Fahamu kuhusu msukule

Fahamu kuhusu msukule

UKIWA NDANI YA YESU HAYO MAMBO UTAKUWA UNASIKIA KWA WENGINE

KWA JINA LANGU MTATOA PEPO MTANENA KWA LUGHA MPYA NA MATAKULA CHA KUFISHA WALA HAKITA WADHURU

NIME WAPA AMRI JUU YA KULA FALME NA MAMLAKA ZA GIZA

YESU ANASEMA NJOONI WOTE WENYE KUSUMBUKA NA KUELEMEWA NA MIZIGO NAYE ATAWAPUMZISHA HIYO NDIO MIZIGO YENYEWE

HAKUNA UGANGA WALA UCHAWI JUU YA ISRAEL

inamana islael hamna uchaw
 
UKIWA NDANI YA YESU HAYO MAMBO UTAKUWA UNASIKIA KWA WENGINE

KWA JINA LANGU MTATOA PEPO MTANENA KWA LUGHA MPYA NA MATAKULA CHA KUFISHA WALA HAKITA WADHURU

NIME WAPA AMRI JUU YA KULA FALME NA MAMLAKA ZA GIZA

YESU ANASEMA NJOONI WOTE WENYE KUSUMBUKA NA KUELEMEWA NA MIZIGO NAYE ATAWAPUMZISHA HIYO NDIO MIZIGO YENYEWE

HAKUNA UGANGA WALA UCHAWI JUU YA ISRAEL
Nyie ndio wachawi wenyewe unatuzuga ili uendelee kutumaliza tukawalimie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Msukule ni mtu ambaye anahesabiwa amekufa, lakini ukweli ni kuwa mtu huyo huwa amechukuliwa na Mchawi ili amtumie katika kazi zake maalum au amtumie katika mambo yake mengine anayoyataka.

Mchawi humfanya mtu huyo awe maiti au kama kitu kinachojiendesha chenyewe kikiwa kimekufa lakini hakijaoza wala hakiozi.

Mchawi kabla ya kumchukua mtu Msukule hufanya Mkataba Maalum na Jini anayeitwa “BAKAS” ili amsaidie katika kazi hiyo, na kuna Sadaka maalum ambayo hutoa kumlipa Jini huyo kama malipo ya kazi yake. Huyu Bakas ni Jini anayetawala siku ya Jumamosi.

Baada ya kukubaliana na Jini Bakas Mchawi huchagua mtu ambaye anataka kumchukua na akishampata huenda nyumbani kwa mtu huyo kinyume nyume mpaka anafika mlango wa mbele.

Anapofika mlangoni hunyonya roho ya mtu anayemtaka kwa kupitia tundu ya ufunguo na kama tundu hiyo haipo hutoboa tundu ndogo ambayo huiziba akimaliza kazi yake.

Baada ya kuipata roho anayoitaka huitia ndani ya chupa na kuziba chupa hiyo na kuondoka. Kazi hiyo hufanyika usiku wa manane kati ya saa nane na saa tisa usiku.

Siku inayofuata yule aliyechukuliwa roho yake huanza kuugua na hufa ghafla.

Baada ya Mazishi yule Mchawi huenda kaburini akiongozana na yule Jini Bakas ambaye hujigeuza kama babu kizee mwenye ndevu nyingi nyeupe ili kuuchukua ule mwili wa Marehemu.

Wanapofika makaburini yule Jini hukaa upande wa kichwani kwa maiti na mchawi hukaa upande wa miguuni na kila mmoja wao akifanya uchawi wake lakini kazi kubwa ya kumtoa maiti ndani ya kaburi kufanya na Jini.

