Fikiria leo hii Lowassa angekuwa Rais!

Fikiria leo hii Lowassa angekuwa Rais!

Lowasa angekua Rais mpaka leo angekua bado hajaanza kazi maana angekua kwenye ziara ya kila mkoa kushukuru... Maana anapenda Media kumzungumzia sana
 
mshukuru Mungu wako kwa Magufuli kutekeleza ilani na aliyokuwa akiyazungumza Lowassa nyie kila baada ya korasi ilikuwa hapa kazi tu au

Mkuu labda kama ulikua kwenye kampeni za somalia...ila kampeni zilizofanyika hapa nchini bwana Pombe alikua kinara kwenye majukwaa na alitumia muda mwingi kuongea na wananchi na inajulikana bwana pombe ndo alizunguka sehem kubwa zaidi ya nchi na kuzungumza mengi sana na wananchi wake...so nakuomba uwe unafikiri kabla ya kubwabwaja humu jukwaan
 
Kama tungemchagua Lowassa kuwa Raisi wa wa 5 wa JMTZ unafikiri mpaka sasa hivi ni nini kingekuwa kimetokea? Unafikri wagonjwa Muhimbili wangetoka sakafuni na kuhamia kitandani? Unafikiri Lowassa, Mbowe Lisu &Co. wangeacha kutumia milioni 250 na badala yake kuzipeleka Hospitali kusaidia Watanzania? Rejea Tundu Lissu kutetea milioni karibia 300 walizokuwa walipwe kama Wabunge, je angeziacha hizi za juzi kama angekuwa na madaraka?

Unafikiri Lowasa na Mbowe wangeahirisha kuuza sura Disemba 9 na badala yake kutumia hizo fedha kwa ajili ya maendeleo?
Unafikiri Lowassa na Mbowe wangefuta safari za nje ya nchi?

Mke wa Lowassa unafikiri leo hii angekuwa kimya kama mama Janeti au tayari angeshaanzisha NGO na sia ajabu sasa hivi angekuwa yuko safari ndefu ya Marekani na Ulaya kuuza wazo lake?

Mungu bado hajachoka na sisi Watanzania anatupenda na ndiyo maana ametuongoza na tukafanya maamuzi ya busara, leo hii ukiwauliza waliompigia kura Dr. Pombe Magufuli kama wana majuto yoyote ya kufanya jibu lake ni HAPANA kubwa!

JPM anafanya mambo ambayo wa Tz wengi tulitaka.swali la kujiuliza ni je haya yote yanafanyika katika mpangilio na utaratibu sahihi.sasa hivi imeanza kua ni showoff,sidhani kama kuna haja ya vyombo vya habari kujulishwa kua waziri amewafungia geti wafanyakazi waliofika kazini baada yake.
Kwa upande wa Lowassa sina shaka tungeshuhudia mabadiliko katika mpangilio mathubuti na yenye kunufaisha.ni mtu mwenye busara na aliyehitaji uongozi wa juu wa nchi hii kuisogeza Tz mbele kupitia njia anazoamini na alizotueleza wakati wa campaign.
Cha msingi ni kila mtu kufanya kazi anayotakiwa kufanya (Be responsible)..play your part and play it well.
Pia JPM tumuombee apate washauri wenye weledi na mapenzi mema na hii nchi ili dhamira yake ya kuivusha nchi hii iweze kutimia.
JPM ni mtu msafi mwenye malengo mazuri lakini ni dhahiri kua hawezi kufanya yote hayo bila tasisi,including ccm
EL peke yake alivyo ni taasisi kuna mambo mengi angeweza kuyafanya bila kuhitaji maelekezo
Tanzania ni moja muda wa kusakama viongozi wa upinzani au waliokua wakigombea urais umeisha.
JF tujadili masuala ya maendeleo.ama basi tunapochambua kuhusu wanasiasa tuache chuki pembeni penye ukweli tuweke ukweli.
 
