Fikiria leo hii Lowassa angekuwa Rais!

Fikiria leo hii Lowassa angekuwa Rais!

Sipendi hata kufikiria maana ingekuwa zero kabisa,hana ubavu kuyafanya haya ambayo yanafanyika,angekuwa karidhika baada ya tamaa yake na ufisadi wake kumfikisha ikulu,kwanza angelikuwa na mkutano mkubwa na mafisadi wenzake,na kuanza kulipa visasi
 
Kama tungemchagua Lowassa kuwa Raisi wa wa 5 wa JMTZ unafikiri mpaka sasa hivi ni nini kingekuwa kimetokea? Unafikri wagonjwa Muhimbili wangetoka sakafuni na kuhamia kitandani? Unafikiri Lowassa, Mbowe Lisu &Co. wangeacha kutumia milioni 250 na badala yake kuzipeleka Hospitali kusaidia Watanzania? Rejea Tundu Lissu kutetea milioni karibia 300 walizokuwa walipwe kama Wabunge, je angeziacha hizi za juzi kama angekuwa na madaraka?

Unafikiri Lowasa na Mbowe wangeahirisha kuuza sura Disemba 9 na badala yake kutumia hizo fedha kwa ajili ya maendeleo?
Unafikiri Lowassa na Mbowe wangefuta safari za nje ya nchi?

Mke wa Lowassa unafikiri leo hii angekuwa kimya kama mama Janeti au tayari angeshaanzisha NGO na sia ajabu sasa hivi angekuwa yuko safari ndefu ya Marekani na Ulaya kuuza wazo lake?

Mungu bado hajachoka na sisi Watanzania anatupenda na ndiyo maana ametuongoza na tukafanya maamuzi ya busara, leo hii ukiwauliza waliompigia kura Dr. Pombe Magufuli kama wana majuto yoyote ya kufanya jibu lake ni HAPANA kubwa!
Hahaha
Sijui na bomoa bomoa kama ingetukumba
 
Sipendi hata kufikiria maana ingekuwa zero kabisa,hana ubavu kuyafanya haya ambayo yanafanyika,angekuwa karidhika baada ya tamaa yake na ufisadi wake kumfikisha ikulu,kwanza angelikuwa na mkutano mkubwa na mafisadi wenzake,na kuanza kulipa visasi
mbona mnahangaika sana na Lowasa kwani yeye ndo raisi?Lowasa ataendelea kuwanyima usingizi sana
 
Kiukweli ilitaka moyo kumuelewa Lowassa alikuwa anataka kuifanyia nini Tanzania. Haeleweki kabisa alikuwa ana ajenda gani! Cha ajabu ni pale aliposema, "Watanzania wanipe tu mandate halafu wataona maajabu, nakuapia wallah"....Aaah! Huyu babu vepe? Anatufanya Watanzania wote ni Manyumbu! Eleza mikakati yako babu...usituletee habari za kuonewa hapa.
Kiukweli ilitaka moyo kumuelewa Lowassa alikuwa anataka kuifanyia nini Tanzania. Haeleweki kabisa alikuwa ana ajenda gani! Cha ajabu ni pale aliposema, "Watanzania wanipe tu mandate halafu wataona maajabu, nakuapia wallah"....Aaah! Huyu babu vepe? Anatufanya Watanzania wote ni Manyumbu! Eleza mikakati yako babu...usituletee habari za kuonewa hapa.
 
Lowasa kachanganyikiwa. Kila kick anayoshikilia inabuma mapema
ungekuwa unahangaika na kazi yako kama unavyohangaika na Lowasa ungefanikiwa Sana. Lowasa ni mti wenye matunda mema kurushiwa mawe ni kawaida endeleeni na majungu yenu Lowasa atabaki kuwa hazina ya taifa
 
Rais Dr. John Pombe Magufuli aliuliza hilo swali Ikulu wakati wa mkutano aliouitisha na wafanyabiasha. Edward Lowassa ameyasema hayo kwa nyakati tofauti. Mwanza wakati w msiba wa aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo na juzi januari mosi akiwa Monduli.
Watanzania bado tunahitaji kujiuliza nani tunamhitaji tena 2020?
Tusiwe Mazuzu, Tusijifanye vipofu, tusiweke pamba masikioni na kujifanya viziwi.
 
Mleta mada huwa hajielewi! Hivi isingekatwa Lowasa na cc Magufuli angepita? Kumbuka JPM kapita baada ya kuona turufu inaenda kwa Membe.Lowasa kwa ilani ya CHADEMA,mpaka sasa Mafisadi kama Joka la makengeza Lingekua ndani.Alisema atamwachia Ponda na sasa yuko huru.Hivyo usimpuuze huyu mtu ni mhimu kuliko wewe kwenye hili Taifa.
 
kama unafurahi na kushangilia yanayofanywa na jpm, huku ukishukuru el kuukosa urais. Huna budi kumshukuru na kumpongeza chinjachinja jk kwa kumkata el huku akimwangalia usoni.
 
hahahahahha...kumbukeni maigizo haya yako ndani ya siku sitini tu sasa

Hakuna mabadiiko yoyote kutoka CCM...I can assure you fellows
 
Ww mleta acha kutibua watu SAA hiz, mafisadi mmjezana hapo Lumumba , lowasa angekuwa rais kuanzia vijinin wangeshaanza kupata huduma bora za afya, na mwakan hakuna mwanafunz angeagizwa mchango, na angeshakomoesha mgao wa umeme tungeanza kufurahia umeme wa gesi
ukiwauliza watu wa lumumba kwa hadi sasa kuna changes gani...watabaki wanapiga porojo tu

Serikali ya leo kila mtu anabaini
 
haya tunamhitaji magufuli...una jipya tena?

But kumbuka...he is your last Card
 
Mnajitahidi sana vijana wa lumbumba kushindana na lowasa

Ila tambueni lowasa ni mgodi unaotembea hauwishi madini

Na kingine hata huyo magufuli anajitahidi kuzima upendo wa lowasa kwa watanzania

Na ndiyo maana anakurupuka tu
 
Back
Top Bottom