Jini huomba kwa bidii na kunuiza Uchawi na husema maneno ya kichawi huku akimwaga juu ya kaburi majani ya Mkakaya (Acacia)

Mchawi yeye kwa upande wake husema maneno haya yafuatayo akirudia rudia “Mortoo tombo Mivi” maana yake ni kwamba “aliye ndani ya kaburi ni wangu”

Kwa nguvu za Uchawi mwili hutoka kaburini bila ya kaburi kuchimbwa na kusimama mbele yao na yule mchawi hukabidhiwa maiti huyo.

Baada ya kukabidhiwa kitu cha kwanza ambacho hufanya ni kwenda nyumbani na kumuonesha huyo ndugu zake kuona kama atawakumbuka.

Maiti huyo asipozinduka na kuwagundua ndugu zake au kutambua nyumbani kwao basi Mchawi hujua kwamba kazi imekuwa nzuri na hupelekwa nyumbani kwa mchawi.

Wakifika nyumbani Mchawi humrudishia yule Maiti roho ambayo aliiweka ndani ya chupa na kumnywesha dawa kali ambayo itamfanya asahau kabisa maisha yake yote ya nyuma yaliyopita na baada ya hapo maiti huyo atazinduka na kuwa Msukule.

Msukule ni binaadamu anayeishi lakini hana uhuru na anatumiwa kama mtumwa huku ndugu zake au jamaa zake wakijua kwamba amekufa.

Uchawi huu wa kuchukua Msukule ulianza miaka 500 na 1500 A.D. huko nchini Congo na Haiti na kuenea sehemu nyingi za Dunia.

James
James at February 15, 2020.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama umeweza kuelezeka kuhusu msukule then wewe ni nani usiamini uwepo wa Mungu.
Tuzidi kujiimarisha kwake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoa maada, swali ni kuwa ntajuaje kuwa ndugu yangu kachukuliwa msukule (pale inapotokea ndugu yangu kafariki)...maana nataka kila ndugu yangu anapofariki niwe na prove kama kafa kweli au lah...

Kwa hiyo ww upo kwa ajili ya ndugu zako wafe ili uchunguze wamekufaje,vipi ulianza kufa ww kabla ya hao unaotaka kuwachunguza Mkuu!!!
 
Kuna maza angu mdogo alichukuliwa msukule.. kuna mtaalamu alifanikiwa kumrescue ila kumfanyia reverse transcription to condition yake ya awali na kumuachia uraiani ndo imekuwa mziki mwaka wa pili unakatika sasa

JE KUNA WATAALAMU WANAOWEZA KUREVERSE ENGINEER PROCESS NZIMA NA KUMCONVERT HUYO MTU KATIKA HALI YAKE YA KAWAIDA NA SOUL YAKE???

Sent using Jamii Forums mobile app
Mumpeleke akakanyage mafuta mbona simple tu.
 
Sayansi ya sensa ya sita, upuuzi mtupu ukitumia sensa tano kutafsiri....

Hata hivyo bado ni upuuzi kwa kuwa tumeumbwa kutumia sensa tano na sio zaidi.
 
Acha upopoma, wakati huku kwetu watoto wa wanaoshinda kanisani ndo wanabebwa kichawi KIRAHISI sana!!!


Kizibo

Amesema ukiwa ndani ya Kristo .Sio ukiwa ndani ya kanisa.Unajua tofauti ya kuwa ndani ya Kristo Na kwenda kanisani kila Leo ?Kuwa ndani ya Kristo ni Kuishi maisha yanampendeza Mungu Yaani kuwa msafi.Na hiii haimaanishi kila anaeshinda kanisani ni msafi.Hao wanaoshinda kanisani Na bado Wanachukuliwa misukule ujue hawako ndani ya Kristo.Wanaenda kanisani lakini matendo yao ni maovu.Hakuna aliye ndani ya Kristo (anayeishi maisha matakatifu Au aliye Na wokovu) anayechukuliwa Msukule wewe,HAYUPO.Yaani achukuliwe msukule Na Mungu anakuwa wapi wakati huo kulinda mtu wake ?Likizo Au ?Hakunaga hiyo


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom