Tuipime hii thread na dhamira ya mletaji. Ukiiangalia kwa jicho moja unaweza kufikiri mleta mada ni mpuuzi anayechochea uovu. Ukitumia jicho la tatu utapats funzo kuwa mabadiliko ya tabia kwa mkeo inawezekana ikawa ishara ya kuanza kwa uovu wa mkeo.
Tuijadili katika mtazamo huo tutapata faida nyingi. Nakumbuka nikiwa undergraduate, lecturer mmoja alisema tatizo kubwa la vijana darasani hushindwa kufaulu vizuri kwa kukosa mbinu za kuelewa swali na kushindwa kujua key words zilizobeba swali.
Vijana wanachanganya haya, discuss-jadili, hapa unatoa hoja kwa pande zote mbili , faida na hasara na kutoa msimamo wako. Explain, elaborate n.k, huwezi kutoa jibu sawa kati yao.
Dhamira yangu kwa mfano mke amepunguza wivu na mahaba, hiyo ni indicator kuwa kuna kitu kinaendelea.
Mtoa mada labda unishawishi kuwa umetumia tafsida, lakini neno faida huwezi kulielezea kwa mtindo huo. Ninawashukuru wanajamvi.