figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Salaam Wakuu,
Imedaiwa Eti, Tanzania kupitia Stamico tumesaini mkataba wa kuuza Madini ya Makaa ya Mawe kwa dola 29.5 ambayo ni sawa na Shilingi 69,444 (Elfu sitini na tisa na Mia nne arobaini na nne tu) kwa Tani moja!
Bei ya Soko la Makaa ya Mawe kwenye Market Insider ni dola 315 sawa na shilingi za Kitanzania 740,250 (laki saba na elfu arobaini na mia mbili na hamsini).
Reuters wameripoti kuwa bei ya Madini ya Makaa ya Mawe inatazamiwa kupanda kwa mwaka 2022 kufikia dola za Kimarekani 500 sawa na shilingi za Kitanzania 1,175,000 (Milioni moja na laki moja na elfu sabini na tano)
Afrika Kusini wanauza makaa ya Mawe kwa bei ya Dola za Kimarekani 140.07 ambayo ni sawa na shilingi 329,164 hii ni bei iliyoporomoka toka kwenye bei ya Dola 214.27 sawa na shilingi 503,534 ya mwezi uliopita!
Ukiangalia bei ya Soko la Madini haya na wastani wa bei inaashiria dhahiri pasi na shaka kuwa Mkataba huu una viashiria vikubwa mno vya Rushwa!
Haiwezekani Madini yetu ya Makaa ya Mawe yauzwe kwa bei inayolingana na bei ya Kifusi cha Udongo/Mchanga!
Watoto na wajukuu zetu watakuta mapango na mashimo watatuuliza hapa palifanyika jambo gani?
Tukiwaambia palikuwa na Madini ya Makaa ya Mawe ambayo yaliuzwa kwa Tani elfu 69,444 watatulaani, watatutukana na kutuadhibu!
Ni heri haya Madini tuyaache vizazi vijavyo viyakute kuliko kuyachimba na kuyauza kwa Mikataba iliyojaa rushwa na Ufisadi!
Haiwezekani Mbuzi mmoja awe na thamani kubwa kuliko Tani moja ya Madini ya Makaa ya Mawe!
Naiomba Serikali kupitia vyombo vyake iuchunguze mkataba huu , iuvunje na ichukue hatua kali kwa kila aliyehusika kuruhusu Mkataba wa kifisadi kama huu ili iwe fundisho kwa watumishi wa Umma wote na wanasiasa wasio waadilifu!
Wizara ya Madini.
Napenda kupata kauli ya STAMICO ilikuwaje wakaingia huu Mkataba
Pia, soma;
Thread 'Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya' Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya.
Imedaiwa Eti, Tanzania kupitia Stamico tumesaini mkataba wa kuuza Madini ya Makaa ya Mawe kwa dola 29.5 ambayo ni sawa na Shilingi 69,444 (Elfu sitini na tisa na Mia nne arobaini na nne tu) kwa Tani moja!
Bei ya Soko la Makaa ya Mawe kwenye Market Insider ni dola 315 sawa na shilingi za Kitanzania 740,250 (laki saba na elfu arobaini na mia mbili na hamsini).
Reuters wameripoti kuwa bei ya Madini ya Makaa ya Mawe inatazamiwa kupanda kwa mwaka 2022 kufikia dola za Kimarekani 500 sawa na shilingi za Kitanzania 1,175,000 (Milioni moja na laki moja na elfu sabini na tano)
Afrika Kusini wanauza makaa ya Mawe kwa bei ya Dola za Kimarekani 140.07 ambayo ni sawa na shilingi 329,164 hii ni bei iliyoporomoka toka kwenye bei ya Dola 214.27 sawa na shilingi 503,534 ya mwezi uliopita!
Ukiangalia bei ya Soko la Madini haya na wastani wa bei inaashiria dhahiri pasi na shaka kuwa Mkataba huu una viashiria vikubwa mno vya Rushwa!
Haiwezekani Madini yetu ya Makaa ya Mawe yauzwe kwa bei inayolingana na bei ya Kifusi cha Udongo/Mchanga!
Watoto na wajukuu zetu watakuta mapango na mashimo watatuuliza hapa palifanyika jambo gani?
Tukiwaambia palikuwa na Madini ya Makaa ya Mawe ambayo yaliuzwa kwa Tani elfu 69,444 watatulaani, watatutukana na kutuadhibu!
Ni heri haya Madini tuyaache vizazi vijavyo viyakute kuliko kuyachimba na kuyauza kwa Mikataba iliyojaa rushwa na Ufisadi!
Haiwezekani Mbuzi mmoja awe na thamani kubwa kuliko Tani moja ya Madini ya Makaa ya Mawe!
Naiomba Serikali kupitia vyombo vyake iuchunguze mkataba huu , iuvunje na ichukue hatua kali kwa kila aliyehusika kuruhusu Mkataba wa kifisadi kama huu ili iwe fundisho kwa watumishi wa Umma wote na wanasiasa wasio waadilifu!
Wizara ya Madini.
Napenda kupata kauli ya STAMICO ilikuwaje wakaingia huu Mkataba
Pia, soma;
Thread 'Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya' Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya.