lowasa hapana bora hata huyo SITTaKama anatumiwa basi tusubiri Lowasa achukue ndo mtajua mbivu zipi mbichi zipi.
Mi ndo hapo naichoka Tanzania,fomu zimetangazwa waka ti tume haijamaliza kujumlisha kura ili kupata jumla ya wabunge 289. Je kuna wabunge wasiopata nafasi iyo kama wale ambao hawajatangaza?au wale watakaochaguliwa Nov.14 kama wale wa Nkenge? Tanzania vp? Acheni kupangia vyeo,mnawatangaza watu flan mapema ili kati ya walengo ndo wapate nafasi ya kugombea uspika? Hatari hii!
Magazeti mawili ya Majira na Tanzania Daima yametuhabarisha leo kuwa kuna mkakati mzito ndani ya CCM kumtupia virago vyake Mheshimiwa Samweli Sitta kwa mbinu nzito.........
Uchunguzi wangu umebaini ya kuwa mbinu na sababu za kumg'oa Sitta ni hizi hapa;-
1) Vibosile ndani ya CCM wamemshikia bango Sitta kuwa ndiyo chanzo cha CCM kuporomoka umaarufu kwa kuruhusu mijadala mizito ya ufisadi kama ile ya Richmond kutamba bungeni na hivyo kuwapa upinzani haswa Chadema nafasi ya kukidhoofisha chama chao................Kufanikiwa kwa mkakati wa kumng'oa Sitta kutahakikisha mijadala mizito ya utawala bora kuzimwa kila itakapokuwa inajitokeza bungeni..................................
2) CCM imefanya jitihada za makusudi kuwahamasisha makada wake wengi wenye majina ili kuzigawa kura na kujenga mazingira ya kumdondosha Mheshimiwa Sitta ndani ya vikao vya Chama hicho vitakavyoanza hivi karibuni.
3) Pamoja na Sitta kuwa ni mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho zipo hoja zinajengwa kuhakikisha asihudhurie vikao hivyo kwa madai ya kuwa yeye siyo spika tena kwa sababu bunge lililomchagua halipo tena kwani lilikwisha kuvunjwa na hivyo anakosa sifa za kuwa mjumbe wa vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa na Kamati kuu ya CCM............Lengo hapo ni kupunguza ushawishi ambao Mheshimiwa Sitta aweza kuutumia kutokana na kuwa na nyadhifa hizo ndani ya CCM.
4)Hoja nyingine ni kuwa CCM inajiundia rundo la visingizio vya kukataliwa kwenye chaguzi hii kuwa walikuwa hawateui vijana wengi kwenye nafasi za juu serikalini na hivyo ili kuonyesha wamebadilika nafasi ya uspika apewe kijana.....................lakini hiyo ni janja ya nyani ya kumn'goa Sitta ambaye pamoja na mapungufu mengine aliyonayo ya kuuzima mjadala wa Richmond kutokana na mashinikizo ya Ikulu lakini ameonyesha kujitahidi sana kupanua demokrasia bungeni ambayo wakati wa spika aliyemtangulia Bw. Pius Msekwa uhuru ndani ya bunge ulikuwa ni finyu mno............
ruta, itendee haki jamii ya wa tz ambao ni nutro, unataka kuhalalisha kuwa sita asipopitishwa ccm kugombea uspika hakuna mtanzania mwingine anayeweza kuendesha bunge kwa maslahi ya watanzania?. Unataka sita aendelee kuwa spika mpaka lini?. Haya ni mawazo mgando: its time for change. Tunataka sura mpya.
ruta, itendee haki jamii ya wa tz ambao ni nutro, unataka kuhalalisha kuwa sita asipopitishwa ccm kugombea uspika hakuna mtanzania mwingine anayeweza kuendesha bunge kwa maslahi ya watanzania?. Unataka sita aendelee kuwa spika mpaka lini?. Haya ni mawazo mgando: its time for change. Tunataka sura mpya.
Sura mpya ya Chenge? Sina matatizo na wagombea wengine wote waliochukua fomu, mimi nina tatizo na Chenge na km sura mpya ni Chenge basi CCM itakuwa haitutendei haki.
