Eti kelbu mbili tu hadi sasa bado kanuna

Eti kelbu mbili tu hadi sasa bado kanuna

Mkuu pole, avatar yako ishaejieleza kilichopelekea ukampa kelbu shemeji..
 
Kusema ule ukweli, huyu shemeji/wifi yenu toka niwe nae huu ni mwaka wa 7 sasa na hata siku moja sijawahi kumtandika kibao hata kamoja.

Jana sasa Kuna sehemu tulikuwa tunaenda ni nje kidogo ya mji, nikaazima gari kwa rafiki yangu (maana mimi sina) tumeenda safari yetu vizuri tu sasa wakati wa kurudi tulipoanza kuingia mjini tukapita sehemu kuna kiji grosary tukaamua kugonga chupa zetu za bia mbili mbili na kilo moja ya kale ka nyama ambako wengine wanapiga kelele kuwa sir god amekapiga marufuku kuliwa (lakini wakiwa chemba wanabadilisha majina ili kujipa uhalali wa kukala).

Tulipomaliza tukaendelea na safari huku story zimekolea ghafla akaingia barabarani mwendesha bodaboda na mbele yetu zinakuja gari mbili huku zimetanua barabarani na nyuma yangu tena kuna gari inataka kuniovateki, kwa kihoro shemeji/wifi yenu akaniparamia mwilini kwa ghafla hadi nikataka kupoteza uelekeo.

Kwa harakaharaka nikaachia kelbu mbili za maana kwake akatulia,nikaweka utulivu barabarani ni solve kwanza tatizo lililokuwa linakaribia kutufika (tena ukizingatia hii ni December).

Nilipoweka mambo sawa nikapaki gari pembeni nikaanza kumlaumu sana kwa kitendo alichokifanya huku nikimwelezea na matatizo ambayo angesababisha nikaongezea na kumkumbusha kuhusu historia mbali mbali za Huu mwezi,yeye akawa yuko kimya tu.

Nikawasha gari safari hiyo hadi home kibubu bubu tu, asubuhi nikaenda kazini nilipotoka nikaenda kwenye kikao cha harusi ya rafiki yangu (sio yule aliyeniazima gari)saa hizi nimeingia home eti bado kanuna tu toka hiyo jana,sasa nauliza bandugu hivi Huyu mtu nikimuongeza kelbu nyingine nitakuwa nakosea kweli.
Wewe ndiyo kelb (mbwa) hukuna sababu yeyote inayokupa haki ya kumpiga si mkeo tu bali mwanamke yeyote. Watu wanaongea kwa mdomo siyo mikono huyo biniadamu siyo punda, hata punda wangeweza kutufanyia shughuli zetu bila kupigwa ila tumefanya waamini hawawezi kufanya kazi bila kupigwa. Wewe siyo unatakiwa uonyeshe ubabe kwa kumpiga tena mkeo kwa kukukasirikia, unatakiwa umuombe msamaha wa kweli aamini na umbembeleze, nguvu zako katumie katika masuala mengine ya maana siyo kujisifu umempiga makofi mkeo upo dunia gani.
 



Nikawasha gari safari hiyo hadi home kibubu bubu tu, asubuhi nikaenda kazini nilipotoka nikaenda kwenye kikao cha harusi ya rafiki yangu (sio yule aliyeniazima gari)saa hizi nimeingia home eti bado kanuna tu toka hiyo jana,sasa nauliza bandugu hivi Huyu mtu nikimuongeza kelbu nyingine nitakuwa nakosea kweli.
Kama ndio njia mnayotumia kusolve matatizo yenu muongeze unazoona zinafaa ili yaishe.
 
moja ya kale ka nyama ambako
wengine wanapiga kelele kuwa
sir god amekapiga marufuku
kuliwa (lakini wakiwa chemba
wanabadilisha majina ili kujipa
uhalali wa kukala).........
..... Aisee hapo kwenye hayo maneno nmecheka sana....
 
Mke hapigwi, akipigwa kwa upande wa khanga.

Mashikolo mageni, siku nyingine kabla ya kumpandisha kwenye gari inabidi umpe darasa kwanza, hapa ndipo unapofungia mkanda, ukiona kama ajali inakuja ufanye hivi, etc.

Sasa wewe mtu hata darasa hujampa unamzaba vi kelbu?
Huyu ana matatizo na kasahau fact kwamba he was "drinking and driving"!kisha anamlaumu mkewe kwa uzembe wake!Men men men!Mkewe ana kila haki ya kununa maana kaonewa!
 
Huyu ana matatizo na kasahau fact kwamba he was "drinking and driving"!kisha anamlaumu mkewe kwa uzembe wake!Men men men!Mkewe ana kila haki ya kununa maana kaonewa!

Duh,

Kibongobongo naona kama "Drinking and driving" siyo issue.

Siwezi hata kushangaa nikiambiwa traffic police hawana breathalyzers.
 
Back
Top Bottom