Haya maswala ya GDP si yanategemea idadi ya watu? Halafu mbuzi na ng'ombe wa wamasai wala kuku wa kule Singida sidhani kama huwa wanathaminishwa, hivyo hichi kipimo sio cha kuamini sana tuangalie maisha ya wanamibia weusi na sisi wa TZ weusi yakoje. Pia tuangalie ugumu wa maisha ya TZ kulinganisha na Namibia yakoje? Hizi takwimu kwangu mimi sioni kama ni kipimo sahihi kwa maisha ya mwafrika.
Kenya wana GDP kubwa ila raia wao wengi wanamaisha magumu sana, hivyo wale wachache waliojilimbikizia mali nyingi ndio pesa zao ugawanywa hata kwa wale wasio na uwezo wakupata mlo mmoja kwa siku ili kutoa faraja kwao kwa kwa njia ya GDP. Tufike mahali Afrika tuwe na njia yetu ya kupima maendeleo yetu alisema PLO Lumumba.