Kuna maisha mengine zaidi ya haya ya duniani?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,620
46,261
Kila ninapowaza kuhusu maisha mengine baada ya haya ya duniani huwa najawa na maswali mengi ambayo sijawahi kupata majibu yake mazuri, Mfano

Swali la kwanza ni tofauti kubwa sana kati ya dini/imani za binadamu kuhusu hayo maisha mengine baada ya haya ya duniani.
Katika dini zote wanazoamini mbingu, maelezo ya aina ya mbingu katika hizo dini zote ni tofauti sana kiasi cha kuzua maswali kutakuwa na mbingu ngapi na kama mungu ni mmoja au miungu wako wangapi.

Swali la pili ni kuhusu wanyama, Sijawahi kupata jibu la kueleweka kuhusu hawa wanyama wanaofugwa na binadamu kama kitoweo au pet pamoja na wanyamapori kama watakuwepo au hawatakuwepo mbinguni. Kuku uliyemchinja ukamla utakutana naye mbinguni? Itakuaje

Jambo la tatu, ni lini hasa hayo maisha mengine baada ya haya yanaanza. Kuna wanaoaimini yanaanza pindi tu pale mtu anapokufa, kuna wanaoaimini yataanza kwa pamoja baada ya mwisho wote wa dunia wa watu kufika kwa pamoja.

Jambo la mwisho ni kama hakuna maisha mengine inakuwa Jambo la kuhuzunisha zaidi na kukosesha raha ukifikiria kwamba mnapoachana na ndungu, jamaa, marafiki na wale unaowapenda baada ya maisha haya ndio imetoka hivyo hakuna kuonana tena. Walioteseka katika dunia hii maisha yao yote ndio imetoka hivyo (hawatapata fursa ya kuimba milele na kutosikia njaa, hamu au mateso wakienda mbingu hiyo, kupata mabikiria na vileo wakienda mbingu hiyo) na watu waliofanya maovu makubwa pia hapa duniani ndio imetoka hivyo baada ya maisha haya.
 
Maisha Halisi ni hapahapa juu ya nchi sema je upo kwenye mfumo gani?

Je ni dunia (philosophy,psychology,theology,miungu yote,mizimu yote ect)

Au ni mfumo wa aliyekuumba yaani Real Source ambaye hana dini wala dhehebu au kabila.

Anasema hatulalala(kufa) sote bali sote tutabafilika korintho 15:51
4f3fff4a-1d8f-4784-861d-51862b8f8ffa.jpg
 
Maisha mengine yapo ili wale waovu walipwe kulingana na uovu wao walioufanya hapa duniani ...mfano waliokuwa ma dicteta na dunia iliwaogopa. Pia wenye kudhulumiwa walipe haki zao.
Yatakuwa maisha yasiyo na mwisho baada ya hukumu.
Wanadamu wote watafufuliwa kuanzia wa mwanzo kuumbwa na wa mwisho. Yani kuanzia Nabii Adam.
Mungu wetu ni muweza. Alituumba tukiwa si lolote hivyo hashindwi kuturejesha.
Hiyo ni kwa mujibu wa Uislam.
 
Ukifa ndo end of story
Quran 36:77
- Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri!

Quran 36:78
- Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika?

Quran 36:79
- Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba.


UTAFUFULIWA UTAKE USITAKE HIYO NI AHADI YA ALLAH
 
Quran 36:77
- Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri!

Quran 36:78
- Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika?

Quran 36:79
- Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba.


UTAFUFULIWA UTAKE USITAKE HIYO NI AHADI YA ALLAH
That will never happen. Ukifa unakua mifupa mitupu. Over .
 
Kila ninapowaza kuhusu maisha mengine baada ya haya ya duniani huwa najawa na maswali mengi ambayo sijawahi kupata majibu yake mazuri, Mfano

Swali la kwanza ni tofauti kubwa sana kati ya dini/imani za binadamu kuhusu hayo maisha mengine baada ya haya ya duniani.
Katika dini zote wanazoamini mbingu, maelezo ya aina ya mbingu katika hizo dini zote ni tofauti sana kiasi cha kuzua maswali kutakuwa na mbingu ngapi na kama mungu ni mmoja au miungu wako wangapi.

