FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,883
- 109,202
- Thread starter
- #1,901
Faiza naomba nieleweshe juu ja jambo hili. Kunasehumu mkoani pwani Wilaya rufiji,utete. Kuna chemchem inatoa maji moto mda wote na maji hayo yanatokota kama yapo jikoni hivi kinasababisha hivyo. Na istoshe maji yale ni kama dawa kwa watu kwenye vipele ukioga Yale maji kesho vipele vyote vimekauka.
Naam, hizo ni chemchem za maji moto, zipo sehemu mbali mbali Tanzania na zipo nyingi sana na sehemu mbali mbali duniani. Kingereza zinajulikana kama "hot water springs" au "geysers".
Zingine zinakuwa za moto sana kiasi hakuna awezae kuzioga na zingine huwa vuguvugu na watu huweza kuoga.
Kutibu mapele ni kutokana na "minerals" virutubisho vilivyomo kwenye hayo maji.
Kuna chemchem kama hizo nyingi watu huamini kuwa kuna mizimu na huenda kufanya ada zao za kishirikina hapo.
Nchi zingine ni vivutio vikubwa vya utalii na utakuta sehemu kama hizo zimejengewa vizuri sana na watu huenda kujiburudisha kwa kuoga kwenye hayo maji ya moto:
Ni maji yaliyoingia chini ya ardhi kutokea ardhini na kufika kwenye miamba ya joto/moto na kurudi tena juu yakiwa ya moto. Tazama:
Soma uzi huu pia: Maajabu ya maji Moto kisaki(Hot spring)