Tanzania yetu ingekuwa inachungulia kaburi, pesa ya Watanzania wangekuwa wanaikomba kama vichaa. Dili za ufisadi tayari zingekuwa zimeisha ongezeka mara dufu
 
kwel bila lowasa na ukawa tz haitopata maendeleo kamwe,ukawa ndo njia pekee ya kuifikisha tz ktk ahadi ya milele,magu na ccm yake wanazidi kupalilia na kukaribisha laana na kuipa mizimu na kuzimu mamlaka ya kuendelea kulitafuna taifa,,.pole xana tz yangu ,,pole xana watz
 
WEWE acha hizo, hapa kazi tu hapa kazi tu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Tena walikuwa wamekwisha kugawana uwaziri na ss hvi kwao ingalikuwa ni kupongezana tu, hakika maombi ya watz Mungu aliyasikia na kutupatia kiongozi ambaye kwa sasa watz tunaanza kupata matumaini mapya na hii serikali, cha msingi ni cc kuwafichua wala rushwa ili na yy apate hamasa ya utendaji wake.
Wee wa ajabu kweli, mungu ameyasikia maombi au ni ubabe babu kubwa uliotumika, matumainingani unayapata wakati kwa serikali gani ileile ya mawaziri walewale waliokuwa na tuhuma zilezile. Hivi huko ccm hakuna watu, si angeomba tu watu wa ukawa! Unanichekesha kweli ndugu, serikali yako haiwajui wala rushwa? Inawajua fika na inawapa kazi kama walivyorudishwa mawaziri wenye tuhuma kazini. We funua kidomo chako useme fulani kala rushwa, weeeee, utajuta na hatua hazitachukuliwa! Magufuli alianza vizuri, na yule ni mpinzani wa ccm na mwana mabadiliko. Lakini katika mfumo walio nao wenzetu sio rahisi kuwageuka wenziwe akijua wazi wenye ccm ndio waliomweka pale. TUONE MBIO ZAKE! Na niyafurahi akifanya vema
 
Mungu bado anaipenda Tanzania. Salute to Lowassa lakini tumwache Jembe Magufuli aibadilishe Tanzania.
 
Falsafa mbili tofauti,kila mtu alitaka kulitumikia taifa.

Magufuli unapata elimu ukiwa kazini.

Lowassa utafanya kazi baada ya elimu.
 
Tena walikuwa wamekwisha kugawana uwaziri na ss hvi kwao ingalikuwa ni kupongezana tu, hakika maombi ya watz Mungu aliyasikia na kutupatia kiongozi ambaye kwa sasa watz tunaanza kupata matumaini mapya na hii serikali, cha msingi ni cc kuwafichua wala rushwa ili na yy apate hamasa ya utendaji wake.
Wee wa ajabu kweli, mungu ameyasikia maombi au ni ubabe babu kubwa uliotumika, matumainingani unayapata wakati kwa serikali gani ileile ya mawaziri walewale waliokuwa na tuhuma zilezile. Hivi huko ccm hakuna watu, si angeomba tu watu wa ukawa! Unanichekesha kweli ndugu, serikali yako haiwajui wala rushwa? Inawajua fika na inawapa kazi kama walivyorudishwa mawaziri wenye tuhuma kazini. We funua kidomo chako useme fulani kala rushwa, weeeee, utajuta na hatua hazitachukuliwa! Magufuli alianza vizuri, na yule ni mpinzani wa ccm na mwana mabadiliko. Lakini katika mfumo walio nao wenzetu sio rahisi kuwageuka wenziwe akijua wazi wenye ccm ndio waliomweka pale. TUONE MBIO ZAKE! Na niyafurahi akifanya vema
 
Angekua bado hajaanza kazi angekua yupo ziarani kuwashukuru watanzania kwa kumchagua
 
Kwa nyakati tofauti Lowassa na viongozi wengine wa chadema wamekuwa wakitoa kauli kuhusu Wafanyabiashara wakubwa , kauli ambazo hapana shaka , endapo Chadema wangefanikiwa kuunda serikali chini ya Edward Lowassa, basi kwenye upande wa kukusanya kodi wafanyabiashara wakubwa wasingeguswa kabisa au kungekuwa na hali kuwanyanyasa wale wafanyabiashara ambao wangeonekana kutokiunga mkono chama hicho.
1. Juzi alikaririwa na vyombo vya habari kutoka Monduli akisema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa maelekezo ya Serikali imekuwa ikiwatoza kodi kubwa Wafanyabiashara kwa sababu waliifadhili Chadema kwenye kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Kauli kama hii pia aliitoa jijini Mwanza akiwa kwenye msiba wa aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema wa mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo.
2. Wakati wa harambee ya CHADEMA iliyofanyika septemba 22 mwaka jana , mwenyekiti wa Chamahicho, Freeman Aikaeli Mbowe alisema kulikuwa na matajiri watano wenye uwezo wa kiuchumi ambao walikuwa tayari kukisaidia kwenye shughuli zake za kampeni lakini hawataki kutajwa majina yao kwa hofu ya kufuatiliwa na vyombo vya dola.

