Eti jeshi linamtetea aliyeua watoto

Eti jeshi linamtetea aliyeua watoto

Lakini wewe huoni pana walakini kwenye hii issue ya mwanajeshi aliyeua? Kwanini jeshi likurupuke kumtetea mtu aliyeua wakati bado mazingira ya kuua hayajafanyiwa uchunguzi? Wa kusema ANA au HANA makosa ni mwajiri wake au ni mahakama? Nadhani waafrika wengi bongo zetu zimeathiriwa na mazingira tunayokulia ndio maana hatuoni uzito wa mtu kuua au kuuawa!

Mkuu hapa kuna hoja mbili.

1: je huyo mjeshi kulikua na ulazima wa kuua hao watoto, kipi cha hatari walichokifanya hadi kufikia hatua ya ya kuwatoa uhai. Je walivunja kioo, walikwaruza gari kwa namna yoyote au walizui njia.?

2:kwa nini Jeshi likurupuke kumtetea kamanda wao.?
Kwa sababu hili ni kosa binafsi wala hakuepo kazini, alikua kwenye mizunguko yake.

Au sheria za jeshi zinaruhusu kamanda aliefanya uhalifu uraiani kutetewa na Taasisi.?
 
Juzi ilipobandikwa taarifa ya mauaji niliandika hapa kuwa kuna kila dalili zinazoonesha mjeda huyo ataukwepa mkono wa sheria pamoja na kujisalimisha kituo cha polisi...
 
Kwanini waweke mawe baraarani?

Sijasoma sehemu yoyote iliyosema waliweka mawe barabarani, zaidi ya kusema walikua wanasherekea kwa fujo na kuzonga magari ya watu.

Labda unionyeshe bandiko lanalosema waliweka mawe barabarani.?
 
Juzi ilipobandikwa taarifa ya mauaji niliandika hapa kuwa kuna kila dalili zinazoonesha mjeda huyo ataukwepa mkono wa sheria pamoja na kujisalimisha kituo cha polisi...
Mkuu taarifa zingine zinasema alikamatiwa Nyumbani kwake sasa sijui zipi ni zipi.
 
wakati watoto wanasherehekea mwaka mpya huko pugu kinyamwezi

huyu mwanajeshi alipita na gari yake sasa inasemekana
wale watoto waliipiga ile gari na mikonoi kwa furaha za mwaka mpya

basi yule meja akatoa pisto akawapiga risasi,

watu wa pale wakaripoti polisi na polisi walipofika walipelekwa nyumbani kwa yule meja wakakuta anaondoka na gari nyingine wakamshika.

Naskia walikufa wanne lakini leo nimesikia magazetini kuwa ni wawili.


acha kuish kwa tetesi.km haujaridhika au kuna maali unaona meja anapendelewa peleka ushaidi kuthibitisha ukweli wako
 
acha kuish kwa tetesi.km haujaridhika au kuna maali unaona meja anapendelewa peleka ushaidi kuthibitisha ukweli wako

Utetezi kama wako hupenda hutolewa na wahalifu.... ''kama una ushahidi......'' Unauwa watu wawili halafu unasema ''kama una ushahidi!''
 
Tusichangie kishabiki tafadhali maisha ya binadamu yamepotea hapo ,matukio ya baadhi ya askari wa majeshi yetu kuua raia bila wao kuchukuliwa hatua zinazostahili ni mengi sana yametokea hivyo inawezekana kabisa huyo Meja aliua huku akijua hakuna wa kumuwajibisha.Tusifurahie vifo kwa binadamu wenzetu leo kwao kesho kwako ,inafaa tukemee sote kwa sauti moja.Jana kwa walioangalia taarifa ya habari I.T.V iliripotiwa police kuwalipua kwa mabomu ya machozi kina mama waliokuwa wakirudi majumbani mwao nyakati za usiku na walikuwa wametoka ktk mkesha wa ibada ya krismass na sote tuliona ni kwa jinsi gani walijeruhiwa vibaya miguuni kwao na walikuwa wamelazwa hospital ,kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas nae aliwatetea askari wake kuwa kina mama hao walikuwa wakiwarushia polisi mawe.

Kila tukio baya linapotendwa na baadhi ya askari wa majeshi yetu dhidi ya raia ,wakubwa wao wmekuwa wakitoa utetezi usiojitosheleza .
Acha kuchanganya habari,

wale vijana waliuwawa kwasababu walikua wanahatarisha hali ya usalama wa mwanajesh na familia yake... Tanzania ya sasa sio ile ya zamani, hatuaminiani, labda ningekua mimi ningefanya hayohayo kutokana na tukio

saa saba usiku watu wanazingira gari yako na kuibutua kwa namna yoyote ile bila kujua una nini ndani ya gari au wewe ni jambazi au la, unadhani hao ni watu wa kawaida?
kilichotufikisha hp ni umaskini, rushwa, ufosadi, na mambo yote yasiyoma nafasi raia maskini kuziweka mbivu na mbichi sehemu husika

it is a sad reality lakini ni vigumu kusema kwa asilimia mia kwamba mwanajeshi kakosea
 
Inasikitisha lakini kwa muda na mambo waliyofanya hao watoto sishangai mtu anapojihami
 
Na wewe kwa akili yako ''pana sana'' umejuaje jeshi lina maelezo ya pande zote? Walikupatia wewe?

Jeshi haliwajibiki kwa mjinga mmoja kama wewe. Common sense inakutaka uache uchunguzi huru ufanyike, huenda mjeshi akanyongwa ili furaha yako itimie. Chuki zako dhidi ya jeshi zitakumaliza wewe mwenyewe.
 
Labda hamjakutana na vijana wamekula bangi ya kutosha hua haana salia mtume alafu msiyaaminisana vyombo vya
Habari manake saivi vinreport tu habari za E
L sijuikafahivi kafanya vile ooh mara amejikwaa hamna kitu vimeshanunuliwa
 
Kama ni Watoto wangekuwa nyumbani kilichofanyika ni halali kabisa na ndicho walichopanda watu wajifunze na hido ndiyo dawa la maadili ya kihuni mtaani. Cheers mjeshi
Haiingii hakilini jeshi kusimama na kumtetea meja aliyeua watoto waliokuwa wakisherehekea sikukuu ya mwaka mpya. Hivi chombo kama jeshi kinaweza kuwa kinakurupuka hivi jamani, inamtetea kwanza hakijui mazingira ya tukio kwa sababu aliyekuwepo ni mtuhumiwa peke yake na hao watoto, wamewauliza watoto wengine wakasema wale walikuwa vibaka ???Hata kijana wa form six anaweza kuwa reasonable kuliko hao wanaotaka kumtetea huyu jamaaa. Ushahidi wa huyu meja ni nini? gari yake haina sehemu yoyote kuonesha kuwa waliipiga, hajachaniwa nguo, hakuna kitu chochote kuonesha kulikuwa na purukushani, sasa nini jeshi linakaa na kuanza kumytetea??? jeshi lilikuwepo kwenye tukio????

nimesikia kwenye magazeti leo asubuhi. . . .
 
Wakati watoto wanasherehekea mwaka mpya huko pugu kinyamwezi huyu mwanajeshi alipita na gari yake sasa inasemekana wale watoto waliipiga ile gari na mikonoi kwa furaha za mwaka mpya basi yule meja akatoa pisto akawapiga risasi, watu wa pale wakaripoti polisi na polisi walipofika walipelekwa nyumbani kwa yule meja wakakuta anaondoka na gari nyingine wakamshika. Naikia walikufa wanne lakini leo nimesikia magazetini kuwa ni wawili.

Hao watoto wana umri gani mkuu?
Just wanapita wanasherekea then mwanajeshi akatoa pisto akawapiga risasi, simple like that??
 
Unaua watoto wawili kwa sababu wameparamia gari yako? Realy? Watu wengine akili zenu zinafanya kazi kama za mbwa... mpaka tukio likukumbe wewe au mtoto wako ndio utajua ubaya wake!
Nadhani hata huyo Meja aliyefanya hivyo ingekuwa sio yeye halafu asimuliwe tukio kama hili isingemuingia akilini na si ajabu angetoa lawama kwa muuaji.
 
