial duties, education nk.

=> ukiwa na d 4 upo qualified kufanya ngazi ya certificate kama nilivyoanisha hapo juu.

=> ukiwa na d 5 sasa hapa wewe umeula!! Hapa unaruhusiwa kabisa kufanya basic diploma katika vyuo vyote wanavyotoa duploma. Kwa mfano vyuo hivyo nilivyovitaja hapa juu, chukua form yako kwa maringo achana na biashara ya kurisit omba kozi ya diploma, teana kama una d ya hesabu na english ndo inakuwa rahisi zaidi kuchukuliwa.

=> kwa wale waliosoma mahesabu kuna vyuo vingine kama dit(daar institute), ait(arusha inst) na mbeya tech msishau kufanya maombi, na kwale waliopiga fresh biology with minimum of d angalieni option za nursing ni nzuri sana na katika vyuo vya matc na cotc.

kama kuna marekebisho yanakaribishwa na kama hoja ama daubt basi uwanja ndio huu. Most welcome!!

Update:


2i9m911.jpg

jidhjp.gif
mkuu utaratibu wa kuwa form 5 at the same time unarisit ulisha badilishwa kitambo na wizara kwanza una clear then unaendelea labda kama mtu nafanya ivo kimagamashi,take my note
 
mkuu utaratibu wa kuwa form 5 at the same time unarisit ulisha badilishwa kitambo na wizara kwanza una clear then unaendelea labda kama mtu nafanya ivo kimagamashi,take my note
Thanks ila ukiangalia vizuri kwenye bandiko langu nimeweka updatee, ulichokiandika ww ndio kipo kwenye update hapo juu by structuralist
 
Last edited by a moderator:
nashukuru kwa ufafanuzi wako mzuri. ila bado nahitaji ufafanuzi zaidi. je ukiwa una pass 3 unaweza kusomea kozi zipi na vyuo gani wanachukua wenye pass 3..? mimi nina C 2 na D 2. C1 ya dini ndio maana nikasema nina pass 3. pls nijuze.
 
Msaada kwa anaefahamu chuo cha utumishi tawi la Mtwara kilipo naitaji kwenda kusoma uko.
 
Njoo mjini wenyew utatukuta wa Gas City
 
Panda gari za mtwara hadistand kuu ya mtwara then unaweza kuchukua bodaboda, bajaza ama tax na ni mwendo wa kama dakika 7 hadi 10 kutoka stand kuu
 
asante! nategemea mwez wa kwanza ntakuwa uko, unaweza kuniambia gharama za hostel au kupata chumba
 
Mara nyingi chumba mtwara cha kawaida hakizidi 30,000 na kwa hostel nitakujulisha subr nifanye utafiti
 
Back
Top Bottom