Eric Shigongo: Ukisoma Ripoti za Uchumi wetu ni nzuri sana lakini Wananchi hawana fedha mfukoni

Eric Shigongo: Ukisoma Ripoti za Uchumi wetu ni nzuri sana lakini Wananchi hawana fedha mfukoni

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Eric Shigongo, ametoa kauli yenye msisitizo mkubwa kuhusu hali halisi ya uchumi wa Tanzania, akiongea bungeni jijini Dodoma. Akizungumza katika kikao na wanahabari, Mbunge Shigongo amesema kuwa licha ya rekodi rasmi kuonyesha kuwa uchumi wa nchi unaendelea kukua, wananchi wengi bado wanakabiliwa na changamoto kubwa za kipato.

“Rekodi zinaonyesha ukuaji wa uchumi, lakini katika maisha halisi, wananchi wengi hawana fedha za kutosha. Vipato vyao ni vidogo sana, jambo linalowafanya kushindwa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi,” amesema Mbunge Shigongo.

Mbunge huyo ameweka wazi kuwa tatizo la ukosefu wa fedha mkononi kwa wananchi ni la kimsingi na linahitaji suluhisho la haraka. Amesisitiza kuwa Watanzania wanahitaji fursa za kiuchumi ambazo zitawawezesha kuzalisha mapato yao wenyewe badala ya kutegemea misaada au mishahara midogo.

“Serikali lazima itengeze fursa zinazowawezesha wananchi kupata fedha kwa njia endelevu. Hii ni muhimu kwa ajili ya kuwaondolea umaskini na kuhakikisha kuwa ukuaji wa uchumi unaonekana kwa kila mwananchi, siyo tu kwa takwimu,” aliongeza Mbunge Shigongo.

Kauli hii inajitokeza wakati ambapo baadhi ya wananchi wanashikilia kuwa ukuaji wa uchumi wa Tanzania hauonekani katika maisha yao ya kila siku, huku gharama za maisha zikiwa juu na fursa za ajira na biashara za kipato zinaonekana kuwa chache katika baadhi ya maeneo.
 
Hivi hawa mazafakas huwa hawawezi kuchangia bila kuimba mapambio ya praise and worship?

Mtu anasema hali ya kifedha ya wananchi ni mbaya, lakini bado anamsifia fazafaka ambaye yuko nyuma ya hiyo hali mbaya! Upumbavu gani huo?
 
Back
Top Bottom