Eti JF ni CHADEMA?

Eti JF ni CHADEMA?

kwenu wanazuoni, wachambuzi, watafiti, watalaam wa JF na uongozi wa CHADEMA, asalaaaaaaaaaam Aleykum,

Leo nataka mnieleze uhusiano kati ya chadema na Jamii forums baada ya kufanana, kuoana na kurandana katika mambo yafuatayo;

(i) Rangi za ukuraza wa JAMII FORUMS zinafanana na rangi za BENDERA ya Chadema
(ii) Msimamo wa wana JF wengi na Chadema almost ni sawa.
(iii) Baadhi ya washirika wakuu wa JF pia ni washirika na viongozi wa Chadema
(iv) JF na CHADEMA wote kwa sasa wanadai wako kwenye vita dhidi ya ufisadi
(v) Walipua mabomu wa humu JF wanalipua na evidence (attachments) kama ilivyo kwa walipua mabomu wa Chadema (wazee wa nyaraka) ie Zito, Slaa, n.k
(vi) Kwa kufuatilia majadiliano mbalimbali ya humu JF inaonyesha kuna uhusiano wa kisiasa, kifamilia na ule wa kupashana habari kati ya wana JF na CHADEMA...

Kama kuna mtu nimemkwaza naomba aombe mungu amsamehe ila kwa sasa naomba kujifunza sihitaji kutukanwa wala kurushiwa maneno ya kejeri...

TUMSIFU YESU KRISTO



Kwani kuna rangi zilibatizwa kwamba ni za CHADEMA au za CCM pekee?

Mshiriki mkuu yupi huyo ambaye ni CHADEMA? Toa majina tafadhali. Mfano unaweza kusema Ole ni CHADEMA n.k.

Nani amesema JF iko kwenye vita?


Nani amekwambia JF wanalipua mabomu? Mabomu yanalipuliwa na wachangiaji wa JF ambao wanaandika yale yanayowakereketa kama wewe ulivyoandika hapa.

Hakuna uhusiano wowote kati ya JF na CHADEMA pengine uhusiano mkubwa ulioko ni wa CCM na JF kwani waliwachukua baadhi ya wanachama wake kwa nahojiano sijaona CHADEMA kuwa na mahojiano na uongozi wa JF.




Kama nimekukwaza naomba uombe mungu akusamehe ila kwa sasa naomba ujifunze, sihitaji kutukanwa wala kurushiwa maneno ya kejeli...

TUMSIFU YESU KRISTO
 
go to members list, find the name Freeman A. Mbowe, angalia hoja zake zilivyo na rangi.. tehetehe!

hayo majina unayajua wewe kwa ufaham wangu humu unaweza kujiita jina lolote..humu kuna watu wanajiita 50cent so naomba uchangie maada hii acha kunichonganisha na watu mie nimetaka nifahamu nyie mnalichukuliaje shwala hili...tafadhari
 
Hii thread inatupotezea muda wa kujadili issue za maana!
Sasa kama hupendi chadema kwani ccm hawana mitandao ambayo unaweza kwenda huko na kusympathize?
Mimi hapa nimekuwa huru bila chama na bado na enjoy mijadala ya JF!
 
hayo majina unayajua wewe kwa ufaham wangu humu unaweza kujiita jina lolote..humu kuna watu wanajiita 50cent so naomba uchangie maada hii acha kunichonganisha na watu mie nimetaka nifahamu nyie mnalichukuliaje shwala hili...tafadhari
soma michango yake ujue kama ni yeye au la, acha kukimbilia hukumu, vinginevyo futa thread yako basi
 
Halafu wakiona eti kuna chama kinaendelea kupata umaarufu wao wanaanza kulaumu mitandao!
We unafikri kuna watu wanalazimishiwa kujadili chama ambacho tumeshakijadili vya kutosha na sasa ukikitaja unajisikia kutapika?
 

Kwani kuna rangi zilibatizwa kwamba ni za CHADEMA au za CCM pekee?

Mshiriki mkuu yupi huyo ambaye ni CHADEMA? Toa majina tafadhali. Mfano unaweza kusema Ole ni CHADEMA n.k.

Nani amesema JF iko kwenye vita?


