Eti STAMICO wanauza Makaa ya Mawe tani moja kwa Tsh 60,000/= Mkataba huu Uvunjwe

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
Salaam Wakuu,

Imedaiwa Eti, Tanzania kupitia Stamico tumesaini mkataba wa kuuza Madini ya Makaa ya Mawe kwa dola 29.5 ambayo ni sawa na Shilingi 69,444 (Elfu sitini na tisa na Mia nne arobaini na nne tu) kwa Tani moja!

Bei ya Soko la Makaa ya Mawe kwenye Market Insider ni dola 315 sawa na shilingi za Kitanzania 740,250 (laki saba na elfu arobaini na mia mbili na hamsini).

Reuters wameripoti kuwa bei ya Madini ya Makaa ya Mawe inatazamiwa kupanda kwa mwaka 2022 kufikia dola za Kimarekani 500 sawa na shilingi za Kitanzania 1,175,000 (Milioni moja na laki moja na elfu sabini na tano)

Afrika Kusini wanauza makaa ya Mawe kwa bei ya Dola za Kimarekani 140.07 ambayo ni sawa na shilingi 329,164 hii ni bei iliyoporomoka toka kwenye bei ya Dola 214.27 sawa na shilingi 503,534 ya mwezi uliopita!

Ukiangalia bei ya Soko la Madini haya na wastani wa bei inaashiria dhahiri pasi na shaka kuwa Mkataba huu una viashiria vikubwa mno vya Rushwa!

Haiwezekani Madini yetu ya Makaa ya Mawe yauzwe kwa bei inayolingana na bei ya Kifusi cha Udongo/Mchanga!

Watoto na wajukuu zetu watakuta mapango na mashimo watatuuliza hapa palifanyika jambo gani?

Tukiwaambia palikuwa na Madini ya Makaa ya Mawe ambayo yaliuzwa kwa Tani elfu 69,444 watatulaani, watatutukana na kutuadhibu!

Ni heri haya Madini tuyaache vizazi vijavyo viyakute kuliko kuyachimba na kuyauza kwa Mikataba iliyojaa rushwa na Ufisadi!

Haiwezekani Mbuzi mmoja awe na thamani kubwa kuliko Tani moja ya Madini ya Makaa ya Mawe!

Naiomba Serikali kupitia vyombo vyake iuchunguze mkataba huu , iuvunje na ichukue hatua kali kwa kila aliyehusika kuruhusu Mkataba wa kifisadi kama huu ili iwe fundisho kwa watumishi wa Umma wote na wanasiasa wasio waadilifu!

Wizara ya Madini.

Napenda kupata kauli ya STAMICO ilikuwaje wakaingia huu Mkataba

Pia, soma;

Thread 'Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya' Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya.

Screenshot_20220531-140102.png
 
Kama ni kweli kuna shida ila ulitakiwa uweke ushahidi wa hicho unachoongea cha kuuza madini Kwa bei hiyo..

Pili kule Ruvuma kuna kampuni ya mzawa ya Ruvuma Coal Mining Limited ndio imekuwa ikisafirisha Makaa ya Mawe kwa mda mrefu,swali Je wao ndio wanauziwa Kwa bei Hiyo na stamico au wao Wana mgodi wao kama wawekezaji wengine wa madini?

Mwisho kuna Hawa jamaa wa Hiyo sekta wanafai makaa yetu yako daraja ya mwisho ndio maana hayana soko la uhakika pengoline hii ndio Sababu kama kuna ukweli.
 
aiseee hichi nacho ni kituko cha mwaka yani tani moja kwa elfu sitini jamani hii nchi hii inabidi iwe na sheria ya kunyonga kabisa!

Hivi ndio kufungua nchi huku? Hakika inachekesha na kuhuzunisha kwa wakati mmoja! Tunajisifu kwa meli kubwa eti imetia nanga kumbe makaa ya mawe ni kama yanaondoka bure kabisa na no one cares aiseeeee

Ngoja ni lale tuuu
 
aiseee hichi nacho ni kituko cha mwaka yani tani moja kwa elfu sitini jamani hii nchi hii inabidi iwe na sheria ya kunyonga kabisa!

Hivi ndio kufungua nchi huku? Hakika inachekesha na kuhuzunisha kwa wakati mmoja! Tunajisifu kwa meli kubwa eti imetia nanga kumbe makaa ya mawe ni kama yanaondoka bure kabisa na no one cares aiseeeee

Ngoja ni lale tuuu
Ushahidi please
 
Kama ni kweli kuna shida ila ulitakiwa uweke ushahidi wa hicho unachoongea cha kuuza madini Kwa bei hiyo..

