Facebook kununua WhatsApp kwa Sh 30.9 trilioni

Facebook kununua WhatsApp kwa Sh 30.9 trilioni

Watu mnakera sana mnavopondea matangazo, sasa mnataka hela wao watoe wapi???
Software hamjawahi lipia hata kumi, hamtaki kuzinunua, bado mnataka zisiwe na matangazo, hizo data zinazopita kwenye server za jamaa mnajua wanalipa kiasi gani kuendesha? Wafanyakazi wao wale wapi? Midude mingine bna, kwani wewe tangazo linakupunguzia nini kulitazama? Hutaki kuona tangazo hata kama ni la dawa itakayomponya bibi yako anayekaribia kudanja kwa kukosa matibabu??
 
hivi jamaa asingeiuza angekosa nini? hizo hela alizouzia atazifanyia nini?

au aende saudi arabia akanunue visima vya mafuta
 
Hivi whatapp alikuwa anapataje faidi kwa hii app yake naomba kujuzwa.
 
Hivi whatapp alikuwa anapataje faidi kwa hii app yake naomba kujuzwa.

WhatsApp wanacharge $1 kwa mwaka, ila sisi wabongo mara nyingi wanatusamehe na kutupa 1 year free kila mwaka. Ila sidhani kama facebook wamewanunua kwa ajili ya kukusanya direct profit kihivyo, sitashangaa ikiwa bure kabisa tena bila matangazo kama fb messenger.
zaidi wanataka info za watu wanaongelea nini ili kuweza kuwatarget vizuri na ads kwenye facebook na aps/websites zengine. Facebook wamelaunch mobile ads kama Admob ya Google na Im sure watalaunch website ads kama Adsense yao. Fikiria unaongelea kununua gari kwenye chat yako WhatsApp kisha unaenda site yenye Facebook Ads na kuona Ads za wauza magari eneo ulipo.
 
hivi jamaa asingeiuza angekosa nini? hizo hela alizouzia atazifanyia nini?

au aende saudi arabia akanunue visima vya mafuta

Mbali na hela kibao pia kapewa share za Facebook za kutosha ,,, ni win win
 
Tatizo sio rahisi kuwahamisha watu.wote kutoka whatsapp hasa wazee ambao hukuta iko pre installed kwenye device zao. Na ukizungumzia kuhama kila mtu atahamia anapopataka yeye wewe uende telegram, mwingine viber mwingine Line basi itabidi uwe na apps nyingi ambazo zitakuwa zikifanya same thing

Kama facebook wataingiza maswala ya matangazo obvious whatsapp itakufa ama wakikomalia kuchaji watu hela basi.itakufa tu

The Facebook founder said he believed WhatsApp was on track to have a billion users, but insisted he had no plans to place advertising on WhatsApp's interface, saying he did not think ads were the best way to make money from messaging systems.,,
 
Tena hili deal likubali na wai-link facebook na whatsapp ili watu tufaidi vizuri, halafu huenda tusilipie tena kama itanunuliwa.
 
hivi unaweza kitumia simu kama haina pesa au mb kuchati.??????

Haiwezekani , lakini crdt au bundle unalolipia kwenye cm Yako watsap , Facebook au mitandao unayoingia hawapati chochote hiyo ni service nyingine Kabisa , watsap inauzwa dola 1 kwa ,,,
 
ndo yale yale ya EBAY kuinunua SKYPE afu na kuwauzia MICROSOFT !
 
it's a pity that poor BBM wont be able compete with whatsapp.
 
Facebook wamenunua kampuni ya Whatsapp kwa 16 billion dollars.



Sent from my Lumia phone using Tapatalk

hivyo vidolali mtu kama EL angeunganisha nguvu na rafiki zake the like of Rostam wangeshindwa kweli kuinunua whatsapp?!.....ila nahisi biashara ya ikulu inafaida zaidi.lol
 
Hivi whatapp alikuwa anapataje faidi kwa hii app yake naomba kujuzwa.

miliki wa whatsapp alikuwa hapati faida yoyoye kubwa zaidi ya kuwa na subira na kuitumia vizuri kauli ya panda mbengu ili siku moja iote uvune mavuno.na kweli mavuno yameotasiku,siku chache zijazo atatia kibindoni $16 billion toka kwa bwana mdogo tajiri na mmliki wa facebook, mark zuckerberg.
 
miliki wa whatsapp alikuwa hapati faida yoyoye kubwa zaidi ya kuwa na subira na kuitumia vizuri kauli ya panda mbengu ili siku moja iote uvune mavuno.na kweli mavuno yameotasiku,siku chache zijazo atatia kibindoni $16 billion toka kwa bwana mdogo tajiri na mmliki wa facebook, mark zuckerberg.

Hapewe Zote... Anapewa $4 Billion the rest anapewa stock sasa sjajua n stock za fb company au?
 
Jamaa walichomoa dili la google la dola bilioni kumi now imekuwa neema kwao
 
hivyo vidolali mtu kama EL angeunganisha nguvu na rafiki zake the like of Rostam wangeshindwa kweli kuinunua whatsapp?!.....ila nahisi biashara ya ikulu inafaida zaidi.lol

Mkuu hizo billion ni dollar sio za madafu. Lowasa na rostam hawana hizo.

Hiyo pesa inakaribia bajeti ya nchi za afrika mashariki kwa mwaka ndio mjue afrika tunasafari ndefu
 
Back
Top Bottom