Nani amekwambia JF wanalipua mabomu? Mabomu yanalipuliwa na wachangiaji wa JF ambao wanaandika yale yanayowakereketa kama wewe ulivyoandika hapa.

Hakuna uhusiano wowote kati ya JF na CHADEMA pengine uhusiano mkubwa ulioko ni wa CCM na JF kwani waliwachukua baadhi ya wanachama wake kwa nahojiano sijaona CHADEMA kuwa na mahojiano na uongozi wa JF.




Kama nimekukwaza naomba uombe mungu akusamehe ila kwa sasa naomba ujifunze, sihitaji kutukanwa wala kurushiwa maneno ya kejeli...

TUMSIFU YESU KRISTO

Nashukulu kwa mtazamo wako mkuu,,,pia ni faraja kwangu kwa mtu kama wewe unaenipika kila siku kuchangia maada yangu...anyway your my moderator and i respect what your doing so do same kwa wanafunzi maana naona kama umetoa tamko rasmi lenye kukanusha
 
Yani badala ya kujadili mustakabali wa nchi tunajadili rangi?
Watanzania tuamke na hizi siasa za kisimba na yanga kwasababu zitatuzika wazima wazima!
Yani watu wasishiriki mijadala ya JF kwasababu wanarangi za kinini eti?
Yani unataka kusema kuwa Yanga wote ni CCM?
Ama kila mwananchi ni CCM kwasabau bendera ya taifa ina njano na kijani?
Ifungwe hii!
 
Halafu wakiona eti kuna chama kinaendelea kupata umaarufu wao wanaanza kulaumu mitandao!
We unafikri kuna watu wanalazimishiwa kujadili chama ambacho tumeshakijadili vya kutosha na sasa ukikitaja unajisikia kutapika?

Nasubiri mchango wako mkuu nafahamu wewe ni mchambuzi mzuri na sio mtu wa kurukaruka namna hiyo...acha siasa jibu hoja
 
kwenu wanazuoni, wachambuzi, watafiti, watalaam wa JF na uongozi wa CHADEMA, asalaaaaaaaaaam Aleykum,
Bahati mbaya sijui namna ya kuijibu hii salaam. Ndefu sana ingawa inaelekea ya kiislam (lakini sivyo iandikwavyo).

Leo nataka mnieleze uhusiano kati ya chadema na Jamii forums baada ya kufanana, kuoana na kurandana katika mambo yafuatayo;
Sawa sheikh, ngoja nizipitie moja baada ya nyingine ili kuona ukweli wenyewe... Labda yaweza kuwa kweli!

(i) Rangi za ukuraza wa JAMII FORUMS zinafanana na rangi za BENDERA ya Chadema
Tuziangalie hizi bendera kwanza...

CCM:
ccm_flag_anim.gif


CHADEMA:
flag3.gif


NCCR Mageuzi:
powered_by.png


CUF:
CUF_partylogo.png


Zanzibar (bendera)
75px-Flag_of_Zanzibar.svg.png


Sasa katika hoja yako najaribu kuangalia kwanini useme rangi ni za CHADEMA....

Rangi za Logo ya JF (ambayo ni ya muda hata hivyo na ndiyo inaweza kulinganishwa na rangi ya chama flani ama taifa flani...)

logo.gif


Ndani ya Logo yetu kuna rangi za Bendera ya Zanzibar, Bendera ya Tanzania, bendera ya CCM, bendera ya NCCR, CUF, CHADEMA etc.

Hoja kuwa CHADEMA na JF zina rangi sawa ni hoja ya kiuchochezi na sikubaliani nayo kwa kiwango kikubwa. CHADEMA rangi yao almost 30% ni RED na nyingine almost 30% ndiyo inaelekea kuwa karibia na ya JF nyeusi nasi tunayo na white ndiyo haikwepeki!

Naomba kuanzia leo onwards hii hoja ife na wenye mawazo ya kufananisha JF na CHADEMA kirangi basi wajue hiyo si hoja ya kusimamia.
(ii) Msimamo wa wana JF wengi na Chadema almost ni sawa.
Basi sema misimamo ya watanzanania (zaidi ya milioni 6) ambao wanaitembelea JF kwa mwezi ndiyo sawa na CHADEMA including YOU!