TAFAKURI:
1. Ni wazi kabisa Lowassa angekuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania asingeweza kabisa kuwabana Wafanyabiashara wakubwa katika swala zima la kukusanya kodi hasa ukizingatia kuwa walikifadhili chama hicho. Aidha dhana ya kwamba wafadhili wa Chadema wananyanyaswa na TRA ni uthibitisho kwamba hizi ni hisia ambazo alifikiria kuwafanyia wale wafanyabiashara ambao wasingejitokeza kukifadhili chama chake na kufikiria kuwa Serikali ya JPM nayo ina mawazo ya kipuuzi kama hayo. MAGUFULI siyo mtu wa visasi kama LOWASSA.
2. Lowassa kusema kwamba siyo suala la kutaja majina ya wafanyabiashara wanaonyanyaswa bali CCM ifanye utafiti(Reseach) ni makosa na pengine labda hajui wakati gani na nani wa kufanya utafiti. Serikali ya CCM ndiyo anayoituhumu kuwanyanyasa wafanyabiasha waliofadhili Chadema. Kwa mantiki hiyo CCM kama mtuhumiwa hawezi kufanya utafiti. LOWASSA na CHADEMA yake ndiyo waathirika na kwa maana hiyo wao ndiyo wanawajibika kufanya utafiti kama wamekurupuka kuyasema haya bila kufanya hivyo au kama wamefanya utafiti na kujiridhisha, wanawajibika kutaja majina hayo ili Umma kuujua ukweli.
3. Kikubwa kabisa. Zama za kukumbatia Wafanyabiashara kwa sababu tu ya ufadhili wao kwa vyama vya siasa zimepitwa na wakati. LOWASSA anapaswa kuona AIBU kutamka maneno kama ufadhili wa wafanyabiashara kwa vyama siasa kwani yanazidi kurutubisha UFisadi wake wa tangu enzi na enzi. Lowassa anataka kutuambia wafanyabiashara wanaonyanyaswa ni akina nani? ROSTAMA AZIZ na kundi lake au wale Wafanyabiashara watano wakubwa kiuchumi ambao Mwenyekiti alisema wanaogopa kutajwa majina yao? AIBU HII.
 
Serikali imchunguze huyo Lowasa. Tuliambiwa kuwa Lowasa ni tajiri mkubwa ijapokuwa sioni utajiri wake. Inawezekana ana biashara za magendo ambazo halipii kodi
 
Kwa nyakati tofauti Lowassa na viongozi wengine wa chadema wamekuwa wakitoa kauli kuhusu Wafanyabiashara wakubwa , kauli ambazo hapana shaka , endapo Chadema wangefanikiwa kuunda serikali chini ya Edward Lowassa, basi kwenye upande wa kukusanya kodi wafanyabiashara wakubwa wasingeguswa kabisa au kungekuwa na hali kuwanyanyasa wale wafanyabiashara ambao wangeonekana kutokiunga mkono chama hicho.
1. Juzi alikaririwa na vyombo vya habari kutoka Monduli akisema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa maelekezo ya Serikali imekuwa ikiwatoza kodi kubwa Wafanyabiashara kwa sababu waliifadhili Chadema kwenye kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Kauli kama hii pia aliitoa jijini Mwanza akiwa kwenye msiba wa aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema wa mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo.
2. Wakati wa harambee ya CHADEMA iliyofanyika septemba 22 mwaka jana , mwenyekiti wa Chamahicho, Freeman Aikaeli Mbowe alisema kulikuwa na matajiri watano wenye uwezo wa kiuchumi ambao walikuwa tayari kukisaidia kwenye shughuli zake za kampeni lakini hawataki kutajwa majina yao kwa hofu ya kufuatiliwa na vyombo vya dola.

