Fatma Maghimbi huyoooooo!

Fatma Maghimbi huyoooooo!

Let Conservative leave for Reberal Democratic to take place,it could be bad at that time 1995, today a young of 15yrs(1995) that time is ready to be a member of parliament, on her chance, no lose to loose the lost ideas.
Peoples!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!POWER!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Waache wakimbilie Titanic. This time hakutakuwepo boti za kuwakomboa.
 
Siasa ajira....a.k.a usaliti kwa wananchi..
 
Inasikitisha. Sijui nini kimempata Mama Maghimbi sikutegemea. lakini siwezi kutoa hukumu kwani huko CUF sikujui vizuri.
 
alitoswa kwenye ubunge kwenye jimbo lake la chakechake huko pemba, may be alianza kutengwa kwenye chama maana hata hakuwa akisikika kabisa kama 1995-2005, ubunge wa 2005-2010 naona alikuwa yupoyupo tu
 
Kila mfugo utarejea zizini this tyme.
Zama za hatari hizi. wanatumia majeshi yao ya akiba.
yataisha na kubakia mabua pekee
 
Wanasiasa wote hapa Tanzania wanaangalia matumbo yao na familia zao, hivyo sioni ajabu kwa huyu mama ambaye alisha wahi kuwa mkuu wa kambi ya upinzani bungeni kwenda CCM na kuwaponda wapinzani.
Na wala siku ikitokea Hamad Rashid au Zitto au Dr Slaa kwenda CCM sitashangaa. Na ikitokea siku ccm ikatoka madarakani upinzani ukachua serikali pia sitashangaa kina Ngeleja, Lowassa na wengineo kwenda chama kilichochukua madaraka
 
Haya ndiyo matunda ya Muafaka baina ya CCM na CUF, hivyo CCM wanavuna walichopanda CUF....
 
Inasikitisha. Sijui nini kimempata Mama Maghimbi sikutegemea. lakini siwezi kutoa hukumu kwani huko CUF sikujui vizuri.
alishindwa kura za maoni, na chama hakina ulaji kama ccm... angefanya nini na yeye anahitaji mlo?
 
alishindwa kura za maoni, na chama hakina ulaji kama ccm... angefanya nini na yeye anahitaji mlo?

Mkuu Acid !,
Simtetei Mama Maghimbi,Lakini Mimi kama walivyo wengi hapa nimeshangazwa sana na Mama huyu kuondoka CUF na kurudi CCM.Kati ya Viongozi wa vyama vya Upinzani niliokuwa nawaamini kutokana na michango yao Bungeni na kwenye Majimbo yao ni pamoja na Mwanamama huyu ambaye kwa Taaluma ni mwanasheria.

Mama Fatma Mussa Maghimbi (64) alikuwa ni Mwanzilishi wa Chama cha CUF,na ana uhusiano wa karibu na Katibu Mkuu wa Chama hicho Seif Sharif Hamad.Mama huyo ambaye ameolewa Bara,na Mmoja wa Waanzilishi wa Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro Mzee Mussa Y.Maghimbi aliingia CUF mwaka 1992 na amekuwa Mbunge wa Chake chake (Mkoa wa Pemba Kusini) toka mwaka 1995.Kabla ya hapo Mama huyo alikuwa mfanyakazi wa Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam toka mwaka 1971.

Pamoja na mambo mengine Mama Maghimbi amekuwa mshiriki wa moja kwa moja wa siasa za Pemba na haswa CUF pamoja na kwamba muda wake mwingi anautumia Dar-es-salaam anakoishi na familia yake,yeye pamoja na Prof.Haroub Othman (RIP) na Mzee Hassan Said ni waanzilishi wa Zanzibar Legal Services Centre (ZLSC),Taasisi inayotoa ushauri na huduma za kisheria bure kwa watu wasio na uwezo,katika vipindi tofauti Mama Maghimbi amekuwa kiongozi wa Upinzani Bungeni na pia amekuwa Waziri Kivuli wa Mambo ya Katiba na Sheria.

katika kura za Maoni za CUF zilizofanyika mwezi Mei Mama Maghimbi pamoja na Wabunge wengine 11 walishindwa katika kura za maoni.Inawezekana kuwa Mama Maghimbi kahama CUF kwa sababu za kutofautiana na sura mpya za sasa zilizopo CUF,ambako kumejaa vijana wengi wenye damu ya mabadiliko ya haraka.
Mama Maghimbi amesoma sheria Chuo Kikuu cha D'salaam mwaka 1989 na baadaye kusoma shahada ya pili ya sheria Warwick, England mwaka 1994.Mama Maghimbi ana watoto 3.
 
WAKATI huyu mama akiwa kiongozi wa upinzani bungeni,it was about this time upinzani ulikuwa toothless,na lawama alitupiwa yeye cause she was not up to the task.On her move to CCM hii no opportunist venture na endapo CCM ikishinda anataka a share of the spoils which in the really sense she is not entitled-POLITICS SUCKS!!!!!!!
 
Waungwana wasiomjua Bi Fatma hawakuni kichwa kwani ni mtu alietumia miaka yake kumi na tano ya Ubunge wa ke huko Pemba kuwaambia Wapemba kuwa Watu wa Bara ni wabaya yeye kaolewa nao na anawajua na alitumia maneno haya kwenye kampeni zake kuwagombanisha watu wa bara na visiwani kwa maslahi yake ya kisiasa , tusubiri sasa ameingia CCM kwani alikua akiwahutubia wana CUF na kuwaambia CCM ni wauwaji wa Wapemba na Wazanzibari sijui leo vipi bibi huyu anakula matapishi yake na kuingia CCM tusubiri tumsikie .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom