Fatma Maghimbi huyoooooo!

Katika vitu ambavyo sitakaa nifanye katika maisha yangu ni kusema kitu hiki leo tena dunia nzima ikinisikiliza halafu kesho kufanya tofauti kabisa na maneno yangu ya jana. To me this is so embarassing, kweli hata watoto wangu watanishangaa sana. iweje majority ya wanasiasa wanaishi kwa uongo tena uongo mkubwa sana ina maana they have no one from their family to tell them this is not right ama kila mtu huku Tz anaona uongo ni sawa?


Ukweli ni kwamba it is easy for them to be so, kwa sababu kwao siasa ni kama mchezo wa kuigiza..leo anaeza kuigiza kama polisi ..kesho akaigiza kama jambazi..na hii yote inasababishwa na njaa (kujaza viriba-tumbo). Kama wanasiasa wengi wangekuwa wanachukulia siasa kama it is something this nation depends on it, tungekuwa na very challenging system, si tu kutoka upinzani, bali hata kutoka kwene chama tawala. It is sad ndio tulipo na hii ndio pool ya watu tulionao.
 
mwenda tezi na omo hurejea ngamani

wale wote walioapa na kuahidi watakilinda mpaka kufa hawawezi kihama

hata slaa ni wetu is A matter of time
 
Sasa turudi na tuwatazame wanasiasa waliondoka CUF, nyinyi ndio mtaniambia ni nani na nani ndio walioendelea mbele katika hayo waliyoyafatia huko walikokwenda.
Mapalala, Michael Nyaruba, Shaibu Akwilombe, Tambwe Hiza, Wilfred Lwakatare, Aliekuwa mbunge wa Kigamboni, Pro. Abdalla Safari, Naila Jidawi, Salim Msabah, na wengine marehemu siwataji (mungu awe radhi nao) n.k
kuondoka kwao mimi sioni kama ni pigo kubwa sana kwa Chama, in fact ni changamoto ambazo chama lazima ikutane nazo na ioneshe uwezo wa ku-zi handle. Huo ndio upevu wa kisiasa.Mpooo CUF zindabaad. Viva CUF ,Viva Tanzania Viva WaTanzania Aluta continue...!!!:yield:
 
LOOOOOOOOOOOOOOOOOOO!
Licha ya umri wake, ila nisingejali iwapo angekuwa amefunnga ndoa na mume mwingine au kupata ujauzito. Lakini hili; abarikiwe hakika kazi tunayo!
 
Kwa nini wamerudishia kadi Kawe? mimi nigedhani ingekuwa vyema huyu mama angefanya hivyo Pemba! Au ndiyo anahamia kwa machogo?

Amandla.....
 
Kwani naye alikuwa mpinzani au ndio vile vibandiko tulivyovizoea ambavyo vinawekwa kila sehemu kudanya watu wengine?
 
Mkuu Acid !,
Simtetei Mama Maghimbi,Lakini Mimi kama walivyo wengi hapa nimeshangazwa sana na Mama huyu kuondoka CUF na kurudi CCM.Kati ya Viongozi wa vyama vya Upinzani niliokuwa nawaamini kutokana na michango yao Bungeni na kwenye Majimbo yao ni pamoja na Mwanamama huyu ambaye kwa Taaluma ni mwanasheria.

Mama Fatma Mussa Maghimbi (64) alikuwa ni Mwanzilishi wa Chama cha CUF,na ana uhusiano wa karibu na Katibu Mkuu wa Chama hicho Seif Sharif Hamad.Mama huyo ambaye ameolewa Bara,na Mmoja wa Waanzilishi wa Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro Mzee Mussa Y.Maghimbi aliingia CUF mwaka 1992 na amekuwa Mbunge wa Chake chake (Mkoa wa Pemba Kusini) toka mwaka 1995.Kabla ya hapo Mama huyo alikuwa mfanyakazi wa Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam toka mwaka 1971.