TAFAKURI:
1. Ni wazi kabisa Lowassa angekuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania asingeweza kabisa kuwabana Wafanyabiashara wakubwa katika swala zima la kukusanya kodi hasa ukizingatia kuwa walikifadhili chama hicho. Aidha dhana ya kwamba wafadhili wa Chadema wananyanyaswa na TRA ni uthibitisho kwamba hizi ni hisia ambazo alifikiria kuwafanyia wale wafanyabiashara ambao wasingejitokeza kukifadhili chama chake na kufikiria kuwa Serikali ya JPM nayo ina mawazo ya kipuuzi kama hayo. MAGUFULI siyo mtu wa visasi kama LOWASSA.
2. Lowassa kusema kwamba siyo suala la kutaja majina ya wafanyabiashara wanaonyanyaswa bali CCM ifanye utafiti(Reseach) ni makosa na pengine labda hajui wakati gani na nani wa kufanya utafiti. Serikali ya CCM ndiyo anayoituhumu kuwanyanyasa wafanyabiasha waliofadhili Chadema. Kwa mantiki hiyo CCM kama mtuhumiwa hawezi kufanya utafiti. LOWASSA na CHADEMA yake ndiyo waathirika na kwa maana hiyo wao ndiyo wanawajibika kufanya utafiti kama wamekurupuka kuyasema haya bila kufanya hivyo au kama wamefanya utafiti na kujiridhisha, wanawajibika kutaja majina hayo ili Umma kuujua ukweli.
3. Kikubwa kabisa. Zama za kukumbatia Wafanyabiashara kwa sababu tu ya ufadhili wao kwa vyama vya siasa zimepitwa na wakati. LOWASSA anapaswa kuona AIBU kutamka maneno kama ufadhili wa wafanyabiashara kwa vyama siasa kwani yanazidi kurutubisha UFisadi wake wa tangu enzi na enzi. Lowassa anataka kutuambia wafanyabiashara wanaonyanyaswa ni akina nani? ROSTAMA AZIZ na kundi lake au wale Wafanyabiashara watano wakubwa kiuchumi ambao Mwenyekiti alisema wanaogopa kutajwa majina yao? AIBU HII.


HUYU MZEE ANAANZA KUTUDHALILISHA WANAUKAWA.SOTE KAMA WAPINZANI TUMEKUWA TUNASEMA SERIKALI YA CCM HAIKUSANYI KODI KWA WAKUBWA BALI KWA VIDAGAA.SASA MAGUFURI AMEANZIA JUU BASI KELELE ZIMEANZA.KODI ZIPO KISHERIA NA SHERIA HIZO ZILIPITISHWA NA BUNGE NA YEYE AKIWEMO.SASA KUNAHAJA GANI YA KUPISHA SHERIA KWA MBWEMBWE WAKATI HATUWEZI KUZISIMAMIA.PIA NAJUA UKIBANDIKIWA KODI KUBWA KULIKO UHALISIA KUNAKUKATA RUFAA.TATIZO UNAKUTA MTU ALIKKWEPA SANA MIAKA YA NYUMA KWA HIYO AKIAPEAL ANAGOPA MAKUBWA KUBUMBULUKA
 
HUYU MZEE ANAANZA KUTUDHALILISHA WANAUKAWA.SOTE KAMA WAPINZANI TUMEKUWA TUNASEMA SERIKALI YA CCM HAIKUSANYI KODI KWA WAKUBWA BALI KWA VIDAGAA.SASA MAGUFURI AMEANZIA JUU BASI KELELE ZIMEANZA.KODI ZIPO KISHERIA NA SHERIA HIZO ZILIPITISHWA NA BUNGE NA YEYE AKIWEMO.SASA KUNAHAJA GANI YA KUPISHA SHERIA KWA MBWEMBWE WAKATI HATUWEZI KUZISIMAMIA.PIA NAJUA UKIBANDIKIWA KODI KUBWA KULIKO UHALISIA KUNAKUKATA RUFAA.TATIZO UNAKUTA MTU ALIKKWEPA SANA MIAKA YA NYUMA KWA HIYO AKIAPEAL ANAGOPA MAKUBWA KUBUMBULUKA
Lowasa kachanganyikiwa. Kila kick anayoshikilia inabuma mapema
 
Ni wazi kabisa Lowassa angekuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania asingeweza kabisa kuwabana Wafanyabiashara wakubwa katika swala zima la kukusanya kodi hasa ukizingatia kuwa walikifadhili chama hicho.

Unamaanisha kua nayeye angewabana wale waliokifadhili CCM?
 
Back
Top Bottom