Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kama vile samaki anavyohitaji maji ili aishi vivyo hivyo fisadi huitaji
ufisadi ili aishi na kufanikiwa. Kumtoa fisadi kutoka ufisadi ni sawa na
kumtoa samaki kwenye maji ukidhania unamuokoa. Lakini samaki huvuliwa ili kugeuzwa mlo na siyo mapambo!
Wapo wengine hufanya uvuvi kama mchezo; wenyewe wanaita sport fishing ambapo samaki hutolewa kwenye maji, anaachwa anatapatapa halafu anarudishwa majini kuendelea kuishi. Ukiniuliza mimi hivi ndivyo ninavyoona mchezo wa CCM na ufisadi - Sport Corruption.. ambapo mafisadi huchezewa chezewa, hupewa chambo, hunaswa na kutolewa majini na watu wanashangilia. Lakini kabla hawajafa kwa kukosa oksijeni hurudishwa majini ambapo huruka ruka kwa furaha huku wananchi wakisubiri waone nani mwingine atavuliwa.
Kumbe hatuhitaji wavuvi wa michezo tunataka wale wenye kuvua samaki ili kuwageuza kitoweo. Hawa wanafuata kanuni asili ya mababu kuwa "usivue samaki ambaye hutaki kumla" (msiniulize mababu walisema lini hilo).
Tunahitaji viongozi wapya ambao hawatakuwa na muda wa mchezo na mafisadi bali watawakaanga na kuwageuza geuza katika jungu kuu la sheria huku mafuta ya ushahidi yakizidi kumiminwa juu yao.
ufisadi ili aishi na kufanikiwa. Kumtoa fisadi kutoka ufisadi ni sawa na
kumtoa samaki kwenye maji ukidhania unamuokoa. Lakini samaki huvuliwa ili kugeuzwa mlo na siyo mapambo!
Wapo wengine hufanya uvuvi kama mchezo; wenyewe wanaita sport fishing ambapo samaki hutolewa kwenye maji, anaachwa anatapatapa halafu anarudishwa majini kuendelea kuishi. Ukiniuliza mimi hivi ndivyo ninavyoona mchezo wa CCM na ufisadi - Sport Corruption.. ambapo mafisadi huchezewa chezewa, hupewa chambo, hunaswa na kutolewa majini na watu wanashangilia. Lakini kabla hawajafa kwa kukosa oksijeni hurudishwa majini ambapo huruka ruka kwa furaha huku wananchi wakisubiri waone nani mwingine atavuliwa.
Kumbe hatuhitaji wavuvi wa michezo tunataka wale wenye kuvua samaki ili kuwageuza kitoweo. Hawa wanafuata kanuni asili ya mababu kuwa "usivue samaki ambaye hutaki kumla" (msiniulize mababu walisema lini hilo).
Tunahitaji viongozi wapya ambao hawatakuwa na muda wa mchezo na mafisadi bali watawakaanga na kuwageuza geuza katika jungu kuu la sheria huku mafuta ya ushahidi yakizidi kumiminwa juu yao.