Pamoja na mambo mengine Mama Maghimbi amekuwa mshiriki wa moja kwa moja wa siasa za Pemba na haswa CUF pamoja na kwamba muda wake mwingi anautumia Dar-es-salaam anakoishi na familia yake,yeye pamoja na Prof.Haroub Othman (RIP) na Mzee Hassan Said ni waanzilishi wa Zanzibar Legal Services Centre (ZLSC),Taasisi inayotoa ushauri na huduma za kisheria bure kwa watu wasio na uwezo,katika vipindi tofauti Mama Maghimbi amekuwa kiongozi wa Upinzani Bungeni na pia amekuwa Waziri Kivuli wa Mambo ya Katiba na Sheria.

katika kura za Maoni za CUF zilizofanyika mwezi Mei Mama Maghimbi pamoja na Wabunge wengine 11 walishindwa katika kura za maoni.Inawezekana kuwa Mama Maghimbi kahama CUF kwa sababu za kutofautiana na sura mpya za sasa zilizopo CUF,ambako kumejaa vijana wengi wenye damu ya mabadiliko ya haraka. Mama Maghimbi amesoma sheria Chuo Kikuu cha D'salaam mwaka 1989 na baadaye kusoma shahada ya pili ya sheria Warwick, England mwaka 1994.Mama Maghimbi ana watoto 3.

Mama Maghimbi ana mengi ya kutufundisha sisi vijana tunaokubali kubebwa kama vipochi bila ya kudadisi mambo....Amekuwa disappointed na CUF kwa muda mrefu sana na zaidi wale wanaojidai kuwa ndio wenye chama walikuwa wakimtenga tangia wamuondoe katika uongozi wa kambi ya upinzani bungeni....
 
Mama Maghimbi ana mengi ya kutufundisha sisi vijana tunaokubali kubebwa kama vipochi bila ya kudadisi mambo....Amekuwa disappointed na CUF kwa muda mrefu sana na zaidi wale wanaojidai kuwa ndio wenye chama walikuwa wakimtenga tangia wamuondoe katika uongozi wa kambi ya upinzani bungeni....

Mkuu,nafikiri mvumilivu hula mbivu! Nina ogopa sana jinsi hivi vyama vya upinzani vilivyojengwa jengwa. Kama alisimamia haki, alitakiwa asimame hivyo mpaka mwisho. Tukumbuke historia haziandikwi na watu wanaobadilika kutokana na kuvuma kwa upepo, na Mandela ni shahidi mkubwa wa hilo.
Mi naona amerejea kule alikokuwa siku zote, Lol
 
mwenda tezi na omo hurejea ngamani

wale wote walioapa na kuahidi watakilinda mpaka kufa hawawezi kihama

hata slaa ni wetu is A matter of time

Slaa wenu? Kaa la moto? Labda mumbadilishe mtazamo kwanza ama sivyo ni kubabuka tu! Waliomwengua awali hawakuwa wajinga kama inavyofikiriwa; jamaa hafiti kabisa katika mipangilio ya wakulu (mafiosi) wenye chama chao. Manake huo ndio mlango ambao kelele zake shurti mwenye jumba alale macho! :biggrin1::biggrin1::biggrin1::biggrin1:
 
"kwenye msafara wa mamba na kenge,mjusi wamo"
wako wengi lakini watajichuja wenyewe kutokana na mabadiliko ya siasa ndani ya vyama vya upinzani ambavyo navyo vinafanya demokrasia katika michakato yakupata viongozi hakuana aliyezaliwa kuongoza wote twafaa kwa kujifunza na vipaji huree mh mghimbi aluta kontinua nenda kwenu sifa ya ccm ni kuwa na watu wake kwenye vyama vya upinzani lakini naamini vijana wanaokuja kuchukua sasa madaraka ndani ya vyama hivi ni wapizani wa kweli wengi wao.
 
Mama Fatma Mussa Maghimbi (64) tunamtakia kila la kheri na safari zake zote mbili
 
Mkuu,nafikiri mvumilivu hula mbivu! Nina ogopa sana jinsi hivi vyama vya upinzani vilivyojengwa jengwa. Kama alisimamia haki, alitakiwa asimame hivyo mpaka mwisho. Tukumbuke historia haziandikwi na watu wanaobadilika kutokana na kuvuma kwa upepo, na Mandela ni shahidi mkubwa wa hilo.
Mi naona amerejea kule alikokuwa siku zote, Lol

Taib.