Ukinionyesha sheria yeyote inayosema mtoto akizurura usiku wa manane mwaka mpya basi na auwawe kwa kupigwa risasi basi kweli nitaamini sijui nilisemalo!

Kijana tuliza munkari, kuna matukio ambao watoto wameua wazazi wao na wazazi watoto wao. Hapa kinachogomba ni mazingira. Wewe unaendesha gari usiku mnene, mara kundi la vibaka linatokeza mbele yako na kuonyesha shari. Tuna namna tofauti ya ku react. Meja kaamua kujihami kwa kuchomoa bastola yake. Baada ya kuondoka salama eneo la tukio, inadaiiwa kiwa wale ni "watoto wa waungwana" wala si vibaka. Na kama ni watoto hoja ya msingi inakuwa, wazaxi walijua waliko watoto wao muda ule? Make no mistake, usimchezee usiyemjua usiku wa manane. Nchi hii imeharibika, haaminiwi mtu, labda ni wewe tu unayeweza kutoka kwenye gari kuwauliza usiowajua kama wanakutania tu ama wanataka kukidhuru.
 
Unaua watoto wawili kwa sababu wameparamia gari yako? Realy? Watu wengine akili zenu zinafanya kazi kama za mbwa... mpaka tukio likukumbe wewe au mtoto wako ndio utajua ubaya wake!
Inasikitisha sana kwakweli hasa baada yakusikia umri wao huo mdogo. Ila hebu tutafakari kama kweli watu wanakuja kulizingira gari lako tena usiku wa saa 7? Je utatambuaje kama hawa ni watoto? Tunaambiwa wapo wa miaka 16, sasa je kimaumbile tu tena kwenye giza kuna utofauti gani mtu wa miaka 16 na 18,20-23? Nadhani tuungane kuwapa Pole lakini tusimlaumu sana Mjeda kwa mazingira hayo; PIA IPO SIKU NAWE INAWEZA IKAKUTOKEA MAZINGIRA TOFAUTI NA HAYO KISHA UKACHUKUWA MAAMUZI YAKUSHANGAZA. Tuwalaumu wazazi/walezi kwani hata mimi siwezi kukubali kijana wangu mdogo akae barabarani kuchoma matairi nakusimamisha magari ya watu. Inawezekana huyo Mjeda ameshawahi kuishi Marekani kwani ndio zao hizo, huwezi kuingilia mali za mtu bila sababu. Angalia tu yule kijana mdogo wa Marekani aliyeuawa na jirani yao kisa alihisiwa mwizi alipokatisha kwenye nyumba ya jirani yao huyo. Tukio hilo liliwachukiza wengi sana na hata Obama alikasirishwa lakini mahakama ilimuachia huru yule jamaa.
 
Mkuu hapa kuna hoja mbili.

1: je huyo mjeshi kulikua na ulazima wa kuua hao watoto, kipi cha hatari walichokifanya hadi kufikia hatua ya ya kuwatoa uhai. Je walivunja kioo, walikwaruza gari kwa namna yoyote au walizui njia.?

2:kwa nini Jeshi likurupuke kumtetea kamanda wao.?
Kwa sababu hili ni kosa binafsi wala hakuepo kazini, alikua kwenye mizunguko yake.

Au sheria za jeshi zinaruhusu kamanda aliefanya uhalifu uraiani kutetewa na Taasisi.?

Kwanza nawapa pole wafiwa wote kwa janga hili.

Tukirudi kwenye tukio nafikiri jeshi linatakiwa kumchukulia hatua mwanajeshi yeyote anayeshiriki ktk matukio kama haya labda ndiyo maana wanakuja na utetezi ni kwa nini hawakuchukua hatua hizo kama kumweka quarter guard (kumfunga katika mahabusu ya wanajeshi). Kumbuka hawa wana polisi wao wakijulikana kwa mavazi yao ya MP (Military Police).

Mimi siwezi kuhukumu hapa kwani sikuwepo na habari zinatofautiana has juu ya nini kilijiri, kwamba kulikuwa na mawe makubwa halafu kundi likakuvamia toka pande zote, nawe umeishatia mbili tatu kusherehekea mwaka mpya lolote laweza kutokea kutokana na panic unayoipata.