Hivi kwani CCM mmeishiwa watu? Chenge ni mjumbe wa CC, Kamati ya Maadili ya CCM [sijui kwa maadili gani aliyo nayo mpaka anaendesha gari haina leseni na tuhuma kibao za ufisadi, mikataba mibovu yote ametuingiza mkenge yeye]. Mjumbe wa NEC na mazagazaga mengine kibao. Hapo sikubaliani na wewe, ila kwa kuwa ni chama chenu endeleeni na fanyeni mpendavyo, siku za CCM zinahesabika.
Mkuu Mtanzania,
Ninakubaliana na wewe kuhusu minyukano ya makundi ya Sitta & Co. Vs Lowassa & Co. Uhasama huo naona bado unaendelea na kundi lolote litakalo-win nafasi ya Spika litakuwa linajiweka kwenye nafasi nzuri kwa ajili ya 2015.
Nina uhakika ndani ya CC hakuna mwenye uwezo wa kufungua mdomo na kutoa kasoro za Chenge [labda wewe mzee kwa kuwa mwana CCM unaweza kuniambia kama kuna mtu mwenye balls za kusema Chenge hafai na hivyo wakate jina lake]. Mbaya zaidi wajumbe wengi wa CC ni pro-Lowassa & Co. Sitta wanaweza kumkata jina kirahisi sana kutokana na kasheshe zilizomkuta kwenye Bunge la 9.
Kama CC ina nia njema na watanzani na Taifa kwa ujumla, basi ni bora wakate majina ya Chenge, Sitta, na Kilango maana wote hao wana camps zao. Mama Makinda pia sina imani nae sana.
All in all ni juu ya Kamati Kuu ya CCM na wabunge wake kuamua kusuka au kunyoa, maana salaam zimeishawafikia ni juu yao kukaidi na kuendelea mbele kukumbatia mafisadi na ufisadi au kubadilisha mwelelekeo.
SAWA CC INAWEZA KUWA NA WATU WENGISura mpya ya Chenge? Sina matatizo na wagombea wengine wote waliochukua fomu, mimi nina tatizo na Chenge na km sura mpya ni Chenge basi CCM itakuwa haitutendei haki.
Hivi kwani CCM mmeishiwa watu? Chenge ni mjumbe wa CC, Kamati ya Maadili ya CCM [sijui kwa maadili gani aliyo nayo mpaka anaendesha gari haina leseni na tuhuma kibao za ufisadi, mikataba mibovu yote ametuingiza mkenge yeye]. Mjumbe wa NEC na mazagazaga mengine kibao. Hapo sikubaliani na wewe, ila kwa kuwa ni chama chenu endeleeni na fanyeni mpendavyo, siku za CCM zinahesabika.
Mkuu Mtanzania,
Ninakubaliana na wewe kuhusu minyukano ya makundi ya Sitta & Co. Vs Lowassa & Co. Uhasama huo naona bado unaendelea na kundi lolote litakalo-win nafasi ya Spika litakuwa linajiweka kwenye nafasi nzuri kwa ajili ya 2015.
Nina uhakika ndani ya CC hakuna mwenye uwezo wa kufungua mdomo na kutoa kasoro za Chenge [labda wewe mzee kwa kuwa mwana CCM unaweza kuniambia kama kuna mtu mwenye balls za kusema Chenge hafai na hivyo wakate jina lake]. Mbaya zaidi wajumbe wengi wa CC ni pro-Lowassa & Co. Sitta wanaweza kumkata jina kirahisi sana kutokana na kasheshe zilizomkuta kwenye Bunge la 9.
Kama CC ina nia njema na watanzani na Taifa kwa ujumla, basi ni bora wakate majina ya Chenge, Sitta, na Kilango maana wote hao wana camps zao. Mama Makinda pia sina imani nae sana.
All in all ni juu ya Kamati Kuu ya CCM na wabunge wake kuamua kusuka au kunyoa, maana salaam zimeishawafikia ni juu yao kukaidi na kuendelea mbele kukumbatia mafisadi na ufisadi au kubadilisha mwelelekeo.