Ni rahisi kwa mnafiki kubadilika kama kinyonga. Ila kwa mwanamapinduzi yu tayari kujitoa kwa kile anachokiamini. Kama kweli tatizo lilikuwa CUF, basi alikuwa na nafasi ya ku-retire siasa kwa heshima wakati angali kiongozi. Na angeheshimika kama mmoja wa wamama madhubuti ktk duru za siasa ya nchi hii. Lakini kwenda kuungana na adui, it speaks volumes kuhusu huyu mama. Pengine kama ulivosema alikuwa inside operative wa CCM.
 
Mkuu Acid !,
Simtetei Mama Maghimbi,Lakini Mimi kama walivyo wengi hapa nimeshangazwa sana na Mama huyu kuondoka CUF na kurudi CCM.Kati ya Viongozi wa vyama vya Upinzani niliokuwa nawaamini kutokana na michango yao Bungeni na kwenye Majimbo yao ni pamoja na Mwanamama huyu ambaye kwa Taaluma ni mwanasheria.

Mama Fatma Mussa Maghimbi (64) alikuwa ni Mwanzilishi wa Chama cha CUF,na ana uhusiano wa karibu na Katibu Mkuu wa Chama hicho Seif Sharif Hamad.Mama huyo ambaye ameolewa Bara,na Mmoja wa Waanzilishi wa Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro Mzee Mussa Y.Maghimbi aliingia CUF mwaka 1992 na amekuwa Mbunge wa Chake chake (Mkoa wa Pemba Kusini) toka mwaka 1995.Kabla ya hapo Mama huyo alikuwa mfanyakazi wa Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam toka mwaka 1971.

Pamoja na mambo mengine Mama Maghimbi amekuwa mshiriki wa moja kwa moja wa siasa za Pemba na haswa CUF pamoja na kwamba muda wake mwingi anautumia Dar-es-salaam anakoishi na familia yake,yeye pamoja na Prof.Haroub Othman (RIP) na Mzee Hassan Said ni waanzilishi wa Zanzibar Legal Services Centre (ZLSC),Taasisi inayotoa ushauri na huduma za kisheria bure kwa watu wasio na uwezo,katika vipindi tofauti Mama Maghimbi amekuwa kiongozi wa Upinzani Bungeni na pia amekuwa Waziri Kivuli wa Mambo ya Katiba na Sheria.

katika kura za Maoni za CUF zilizofanyika mwezi Mei Mama Maghimbi pamoja na Wabunge wengine 11 walishindwa katika kura za maoni.Inawezekana kuwa Mama Maghimbi kahama CUF kwa sababu za kutofautiana na sura mpya za sasa zilizopo CUF,ambako kumejaa vijana wengi wenye damu ya mabadiliko ya haraka.
Mama Maghimbi amesoma sheria Chuo Kikuu cha D'salaam mwaka 1989 na baadaye kusoma shahada ya pili ya sheria Warwick, England mwaka 1994.Mama Maghimbi ana watoto 3.

Kama yeye na mumewe wanalandana basi ni bure kabisa! Halafu umesehau kwamba alikuwa katibu mhutasi (personal secretary) wa Hayati Abeid Karume na kuwa wapenzi kama nyumba ndogo. Mimi mchango wake wala sijauona kama ule wa Dr. Slaa, Zitto Kabwe.
 
Alikotoka na aendako the difference is the same, nyumba ni ileile waweza kupitia mlango wowote, mtakutana tu ndani!
 
,,,,,,,,,,,,,,Binafsi nitoe angalizo kwa CUF na CHADEMA na hasa CHADEMA kwa maana naona CUF hasa kwa upande wa visiwani wameanza kujirekebisha tena nitoe pongezi za dhati kwa Maalim Seif Sharif Hamad kwa kuona mbali ambapo wengine hawajapaona na bila shaka Mungu atambariki na kumuongoza katika azma yake njema ya kusaini makubaliano ya mwafaka. CHADEMA niwaonye tu kuwa kama kweli wanataka kuwa chama kizuri cha upinzani wajaribu kuacha pupa, watulie chini , waache kulumbanalumbana , wakubali kukosolewa wawe na moyo na bidii ya kujifunza na mwishowe wakatae ushabiki na......................Nova Kambota Is Always A gentle Man Feel Proud To Visit His Site, call 0717-709618 or 0783-610926,email;novakamota@gmail.com

Na wawe tayari kupokea matokeo ya uchaguzi 31 oct 2010. Na chama kiwaandae wanachama wake kisaikolojia....
 
Back
Top Bottom