boyayoparuparu
JF-Expert Member
- Jul 30, 2015
- 343
- 81
Samweli sitta kwa maoni yangu ndie anaefaa kuwa spika wa bunge lijalo la jamhuri ya muungano wa Tanzania,tulioona alivyo endesha bunge kabla ya zengwe la mzee makamba,bunge lilikuwa huru wapinzani na ccm walikaribia kupewa nafasi sawa katika michango mbalimbali,pia nina imani kuwa kwa kuwa kwake nje ya uspika,atakuwa amejifunza kurekebisha alichokosea,sijasahau kuwa aliharibu kusaidia kuitupilia mbali katiba ya wananchi lakini kama mwanasiasa najua kuwa alipenda zaidi kukifurahisha chama ccm kwa lengo la kuja kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho,ningependa pia kumshauri kuwa iwapo atafanikiwa kuupata uspika,miswada inayokuja uhakikishe kuwa inajadiliwa kwa uhuru na kuhakikisha inafikia mwisho kwa kupata uamuzi wa kibunge, richmond leo bado inapigiwa kelele kwasababu muswada wa kuhusu richmond uliondolewa bila kuwa na uamuzi wa kibunge kuwaadhibu wahusika,nasema mzee sitta,ni mtu anaejiamini na mwenye msimamo,acha tabia ya kupima upepo baki na msimamo wako kwa kuzingatia maslahi ya wananchi