(iii) Baadhi ya washirika wakuu wa JF pia ni washirika na viongozi wa Chadema
Washirika wakuu sijaelewa unawalenga kina nani... Kama ni Zitto, Mnyika na Kitila basi unakuwa umechemsha kidogo mkuu... Yupo mtu 'mkubwa' zaidi ya Zitto humu na anatumia nick sawa na mimi na wewe. Tena ni mwanachama asiyekosa kila leo! Think of it,,, naye si kutoka CHADEMA bali CCM.

(iv) JF na CHADEMA wote kwa sasa wanadai wako kwenye vita dhidi ya ufisadi
Kama ni "kwa sasa" kwa maelezo yako basi unakuwa unakosea ndugu yangu... JF ni sehemu ya Jamii ya watanzania, basi watanzania wote ni wa kulaumiwa kuwachukia mafisadi.
(v) Walipua mabomu wa humu JF wanalipua na evidence (attachments) kama ilivyo kwa walipua mabomu wa Chadema (wazee wa nyaraka) ie Zito, Slaa, n.k
Hoja yoyote bila evidence ni uchochezi na ndo maana mara zote huwa tunataka ushahidi. Bila ushahidi unakuwa ni mdaku na mwongo mkubwa. Hili si suala la wewe uwe CHADEMA ama uwe CCM. Evidence ni muhimu popote. Haya si mabomu... Ni ukweli wa mambo!

(vi) Kwa kufuatilia majadiliano mbalimbali ya humu JF inaonyesha kuna uhusiano wa kisiasa, kifamilia na ule wa kupashana habari kati ya wana JF na CHADEMA...
Labda unasahau kuwa hiki ni chombo cha watu kupashana habari, kama na CHADEMA ndivyo walivyo basi si chama cha siasa tu bali cha kupashana habari. Au ulilenga kusemaje hapa mkuu? Huenda sijakusoma vema.

Kama kuna mtu nimemkwaza naomba aombe mungu amsamehe ila kwa sasa naomba kujifunza sihitaji kutukanwa wala kurushiwa maneno ya kejeri...
Hahaha, kusema huhitaji kutukanwa ama kurushiwa maneno ya kejeli unakuwa unasahau kuwa 'penye wengi pana mengi pia'. Pia kumbuka kuwa ukifanya jambo kwa kutarajiwa kupigiwa makofi, tarajia kuzomewa pia!

TUMSIFU YESU KRISTO
Ooops,,, mi nilidhani wewe maalim mkuu...? Sasa umeanza kama kiislam unaishia kikristo?

Ahansate na natumaini nimepunguza kiu yako.

haya mawili yanakuonyesha jinsi ulivyo,yaani unapenda kuchanganya mambo. Rangi zimeumbwa na mungu wala hazihusiani na chama chochote. wakati fulani Michael Jackson alifika hapa Bongo akiwa amevalia shati la kijani na surali nyeusi, alikuwa ni CCM?
Hahaha, well nadhani ulikuwa ni mtizamo wake. Kama hajaridhika na maelezo yangu na viambatanisho (ambavyo huenda akaona nimefanya ki-CHADEMA kwa kuweka attachments 🙂 ) basi anakaribishwa kutoa maelezo ya ziada.

Na hoja zinazotolewa nazo zina rangi?
Kuna KadaMpinzani, yeye rangi zake za maandishi siku za nyuma (naona nowadays kasahau) zilikuwa ni green tu. Kwa sababu hiyo tungesema JF ni sehemu ya CCM tu. Au tuondoe option ya kuandika kwa rangi ili kuepusha JF kufananishwa ama kuhusishwa na vyama flani.

Mkuu nyerererist, muige wa-jina wako. Kuna kitu zaidi nyuma ya ukuta ulio mbele yako. Think of it!
 
