Fahamu kisa cha huyu binti kujinyonga

Fahamu kisa cha huyu binti kujinyonga

Inanikumbusha dada mmoja alikuwa anatoroka usiku kwa baba yake Engineer alikuwa anakaa jirani na kanisa la Kakobe, binti alikuwa anatoroka usiku anaenda kujamiana na mlinzi wa nyumba ya jirani ambaye ni mtu mzima kuliko baba yake. Alipopata mimba babayake hakuwa na tatizo akasema kwa kuwa wanaoendana basi waoane. Yule mlinzi alikubali binti akawa hataki. Walifungishwa harusi wanaishi wote ikawa mwisho wa elimu na mwanzo wa maisha ya taabu. Hiyo ni mmoja wapo ya aina ya mimba ya bahati mbaya
Nyeege mshindo zimemponza binti!!
 
Alikuwa yatima sawa lakini tayari alikuwa ni over 18, mtu aliyezaa naye ni someone's husband.. Sio mchumba nimefafanua hilo
Ila Mkuu mchana huyo mtu au mwanaume amekuwa someone's husband baada ya kumtupa binti na mwanaye. Kibaya mwanao anakufa humziki. Hiyo ni roho ya uharamia na mtoto huyo aliyemtupa anaweza kabisa kuharibu watoto wengine watakaozaliwa. Pia ukweli hatujui binti alitamka maneno gani wakati akiteseka kulea au akijiua. Hivyo ni vyema tu uwe na moyo wa huruma wanaume.
 
Ukizaa na mtu ukagundua hakupendi, kiufupi mdelete kila mahali kwa gharama yoyote utaishi kwa amani sana. Angebaki na uchungu wa kufiwa tu baadae angezoea. Inauma hii mno
 
Alikuwa yatima sawa lakini tayari alikuwa ni over 18, mtu aliyezaa naye ni someone's husband.. Sio mchumba nimefafanua hilo
Nani alisema miaka 18 ni Umri wa Mtu Mzima..!?

Kiasi kwamba mkaupa thamani ya binadamu kuweza kujiamulia alionalo sahihi, kwa kuwa Eti keshakomaa.!?

Nionavyo ni Umri wa kibinadamu Unaotumika kuhukumia watu wao, na ni dhana ya kimagharibi Tu.

Nyinyi kama Ma GT sioni sababu ya kutumia kama Fimbo ya hukumu, kwa kuwa ni kipimo Dhaifu cha Kuhukumia Mtu.

Binadamu hata awe na Mvi mpaka kusikojulikana.Kama hajaumbika Upya ndani Yake na kuruhusu ile Nguvu ya ndani kutenda Kazi ni sawa na Bure.

Alilofanya siwezi Kuribariki wala Kulitolea hukumu.Ni kama Tu wafanyavyo na wengine ila kwa Mitindo tofauti.

Ila kosa nijualo Ambalo wengi wetu hulitenda, ni kupokea Utamaduni wa ulimwengu wenye ulaghai Bila Tashwishi na Baadae ukishakutafuna na kukumaliza ladha na kukutema kama Big G, wale imara huyumba na wengi Kupotea kabisa.

Na Hii tabia ya kudandia Gari hujui linapotoka na wala linakoelekea na wala Hujiulizi na wala kuuliza, ni kwanini iwe hivi na wala isiwe Vile.!? Kweli haijawahi acha watu salama.
 
Baadhi ya picha
IMG-20180512-WA0037.jpg
IMG_20180512_105312_646.jpg
IMG-20180512-WA0015.jpg
IMG_20180512_091923.jpg
IMG_20180512_072454_885.jpg
 
Dah...hivi inakwaje unampenda MTU zaidi ya unavyojipenda wewe na hali wewe siyo bodyguard wake?...
 
Nilisikiliza mahubiri ya mchungaji mmoja anasema Roho ikifikia mawazo ya kujiua your destiny jackpot is just around the corner
 
Back
Top Bottom