Swali la pili ni kuhusu wanyama, Sijawahi kupata jibu la kueleweka kuhusu hawa wanyama wanaofugwa na binadamu kama kitoweo au pet pamoja na wanyamapori kama watakuwepo au hawatakuwepo mbinguni. Kuku uliyemchinja ukamla utakutana naye mbinguni? Itakuaje

Jambo la tatu, ni lini hasa hayo maisha mengine baada ya haya yanaanza. Kuna wanaoaimini yanaanza pindi tu pale mtu anapokufa, kuna wanaoaimini yataanza kwa pamoja baada ya mwisho wote wa dunia wa watu kufika kwa pamoja.

Jambo la mwisho ni kama hakuna maisha mengine inakuwa Jambo la kuhuzunisha zaidi na kukosesha raha ukifikiria kwamba mnapoachana na ndungu, jamaa, marafiki na wale unaowapenda baada ya maisha haya ndio imetoka hivyo hakuna kuonana tena. Walioteseka katika dunia hii maisha yao yote ndio imetoka hivyo (hawatapata fursa ya kuimba milele na kutosikia njaa, hamu au mateso wakienda mbingu hiyo, kupata mabikiria na vileo wakienda mbingu hiyo) na watu waliofanya maovu makubwa pia hapa duniani ndio imetoka hivyo baada ya maisha haya.
Nafikiri neno KIFO pekee linajitosheleza.

_20240128_004216.JPG
 
Kila ninapowaza kuhusu maisha mengine baada ya haya ya duniani huwa najawa na maswali mengi ambayo sijawahi kupata majibu yake mazuri, Mfano

Swali la kwanza ni tofauti kubwa sana kati ya dini/imani za binadamu kuhusu hayo maisha mengine baada ya haya ya duniani.
Katika dini zote wanazoamini mbingu, maelezo ya aina ya mbingu katika hizo dini zote ni tofauti sana kiasi cha kuzua maswali kutakuwa na mbingu ngapi na kama mungu ni mmoja au miungu wako wangapi.

Swali la pili ni kuhusu wanyama, Sijawahi kupata jibu la kueleweka kuhusu hawa wanyama wanaofugwa na binadamu kama kitoweo au pet pamoja na wanyamapori kama watakuwepo au hawatakuwepo mbinguni. Kuku uliyemchinja ukamla utakutana naye mbinguni? Itakuaje

Jambo la tatu, ni lini hasa hayo maisha mengine baada ya haya yanaanza. Kuna wanaoaimini yanaanza pindi tu pale mtu anapokufa, kuna wanaoaimini yataanza kwa pamoja baada ya mwisho wote wa dunia wa watu kufika kwa pamoja.

Jambo la mwisho ni kama hakuna maisha mengine inakuwa Jambo la kuhuzunisha zaidi na kukosesha raha ukifikiria kwamba mnapoachana na ndungu, jamaa, marafiki na wale unaowapenda baada ya maisha haya ndio imetoka hivyo hakuna kuonana tena. Walioteseka katika dunia hii maisha yao yote ndio imetoka hivyo (hawatapata fursa ya kuimba milele na kutosikia njaa, hamu au mateso wakienda mbingu hiyo, kupata mabikiria na vileo wakienda mbingu hiyo) na watu waliofanya maovu makubwa pia hapa duniani ndio imetoka hivyo baada ya maisha haya.
Ukishakufa utatupa mrejesho
 
Mda wako ukisimama, yaani utashindwa kufanya chochote. Hutoweza kupumua, kufikiri, kuongea, kucheka wala kufanya jambo lolote na hutojitambua. Ni sawa labda unaangalia muvi afu ukabofya kitufe cha PAUSE kwenye remote control, hiyo muvie itaganda, haitotoa sauti wala chochote kwa sababu umesimamisha mda. Hapo ndipo tunasema mtu kafa yaan mda wako umeisha, na ukifa hiyo imeisha hakuna cha mbingu wala nini, kinachofuata wewe unabadili form . Binadamu unakuwa maiti, unazikwa unaoza, unaliwa na bacteria, unakuwa mbolea, mimea inastawi, inatoa oksjeni, wanyama wanaivuta, na cycle inaendelea na ni endelevu haina mwisho.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom