Eti jeshi linamtetea aliyeua watoto

Eti jeshi linamtetea aliyeua watoto

Kumbe na wewe hukuwepo eneo la tukio..so huna ushahidi...zaidI ya kukopI ya gazetinI ambapo nao hawakuwepo...naamini huyo meja sio mjinga

Kama sio mjinga ni punguani au --------. Msiwatetee wauwaji kavunja katiba, kavunja haki za binadamu. Kila mtu kazaliwa huru na ana haki ya kuishi. No one is above the law. Huyo ahukumiwe tu kunyongwa na sio blaa blaa za hapa JF.
 
Tusichangie kishabiki tafadhali maisha ya binadamu yamepotea hapo ,matukio ya baadhi ya askari wa majeshi yetu kuua raia bila wao kuchukuliwa hatua zinazostahili ni mengi sana yametokea hivyo inawezekana kabisa huyo Meja aliua huku akijua hakuna wa kumuwajibisha.Tusifurahie vifo kwa binadamu wenzetu leo kwao kesho kwako ,inafaa tukemee sote kwa sauti moja.Jana kwa walioangalia taarifa ya habari I.T.V iliripotiwa police kuwalipua kwa mabomu ya machozi kina mama waliokuwa wakirudi majumbani mwao nyakati za usiku na walikuwa wametoka ktk mkesha wa ibada ya krismass na sote tuliona ni kwa jinsi gani walijeruhiwa vibaya miguuni kwao na walikuwa wamelazwa hospital ,kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas nae aliwatetea askari wake kuwa kina mama hao walikuwa wakiwarushia polisi mawe.

Kila tukio baya linapotendwa na baadhi ya askari wa majeshi yetu dhidi ya raia ,wakubwa wao wmekuwa wakitoa utetezi usiojitosheleza .

Kwani wakati anatenda hili alikuwa katika kutekeleza majukumu yake ya kikazi? Usichanganye madesa, askari ni binadamu kama wewe? Kama angeua wakati akiwa kazini, hoja yako ingesimama. Lakini wakati akiwa mtaani haiwezi kufananishwa na mauaji ya kutumika kisiasa etc.
 
Sikusema kuwa nina ushaahidi ila anapotokea mtu tena mzito kutoia ufafanuzi wa jamboa ambalo kaambiwa na mtuhumiwa sidhani kama ni sawa. unless amesikiliza pande zote amejiridhisha na hapo sasa inakuwa ni mahahaka.

Thibitisha kwamba ametumia maelezo ya mtuhumiwa pekee.
 
Halafu ninashangaa kuwa jeshi kama institution inajiingiza katika criminal case ya mtu mmoja. Yaani ingekuwa kwamba kila insitutuion inaingia kutetea wafanyakazi wake katika criminal cases, basi mahakimu wote wasigewahi kupatikana na hatia. Kwa nchi kama marekani, magavana, maseneta na wabunge wote wa congress wasigewahi kufungwa.
 
Tusichangie kishabiki tafadhali maisha ya binadamu yamepotea hapo ,matukio ya baadhi ya askari wa majeshi yetu kuua raia bila wao kuchukuliwa hatua zinazostahili ni mengi sana yametokea hivyo inawezekana kabisa huyo Meja aliua huku akijua hakuna wa kumuwajibisha.Tusifurahie vifo kwa binadamu wenzetu leo kwao kesho kwako ,inafaa tukemee sote kwa sauti moja.Jana kwa walioangalia taarifa ya habari I.T.V iliripotiwa police kuwalipua kwa mabomu ya machozi kina mama waliokuwa wakirudi majumbani mwao nyakati za usiku na walikuwa wametoka ktk mkesha wa ibada ya krismass na sote tuliona ni kwa jinsi gani walijeruhiwa vibaya miguuni kwao na walikuwa wamelazwa hospital ,kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas nae aliwatetea askari wake kuwa kina mama hao walikuwa wakiwarushia polisi mawe.

Kila tukio baya linapotendwa na baadhi ya askari wa majeshi yetu dhidi ya raia ,wakubwa wao wmekuwa wakitoa utetezi usiojitosheleza .

ya dito utaambiwa meja kaua bila kksudia nchi hii inawenyewe bana. utetezi aikubaliki ukishakuwa mtuumiwa lazima ushtakiwe. wakamtete mahakamani . kule itajulikana kama mjeda ALIZINGIRWA NA HAO WATOO au aliwakosakosa kuwagonga na gari wakamrushia mawe naye akarusha risasi
 
Wale jamaa walioparamia gari unawaita watoto waliokuwa wanasherehekea mwaka mpya ila wangemuua aliyejihami mngeanza kuilaumu polisi na kumtukana mwanajeshi kwa kumwita lege lege....Niwape pole marehemu tu ila iwe funzo kwa vijana hawa wahuni wanaotumia furaha yao vibaya kuharras wengine!
 
  • Thanks
Reactions: y-n
Hivi kwa akili yako finyu unafikiri Jeshi halina maelezo ya pande zote mbili???
Sikusema kuwa nina ushaahidi ila anapotokea mtu tena mzito kutoia ufafanuzi wa jamboa ambalo kaambiwa na mtuhumiwa sidhani kama ni sawa. unless amesikiliza pande zote amejiridhisha na hapo sasa inakuwa ni mahahaka.
 
Wewe ndio unakurupuka. Habari hii iliripotiwa mapema zaidi humu jf na wadau wengi walipata balanced story. Sipendi kurudia hasa kwa vile wewe unaongozwa na emotions. Wewe mtu akitaka kukubaka utatulia amalize ili upate ushahidi? Lakini kitu ninachojiuliza, hawa watoto walikuwa,wanafanya nini barabarani saa saba usiku? Hivi wana wazazi hawa?

Haya kumekucha Tanzania. Kweli Internet imetuletea mambo! Mtoto anayezurura barabarani saa saba usiku wakati wa mkesha wa mwaka mpya adhabu yake ni kuuawa kwa kupigwa risasi!
 
Wewe umejuaje na kwa nini unaamini mwanajeshi sio mjinga?kama ana mtindio je?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Wale jamaa walioparamia gari unawaita watoto waliokuwa wanasherehekea mwaka mpya ila wangemuua aliyejihami mngeanza kuilaumu polisi na kumtukana mwanajeshi kwa kumwita lege lege....Niwape pole marehemu tu ila iwe funzo kwa vijana hawa wahuni wanaotumia furaha yao vibaya kuharras wengine!

Unaua watoto wawili kwa sababu wameparamia gari yako? Realy? Watu wengine akili zenu zinafanya kazi kama za mbwa... mpaka tukio likukumbe wewe au mtoto wako ndio utajua ubaya wake!
 
watoto wanalala mapema, sasa hawa usiku wa manane unawaita watoto? hata mimi na msapoti....

Watu wenye mawazo rahisi kama wewe ndio kesho unasikia ni viongozi... au si ajabu wewe ni kiongozi ... balaa kubwa!
 
Thibitisha kwamba ametumia maelezo ya mtuhumiwa pekee.

Kama unajua utuambie ila wakati anasema hakutaja upande wa pili aliakisi maelezo ya upande mmoja ambayo maana yake upande mwingine haujaulizwa. Hata hivyo hiyo ni kazi ya mahakama na sio jeshi kwa sababu kesi hiyo ipo mahakamani.
 
Unaua watoto wawili kwa sababu wameparamia gari yako? Realy? Watu wengine akili zenu zinafanya kazi kama za mbwa... mpaka tukio likukumbe wewe au mtoto wako ndio utajua ubaya wake!

Hili ni tusi la kwanza kulipokea rasmi kwa mwaka huu...nashukuru,leta na mengine!
 
Kwa sababu Jeshi ni taasisi sio wendawazimu kama nyie mnawaza mambo kwa kutumia moyo badala ya ubongo.

What a foolish answer! Pengine hata maana ya neno taasisi hujui! Kitu kishakuwa taasisi ndio by default hakikosei! Ni taasisi ngapi Tanzania zimesema zinatoa majibu ya uongo kila kukicha! Haloo kalale kama umechoka
 
Haya kumekucha Tanzania. Kweli Internet imetuletea mambo! Mtoto anayezurura barabarani saa saba usiku wakati wa mkesha wa mwaka mpya adhabu yake ni kuuawa kwa kupigwa risasi!

Hujui ulisemalo kijana. Watu kadhaa wmeripoti kupigiwa magari yao kama sehwmu ya sherehe za mwaka mpya. Hata hivyo bado swali halijajibiwa, mtoto anakwenda kuzurura usiku wa manane kisa sherehe za mwka mpya? Kizazi cha dot com mnaokwenda na watoyo wenu baaa. Hovyo kabisa.
 
Back
Top Bottom