Fikiria leo hii Lowassa angekuwa Rais!

Fikiria leo hii Lowassa angekuwa Rais!

Kiukweli ilitaka moyo kumuelewa Lowassa alikuwa anataka kuifanyia nini Tanzania. Haeleweki kabisa alikuwa ana ajenda gani! Cha ajabu ni pale aliposema, "Watanzania wanipe tu mandate halafu wataona maajabu, nakuapia wallah"....Aaah! Huyu babu vepe? Anatufanya Watanzania wote ni Manyumbu! Eleza mikakati yako babu...usituletee habari za kuonewa hapa.
 
Kaka ni mapema mno kuyasema hayo. Ikulu hakuna pesa na ahadi za Magufuli zilikuwa nyingi mno, kama Ikulu kungekuwa na pesa sherehe ingefanyika na wagonjwa wangepata vitanda. Hata kule kufuta safari, sherehe n.k chimbuko lake kubwa ni kwamba Ikulu hakuna pesa kuko tupu kaka.
 
Kaka ni mapema mno kuyasema hayo. Ikulu hakuna pesa na ahadi za Magufuli zilikuwa nyingi mno, kama Ikulu kungekuwa na pesa sherehe ingefanyika na wagonjwa wangepata vitanda. Hata kule kufuta safari, sherehe n.k chimbuko lake kubwa ni kwamba Ikulu hakuna pesa kuko tupu kaka.

Wachache sn wenye uelewa huo mpk wanakela
 
Lowassa ni rais wa mioyo ya watanzania,alichaguliwa kwa asilimia 62,kama haujui,kwahiyo funga mdomo wako kama haujui chochote,na ujifikirie wewe mwenyewe na familia yako

Mbona hayuko ikulu?
Mleta uzi kasema UKWELI, na wewe tulia uone kazi maana Ile deal ya angani Ili fail,
Kama Lowassa angeshinda Sasa hivi tungekuwa bado sherehe baada ya sherehe. Tangia marangu hadi monduli , kuelekea bilkicanas club
 
Ngoja nikuambie moja moja.

Ni aibu Hospitali ya Taifa kupata vitanda mpaka zizuiwe pesa zilizochangiwa kwa tafrija ya Wabunge, zile pesa hazikuwa za mafungu ya serikali bali taasisi ndio zimechanga. Pamoja na jambo hilo kuwa zuri lakini ni aibu.

Ni sawa uchangiwe pesa za Harusi kisha useme kwa vile shemeji yake bwana Harusi ana familia kubwa na hana chakula wala pa kuishi basi hakuna sherehe fedha hizi zinakwenda kununua chakula chake na kumjengea kibanda.

Kuhusu 9 December, wewe unaamini huu ugonjwa Kipindupindu ndio unaweza kuahirisha Isifanyike ili pesa zitumike kufanya usafi?

Basi elewa sababu kubwa ni kuficha aibu ya kuja uwanjani Anayeitwa Rais wa Zanzibar ambaye alikuwa anangojewa kwa hamu ili lile lililotokea Bungeni liendelee. Na kwa vile pale hata umwite Ndugai hawezi kufua dafu kutuliza aibu hiyo ikaonekana ni bora kupotezea tuu.

Eti mama Lowasa hangeweza kutulia kama mama Janeth! Hilo naona niliache maana usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Yaliyo nyuma ya utulivu huo ungeyajua pengine usingepoteza muda wako kuandika.

Hata hivyo Magu anastahili pongezi kwa jinsi anavyoipopoa CCM bila kuitazama usoni kwa kutumia yaleyale waliyokuwa wanayasema wapinzani juu ya serikali kipindi cha awamu ya nne. Ameamua kuwasomesha namba mpaka hawana hamu kabisa. Sasa hivi hata wakitaka kwenda hapo Nairobi lazima kujaza fomu kama wanaomba mkopo wa biashara.
 
,lowasa ni rais wa mioyo ya watanzania,alichaguliwa kwa asilimia 62,kama haujui,kwahiyo funga mdomo wako kama haujui chochote,na ujifikirie wewe mwenyewe na familia yako

Lowassa si rais watz hiyo asilimia 62 mnayoisema ni 62% ya madereva wa bodaboda tu na si ya wapiga kura wote. Kwa Lowassa si raisi wa Tanzania kwa mioyoni kama unavyodai. Lowasa ni rais kwa madereva wa bodaboda pengine na wewe ni mmojawapo.
 
Ngoja nikuambie moja moja.
Ni aibu Hospitali ya Taifa kupata vitanda mpaka zizuiwe pesa zilizochangiwa kwa tafrija ya Wabunge, zile pesa hazikuwa za mafungu ya serikali bali taasisi ndio zimechanga. Pamoja na jambo hilo kuwa zuri lakini ni aibu. Ni sawa uchangiwe pesa za Harusi kisha useme kwa vile shemeji yake bwana Harusi ana familia kubwa na hana chakula wala pa kuishi basi hakuna sherehe fedha hizi zinakwenda kununua chakula chake na kumjengea kibanda.
Kuhusu 9 December, wewe unaamini huu ugonjwa Paulo Makonda aka Kipindupindu ndio unaweza kuahirisha Isifanyike ili pesa zitumike kufanya usafi? Basi elewa sababu kubwa ni kuficha aibu ya kuja uwanjani Anayeitwa Rais wa Zanzibar ambaye alikuwa anangojewa kwa hamu ili lile lililotokea Bungeni liendelee. Na kwa vile pale hata umwite Ndugai hawezi kufua dafu kutuliza aibu hiyo ikaonekana ni bora kupotezea tuu.
Eti mama Lowasa hangeweza kutulia kama mama Janeth! Hilo naona niliache maana usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Yaliyo nyuma ya utulivu huo ungeyajua pengine usingepoteza muda wako kuandika.
Hata hivyo Magu anastahili pongezi kwa jinsi anavyoipopoa CCM bila kuitazama usoni kwa kutumia yaleyale waliyokuwa wanayasema wapinzani juu ya serikali kipindi cha awamu ya nne. Ameamua kuwasomesha namba mpaka hawana hamu kabisa. Sasa hivi hata wakitaka kwenda hapo Nairobi lazima kujaza fomu kama wanaomba mkopo wa biashara.

Safi mkuu.
 
Kumbe unazungumzia mambo ya kufikirika! Kwa taarifa yako muhimbili ingekuwa kama st joseph ya Uingereza.
 
Kwanza angeanza na mikataba ya gesi ya mtwara ili kujimilikisha na jamaa zake pili watu maskini wangekosa pa kukimbilia tatu umeme ungetumia mafuta ya diesel
 
Hapa umenikumbusha jinsi Lowassa alivyotumia nguvu nyingi kukusanya pesa za sherehe za miaka 45 ya Uhuru akiwa Waziri mkuu. Ni wazi asingeweza kufuta sherehe za Uhuru. Tena ndio zingevunja rekodi ya matumizi.
 
Back
Top Bottom