oscarfilimbi1965
Member
- Jan 3, 2016
- 26
- 7
Sibonike acha kunichana mbavu zangu,kwamba ktk huo ukaguzi wa Chachandu mh kavua miwani usoni au kazilegeza ili iwe rahisi kuziona,Kwa kweli kuna vitu ambavyo havitamkiki kirahisi tena mbele ya kadamnasi ya watu au Waheshimiwa wabunge la nchi kubwa yenye watu wanaokadiriwa kufikia milioni Hamsini,inahitaji Kujichetua akili kidogo ili kuondoa aibu,ni kama kujamba ushuzi lazima ujiangalie uko wapi,jee hapa niuachie mzima mzima kwa kishindo au niubane bane,ila ukiona mtu anaachia ushuzi kwa kishindo mbele ya watu lazima ujiulize mara mbili mbili mwenzetu huyu vipi au ni kile Ki-baiskeli cha miguu mitatu ambacho watoto wakiona mwenzao kaletewa na wazazi wake basi nyie nyoote mnakidandia ili kukiendesha.