Mkuu, mbona kupigwa tunapigwa wote hata tunaoelewa lugha kwa confidence kidogo?
Kitu kingine cha kufanya ni money management ili ukipigwa uweze ku revenge.
Kuna siku nilianza na $1700,nikapigwa nikabaki kama na $800 nikaona ujinga huu, nikafunga position, nika reverse trend.
Pair ya AUD/USD pasua kichwa hiyo, unaweza kufanya research zako zote vizuri halafu ikaenda vizuri sana, inaporomoka vibaya sana katika dakika tano tu na kukuharibia hesabu zako zote
Hapo inabidi ujue kitu kinaitwa "kubadilisha gia angani", nikabadilisha gia.
Nikapiga ile $800 iliyobaki, katikakipindi kama cha wiki mbili ikafika just shy of $10,000. Nikawa nimefikia goal langu nikatoa hela kwenye akaunti nikazirudisha benki yangu, nikapumzika siku mbili tatu, nikaanza kutrade upya sasa hivi narudia mchezo vile vile slow but sure.
Sasa hapo utaona umuhimu wa strategic trading, kwamba trades zako zikae kwamba hata ukiliwa, uwe na strategy ya ku revenge ama kwa stop loss ama kwa kuweka trade nyingine against ya kwanza.
Hata wenye uzoefu yanawakuta haya, yakikukuta inawezekana yakakukuta sana kwa sababu huna uzoefu, lakini nature ya hizi habari ni kama kutabiri hali ya hewa, unaweza kubeba mwamvuliwiki nzima mvua isinyeshe, ukisema tu "haijanyesha wiki nzima, leo nitoke bila mwamvuli unaniletea mzigo tu" ndiyo siku mvua inayonyesha.