Fikiria leo hii Lowassa angekuwa Rais!

Fikiria leo hii Lowassa angekuwa Rais!

Kwa nyakati tofauti Lowassa na viongozi wengine wa chadema wamekuwa wakitoa kauli kuhusu Wafanyabiashara wakubwa , kauli ambazo hapana shaka , endapo Chadema wangefanikiwa kuunda serikali chini ya Edward Lowassa, basi kwenye upande wa kukusanya kodi wafanyabiashara wakubwa wasingeguswa kabisa au kungekuwa na hali kuwanyanyasa wale wafanyabiashara ambao wangeonekana kutokiunga mkono chama hicho.
1. Juzi alikaririwa na vyombo vya habari kutoka Monduli akisema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa maelekezo ya Serikali imekuwa ikiwatoza kodi kubwa Wafanyabiashara kwa sababu waliifadhili Chadema kwenye kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Kauli kama hii pia aliitoa jijini Mwanza akiwa kwenye msiba wa aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema wa mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo.
2. Wakati wa harambee ya CHADEMA iliyofanyika septemba 22 mwaka jana , mwenyekiti wa Chamahicho, Freeman Aikaeli Mbowe alisema kulikuwa na matajiri watano wenye uwezo wa kiuchumi ambao walikuwa tayari kukisaidia kwenye shughuli zake za kampeni lakini hawataki kutajwa majina yao kwa hofu ya kufuatiliwa na vyombo vya dola.

TAFAKURI:
1. Ni wazi kabisa Lowassa angekuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania asingeweza kabisa kuwabana Wafanyabiashara wakubwa katika swala zima la kukusanya kodi hasa ukizingatia kuwa walikifadhili chama hicho. Aidha dhana ya kwamba wafadhili wa Chadema wananyanyaswa na TRA ni uthibitisho kwamba hizi ni hisia ambazo alifikiria kuwafanyia wale wafanyabiashara ambao wasingejitokeza kukifadhili chama chake na kufikiria kuwa Serikali ya JPM nayo ina mawazo ya kipuuzi kama hayo. MAGUFULI siyo mtu wa visasi kama LOWASSA.
2. Lowassa kusema kwamba siyo suala la kutaja majina ya wafanyabiashara wanaonyanyaswa bali CCM ifanye utafiti(Reseach) ni makosa na pengine labda hajui wakati gani na nani wa kufanya utafiti. Serikali ya CCM ndiyo anayoituhumu kuwanyanyasa wafanyabiasha waliofadhili Chadema. Kwa mantiki hiyo CCM kama mtuhumiwa hawezi kufanya utafiti. LOWASSA na CHADEMA yake ndiyo waathirika na kwa maana hiyo wao ndiyo wanawajibika kufanya utafiti kama wamekurupuka kuyasema haya bila kufanya hivyo au kama wamefanya utafiti na kujiridhisha, wanawajibika kutaja majina hayo ili Umma kuujua ukweli.
3. Kikubwa kabisa. Zama za kukumbatia Wafanyabiashara kwa sababu tu ya ufadhili wao kwa vyama vya siasa zimepitwa na wakati. LOWASSA anapaswa kuona AIBU kutamka maneno kama ufadhili wa wafanyabiashara kwa vyama siasa kwani yanazidi kurutubisha UFisadi wake wa tangu enzi na enzi. Lowassa anataka kutuambia wafanyabiashara wanaonyanyaswa ni akina nani? ROSTAMA AZIZ na kundi lake au wale Wafanyabiashara watano wakubwa kiuchumi ambao Mwenyekiti alisema wanaogopa kutajwa majina yao? AIBU HII.

Kinachotakiwa tu ni kufuata sharia za nchi na sharia za kodi, hawa wanasiasa waache blaa blaa siasa zimeisha. Unapofuatwa kulipa kodi kinachotakiwa kufanya ni kuthibitisha umelipa kodi stahiki na sio vinginevyo. Hata tunaofanya kazi kwenye - Makampuni makubwa TRA wanafanya hivyo hivyo. Tatizo la wafanya biashara wetu wanafanya biashara kisanii sanii. Hata anayeuza bia tu/soda hajui kwamba VAT - 18% ni kodi ya serikali. Walipe tu au wathibitishe kama wamelipa na sio kuanza blaa blaa kupitia wanasiasa.
 
Ikumbukwe kuwa pia Lowassa aliwanyanyasa wafanyabiashara ambao hawakuisapoti ccm wakati yeye na kikwete wanaingia madarakani 2005, kwahiyo naunga mkono hoja coz inawezekana kutokana huyu jamaa ni mtu wa visasi sana inawezekana alipanga kuwanyanyasa wafanyabiashara ambao hawakuinga mkono cdm.

Sumaye pia aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari akiwa moshi akisema wafanyabiashara wanaotaka mambo yawanyookee wajiunge ccm. Kwahiyo kutokana wao wenyewe walikuwa mamafia lazima wawe na hisia hizoy
 
Serikali imchunguze huyo Lowasa. Tuliambiwa kuwa Lowasa ni tajiri mkubwa ijapokuwa sioni utajiri wake. Inawezekana ana biashara za magendo ambazo halipii kodi
Huyu inawezekana ndiye mmiliki mkuu wa makampuni yanayokwepa kodi.
 