Pili kule Ruvuma kuna kampuni ya mzawa ya Ruvuma Coal Mining Limited ndio imekuwa ikisafirisha Makaa ya Mawe kwa mda mrefu,swali Je wao ndio wanauziwa Kwa bei Hiyo na stamico au wao Wana mgodi wao kama wawekezaji wengine wa madini?

Mwisho kuna Hawa jamaa wa Hiyo sekta wanafai makaa yetu yako daraja ya mwisho ndio maana hayana soko la uhakika pengoline hii ndio Sababu kama kuna ukweli.

mkuu kila thread upo kuhakikisha mambo yanakwenda sawa hahahah
 
aiseee hichi nacho ni kituko cha mwaka yani tani moja kwa elfu sitini jamani hii nchi hii inabidi iwe na sheria ya kunyonga kabisa!

Hivi ndio kufungua nchi huku? Hakika inachekesha na kuhuzunisha kwa wakati mmoja! Tunajisifu kwa meli kubwa eti imetia nanga kumbe makaa ya mawe ni kama yanaondoka bure kabisa na no one cares aiseeeee

Ngoja ni lale tuuu
Ina maana tani moja ya makaa ya mawe tofauti ndogo na tani la mchanga
 
Kwani wewe mwana CCM ulivyokuwa unashangilia meli kubwa kutua mtwara nakusafirisha makaa ya mawe ulikuwa hujui yanasafirishwa kwa Tsh ngapi?
Makaa yanasafirishwa Mwekezaji mzawa kampuni ya Ruvuma Coal Mining Limited,huu ni mgodi kama migodi mingine na taratibu za migodini zinafuatwa .

Hakuna sababu za uzushi
 
Salaam Wakuu,

Imedaiwa Eti, Tanzania kupitia Stamico tumesaini mkataba wa kuuza Madini ya Makaa ya Mawe kwa dola 29.5 ambayo ni sawa na Shilingi 69,444 (Elfu sitini na tisa na Mia nne arobaini na nne tu) kwa Tani moja!

Bei ya Soko la Makaa ya Mawe kwenye Market Insider ni dola 315 sawa na shilingi za Kitanzania 740,250 (laki saba na elfu arobaini na mia mbili na hamsini).

Reuters wameripoti kuwa bei ya Madini ya Makaa ya Mawe inatazamiwa kupanda kwa mwaka 2022 kufikia dola za Kimarekani 500 sawa na shilingi za Kitanzania 1,175,000 (Milioni moja na laki moja na elfu sabini na tano)

Afrika Kusini wanauza makaa ya Mawe kwa bei ya Dola za Kimarekani 140.07 ambayo ni sawa na shilingi 329,164 hii ni bei iliyoporomoka toka kwenye bei ya Dola 214.27 sawa na shilingi 503,534 ya mwezi uliopita!

Ukiangalia bei ya Soko la Madini haya na wastani wa bei inaashiria dhahiri pasi na shaka kuwa Mkataba huu una viashiria vikubwa mno vya Rushwa!

Haiwezekani Madini yetu ya Makaa ya Mawe yauzwe kwa bei inayolingana na bei ya Kifusi cha Udongo/Mchanga!

Watoto na wajukuu zetu watakuta mapango na mashimo watatuuliza hapa palifanyika jambo gani?

Tukiwaambia palikuwa na Madini ya Makaa ya Mawe ambayo yaliuzwa kwa Tani elfu 69,444 watatulaani, watatutukana na kutuadhibu!

Ni heri haya Madini tuyaache vizazi vijavyo viyakute kuliko kuyachimba na kuyauza kwa Mikataba iliyojaa rushwa na Ufisadi!

Haiwezekani Mbuzi mmoja awe na thamani kubwa kuliko Tani moja ya Madini ya Makaa ya Mawe!

Naiomba Serikali kupitia vyombo vyake iuchunguze mkataba huu , iuvunje na ichukue hatua kali kwa kila aliyehusika kuruhusu Mkataba wa kifisadi kama huu ili iwe fundisho kwa watumishi wa Umma wote na wanasiasa wasio waadilifu!
Wizara ya Madini.

Napenda kupata kauli ya STAMICO ilikuwaje wakaingia huu Mkataba

Pia, soma;

Thread 'Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya' Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya
View attachment 2245667
kwa sasa kwenye mkoa wetu hiyo sawa na tan7 mchanga wa lipu.
 
Mawe ya huko ulikotaja yanafanana viwango na haya yakwetu? Lakini Tani 1 sio mengi mbona acha mama afungue nchi. Tim mwendazake mnawivu Sana nyie acheni mama aupige mwingi.
 
Back
Top Bottom