Mparee2
JF-Expert Member
- Sep 2, 2012
- 2,592
- 4,279
Binafsi sioni kama ni sawa kuondoa ushindani kwenye bidhaa (kibiashara)
Nilitamani EWURA watoe bei Elekezi ya juu, ila bei ya chini waache kila mtu ajipangie
Tumeona hii ikifanyika kwenye ada za Shule za private nk
Kuna vituo vya mafuta vyenye uwekezaji mkubwa na wanamitaji mikubwa hivyo wanaweza kuuza mafuta kwa bei rafiki ila wanalazimishwa na sheria wauze bei iliyopangwa lakini pia, unaweza kukutana na mafuta kwenye baadhi ya vituo sio ya kueleweka ila ndio hivyo tena wanatakiwa nao wauze bei hiyo hiyo.
Nafikiri pia bei elekezi ingetolewa kila baada ya miezi mitatu kwa wafanya biashara walioko pembezoni bei elekezi inayotolewa kila mwezi, sidhami kama inawasaidia; sana sana inawapa tu Changamoto kwani logistic ya kufanya manunuzi hadi mzigo uwafikie inawachukua pengine wiki mbili kwa hiyo inakuwa kama wametengwa au hawafikiriwi
"BIASHARA YENYE USHINDANI NDIO HULETA UNAFUU KWA MNUNUZI WA MWISHO/MWANANCHI"
Nilitamani EWURA watoe bei Elekezi ya juu, ila bei ya chini waache kila mtu ajipangie
Tumeona hii ikifanyika kwenye ada za Shule za private nk
Kuna vituo vya mafuta vyenye uwekezaji mkubwa na wanamitaji mikubwa hivyo wanaweza kuuza mafuta kwa bei rafiki ila wanalazimishwa na sheria wauze bei iliyopangwa lakini pia, unaweza kukutana na mafuta kwenye baadhi ya vituo sio ya kueleweka ila ndio hivyo tena wanatakiwa nao wauze bei hiyo hiyo.
Nafikiri pia bei elekezi ingetolewa kila baada ya miezi mitatu kwa wafanya biashara walioko pembezoni bei elekezi inayotolewa kila mwezi, sidhami kama inawasaidia; sana sana inawapa tu Changamoto kwani logistic ya kufanya manunuzi hadi mzigo uwafikie inawachukua pengine wiki mbili kwa hiyo inakuwa kama wametengwa au hawafikiriwi
"BIASHARA YENYE USHINDANI NDIO HULETA UNAFUU KWA MNUNUZI WA MWISHO/MWANANCHI"