Invisible Umepiga kwenyewe.Hoja Imejibiwa kwa hoja kali
 
mkuu tuko vyama mbali mbali hapa, na sote tunakata issue na wala hakuna kiingilio katika kujiunga kwa hio kama wana CUF au NLD ambao walitiana ngumi bwawani waje hapa kutoa hoja zao wanakaribbishwa.


kuhusu rangi inategemea mvuto na pahala.


karibu miti yote ni kijani na haimaanishi kuwa mungu anakipendelea CCM au bahari kuwa blue haina maaana kuwa CHADEMA wao ndio wamiliki wa bahari.


na moja hizi rangi ziliumbwa mwanza kuliko vyama sasa wao kuwa na rangi zinazofanana na vitu vyengine haifanyi kuwa wao wamiliki wa vitu hivyo.

suala la kuwa wachangiaji wengi ni chadema mie nnaamini ni kweli, huenda chadema wanaamini kuwepo hapa ndio kunadi sera zao.

sisi CCM tunaamini kuwafikia wananchi ndio kiboko na ndio maana uchaguzi wa kiteto tulishinda maana tulijikita kule wakati wenzetu wao walikesha hapa na kama ungekuwa ukisoma hapa ungeona CHADEMA weshanyakua jimbo.


usikonde huo ndio mchango wangu maalim nyerererist
 
mimi sielewi kwa nini tujadili haya mambo!! kama mtu hapendezewi na rangi za jamii forums basi aanzishe ya kwake na aweke rangi anazopenda (i mean kujani kibichi kwa wingi).

Tukishakuwa na mambo ya uvyama basi tutataka kujimilikisha kila kitu. tutaanza kusema maji ya bahari ni ya chadema na matawi ya miti yote ni ya CCM.
 
karibu miti yote ni kijani na haimaanishi kuwa mungu anakipendelea CCM au bahari kuwa blue haina maaana kuwa CHADEMA wao ndio wamiliki wa bahari.

mkuu mtu wa pwani, umenichekesha na hii sentensi, its pure logic.
Sometimes we fail to see the bright moon and stare at the finger pointing to the moon, I guess we should ask why are there many issues against the rulling party? is it that people dont like it? i bet not but everyone is caught with the hardship and machungu ya result ya rulling party, Any party stands the chance of being critisized, and thats exactly what we do here, Give credit when its due, and critisize when neccessary.
I admire michango ya mwanaCCM mmoja humu, when the party does bad he admits when CCM does Good he gives credit. He even gives credit even when the other parties do well. A
Lets stick to the focus ya jukwaa, sote twataka kuona our beautiful Tanzania flourish with good leadership, good governance, regardless kinaongoza chama gani, as simple as that.
 
..... why are there many issues against the rulling party? is it that people dont like it? i bet not but everyone is caught with the hardship and machungu ya result ya rulling party, Any party stands the chance of being critisized, and thats exactly what we do here, Give credit when its due, and critisize when neccessary.
Good kinyau! That's what I told the guy.

"Ukishangiliwa sana, kubali kuzomewa pia".

Hata hivyo issue hii ya rangi imekuwa ikiongelewa na wengi and I wonder why. Kama bendera nilizoweka zote hazina rangi inayoelekeana na ya JF ni ya CHADEMA tu then kweli wana JF tuna haki ya kuhojiwa kuwa hivi.

Na: Suala la itikadi/misimamo ya wanachama wa JF ni la wazi kuwa ni watanzania walio wengi wako hivi. Kama mwenzetu haamini basi alinganishe matokeo ya uchaguzi ifikapo 2010 na ya mwaka 2005. Si mtabiri mimi lakini ni wazi yatakuwa na utofauti mkubwa tu.

Tanzania ya leo sio ya jana!
 
Wakati tukisherehekea miaka mitatu ya jamvi letu tukufu, Kuna watu huko wanatusema eti sie wapenzi na wafia damu wa JF eti ni Chadema! Huko katika globu ya misoup... ni kweli jamani?
 
Wewe unasemaje? Sema wewe kwanza kabla sisi wengine hatujasema kwani wewe ndo umeyasikia hayo mitaani.
 
Kwa kuwa wewe ni Chadema na ndio sababu upo JF inawezekana ni chadema.
Acha kueleza mambo ya blogu maana hapa tuko kwenye forum ya great thinkers. Low thinkers sijui watakuwa wako wapi sasa hivi!
Una swali jingine?
 
Back
Top Bottom