Mimi nimeshuhudia watu wakitumia matukio mbali mbali kufanya uharifu. Siku moja maeneo ya kinondoni niliona kundi la vijana wakishangilia baada ya kushinda mechi ya mpira wa miguu (walikuwa wakikimbia wakiimba) . Lakini walitumia fursa hiyo kupora vitu mbali mbali toka kwa akina mama na watoto hasa. Kuna mtoto mmoja mdogo alikuwa anacheza na ki-baiskeli kidogo barazani kwao, aliporwa na kuumizwa sana. Kwani mporaji alishika carrier na kubinua kale katoto na yeye kuondoka na mzigo ule, akimwacha mtoto akivuja damu usoni alipodondokea. Je ungekuwa baba wa mtoto huyo na una pistol ungefanyaje?

Polisi walizuia mambo hayo wakati wa mwaka mpyana wazazi walisikia, je kwa nini hawakuwazuia watoto hao, yote ni majuto ambayo ni mjukuu. Tutumie tukio hili kujifunza

Nyati,
Duma Hill, Mikumi
 
Umejuaje sijawahi kujikuta kwenye mazingira kama hayo! Back to the topic... hicho unachohimiza kuhusu kubadilika hata mimi nakuunga mkono.... lakini si ''kuwafunza watanzania kwa kuwaua kwa risasi''. Itumike njia nyingine!

Ni rahisi sana kunyooshea vidole wengine mpaka siku umehikuta katika hali ya kuogofya. Kwa sasa endeleeni na lectures zenu za "ningekuwa mimi"
 
Kwanza nawapa pole wafiwa wote kwa janga hili.

Tukirudi kwenye tukio nafikiri jeshi linatakiwa kumchukulia hatua mwanajeshi yeyote anayeshiriki ktk matukio kama haya labda ndiyo maana wanakuja na utetezi ni kwa nini hawakuchukua hatua hizo kama kumweka quarter guard (kumfunga katika mahabusu ya wanajeshi). Kumbuka hawa wana polisi wao wakijulikana kwa mavazi yao ya MP (Military Police).

Mimi siwezi kuhukumu hapa kwani sikuwepo na habari zinatofautiana has juu ya nini kilijiri, kwamba kulikuwa na mawe makubwa halafu kundi likakuvamia toka pande zote, nawe umeishatia mbili tatu kusherehekea mwaka mpya lolote laweza kutokea kutokana na panic unayoipata.

Mimi nimeshuhudia watu wakitumia matukio mbali mbali kufanya uharifu. Siku moja maeneo ya kinondoni niliona kundi la vijana wakishangilia baada ya kushinda mechi ya mpira wa miguu (walikuwa wakikimbia wakiimba) . Lakini walitumia fursa hiyo kupora vitu mbali mbali toka kwa akina mama na watoto hasa. Kuna mtoto mmoja mdogo alikuwa anacheza na ki-baiskeli kidogo barazani kwao, aliporwa na kuumizwa sana. Kwani mporaji alishika carrier na kubinua kale katoto na yeye kuondoka na mzigo ule, akimwacha mtoto akivuja damu usoni alipodondokea. Je ungekuwa baba wa mtoto huyo na una pistol ungefanyaje?

Polisi walizuia mambo hayo wakati wa mwaka mpyana wazazi walisikia, je kwa nini hawakuwazuia watoto hao, yote ni majuto ambayo ni mjukuu. Tutumie tukio hili kujifunza

Nyati,
Duma Hill, Mikumi

Hiyo siyo excuse ya kuua comrade tuache sheria ishike mkondo wake. Serikali haikusema watu wasisherehekee mwaka mpya bali ilisema washerehekee kiustaarabu, sasa hatujui hawa walisherehekkea vipi, tunatumia viashiria kufikia conclusion, kwamba wangekuwa na mawe wangepiga gari lakini gari halikupigwa polisi wamesema kwenye media siku ya pili yake kuwa gari ya huyo jamaa haijaharibika popote. Na yeye akasema hajui ilikuwaje akafyatua risasi hata kama angekuwa na kitengo kikubwa bado si makini
 
Back
Top Bottom