Hili mbona lipo wazi sana maana Lowasa mwenyewe anaongoza kwa kukwepa kodi kwenye biashara zake.
 
Serikali imchunguze huyo Lowasa. Tuliambiwa kuwa Lowasa ni tajiri mkubwa ijapokuwa sioni utajiri wake. Inawezekana ana biashara za magendo ambazo halipii kodi
Zipo tarifa kuwa anajihusisha na biashara haramu pia kwahiyo ipo haja amulikwe vizuri sana.
 
Serikali imchunguze huyo Lowasa. Tuliambiwa kuwa Lowasa ni tajiri mkubwa ijapokuwa sioni utajiri wake. Inawezekana ana biashara za magendo ambazo halipii kodi
we ni mpuuzi sana huishi kusema chademaaa,lowasa.uchaguzi umeisha bado tu chademaa,lowasa.omba ushauri kwa mumeo kabla ya kupost ujinga humu usiishi kama mkwere
 
Naona mnaanzisha uzi na kushambulia wenyewe.
 
Ikumbukwe kuwa pia Lowassa aliwanyanyasa wafanyabiashara ambao hawakuisapoti ccm wakati yeye na kikwete wanaingia madarakani 2005, kwahiyo naunga mkono hoja coz inawezekana kutokana huyu jamaa ni mtu wa visasi sana inawezekana alipanga kuwanyanyasa wafanyabiashara ambao hawakuinga mkono cdm.

Sumaye pia aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari akiwa moshi akisema wafanyabiashara wanaotaka mambo yawanyookee wajiunge ccm. Kwahiyo kutokana wao wenyewe walikuwa mamafia lazima wawe na hisia hizoy
Hahahahahahahaha.......kama ndiyo hivyo basi wapigwe tu tena magufuli aanze na Lowasa mwenyewe maana tumechoka hakuna namna nyingine.
 
Mheshimiwa lowassa,no research no right to speak. Mambo mengine mzee ungeturia itafikia point utaanza kupelembwa kwa uliyofanya nyuma kinyume na utaratibu.
No perfect men.
Uchaguzi umekwisha tujenge nchi.
 
Lowassa hajitambui yuko upande upi wa siasa.. Taratibu anaanza kututhibitishia kuwa hakuwa aseti...!!
 
Lowassa hajitambui yuko upande upi wa siasa.. Taratibu anaanza kututhibitishia kuwa hakuwa aseti...!!
Wengine tulijua mapema ndiyo maana tulimpinga mwanzo mwisho hafai kwa lolote anaweza ufisadi tu basi lakini haya mengi ya kutumikia watu siyo kazi yake.
 
Hiyo Lowasa mzee wangu kigeugeu sana, haaminiki anataka nini na kama hatajirrkebisha atazidi kupotea, atulizane ajenge hoja zake kisayansi kuliko kukurupuka
 
Nyinyi mabaradhuli na mafedhuli Tumewaacha mtawale. Kodi Kodi escrow hamzungumzii na huko hazina
 
Kwani kwenye utawala huu JPM wafanyabiashara wakubwa wangapi wameshaguswa mpaka sasa?
 
sijui kwanini huyu mzee hataki kukubaliana na hali halisi kwamba muda wake umeisha. atulie kabisa, kama kuna alichochuma akiwa ujanani akale tu kwa utulivu. kuna uzi humu uliuliza kwamba hivi huyu mzee alichumia juani na sasa ni muda wa kulia kivulini au kinyume chake? ni wazi kwamba uwezo wa kuogelea umemwishia ila analazimisha kujitupa majini sasa ona anavotapatapa. nawaza tu kwa sauti kwamba,
1. hivi inawezekana kweli huyu mzee kaishiwa uwezo wa kufikiri mpaka asijue faida ya kutoza kodi kikamilifu kwa ajili ya ukuaji wa uchumi wa nchi hii?
2. huyu ndiye aliyetokwa mishipa majukwaani na kwenye media kwamba ana uchungu na hii nchi?
tukae kimya yatakuja mengi na kizuri kuliko vyote ni kwamba tutapata wasaa wa kuzijua rangi halisi za watu kama hawa.
 
sijui kwanini huyu mzee hataki kukubaliana na hali halisi kwamba muda wake umeisha. atulie kabisa, kama kuna alichochuma akiwa ujanani akale tu kwa utulivu. kuna uzi humu uliuliza kwamba hivi huyu mzee alichumia juani na sasa ni muda wa kulia kivulini au kinyume chake? ni wazi kwamba uwezo wa kuogelea umemwishia ila analazimisha kujitupa majini sasa ona anavotapatapa. nawaza tu kwa sauti kwamba,
1. hivi inawezekana kweli huyu mzee kaishiwa uwezo wa kufikiri mpaka asijue faida ya kutoza kodi kikamilifu kwa ajili ya ukuaji wa uchumi wa nchi hii?
2. huyu ndiye aliyetokwa mishipa majukwaani na kwenye media kwamba ana uchungu na hii nchi?
tukae kimya yatakuja mengi na kizuri kuliko vyote ni kwamba tutapata wasaa wa kuzijua rangi halisi za watu kama hawa.
 
Mafisadi na wakwepa kodi wangefurahi sana kwakuwa nimwenzao.
 
Back
Top Bottom