Muziki wa Bongo kuna kitu kimoja bado ni challenge sana.
Arrangement.
Wimbo unaweza kuwa na lyrics nzuri. Production nzuri. Sauti nzuri. Vionjo vizuri. Lakini ukikosa arrangement tu, unakisa mvuto.
Nilikuwa nasikiliza Michael Jackson's "Wanna Be Startin' Something", wimbo ulio katika album yenye mauzo mengi kuliko zote duniani nafikiri, Thriller (Thriller imefikisha "Diamond", which is better than "Platnum" in sales, yes, diamond and platinum are sales threshold). Nilipousikiliza wimbo ule, nikajiuliza, ni kwa nini umenikaa kichwani miaka 35 sasa tangu utoke, na ukipigwa unakufanya usisimke na utake kucheza. Nikagundua production ni nzuri, uimbaji ni mzuri, lyrics ni nzuri lakini vyote ni kawaida. Ila arrangement, kuanzia drums za kwanza mpaka mwisho Michael anavyowaimbisha watu "Mama se, Ma Mako Ma makosa", Michael alielewa anataka kufanya nini na kafanya arrangement ya wimbo kama ana chireograph dance move. Chombo gani kitaanza, kipi kitafuatia, chorus itakaa wapi, itajirudia mara ngapi, bassline litaendaje, litakata wapi kuachia vyombo vingine, hirns zitaenda wapi, zitakaa vipi zisiingilie vyombo vingine, Michael atapagawisha vipi, atashirikisha wengine vipi, atamalizia vipi wimbo.
Kila kitu kimepangwa kwa detail sana. Na unaweza kuona watu wamepangua vingi mpaka kufikia hapo.
Sisi tunaenda studio huku tunaangalia muda wa studio kwa bajeti, producer akikupigua beat ya kwanza ndiyo hiyo hiyo. Hakuna hata muda wa kujadili.
Hata kama kila instrument imepigwa vizuri, lyrics nzuri, uimbaji mzuri, bila arrangement wimbo unaboa.