Chimunguru
JF-Expert Member
- May 3, 2009
- 10,678
- 4,377
Mkono wa mara sec baada ya miezi mitatu pale shule walinzi wa shule walikuwa wawili wote wakaugua, uongozi wa shule ukaamua kuwe na zamu ya kulinda ki mabweni pale shuleni. barabarani kabisa kulikuwa na dukacla ushirika na canteen baada ya hapo kuna ofisi za walimu na madarasa pembeni yake kuna mess hafu unapita mabweni ya wasichana mwishoni ndo wanaume. zamu yetu ilipofika bweni la uhuru mgao wa sukari ukawa umeisha so no tea usiku wachizi tukapiga akili tukagundua miezi hiyo mahindi na mihogo ndo imekomaa na mashamba yenyewe ni ya walim, na mwenyekiti wa shule tupo nae bweni moja na yeye ndo anatuchorea ramani ya shamba la mwl gani limemea zaidi tukizama tukiibuka tuna furushi la mahindi mabichi na mihogo tunachemsha usiku ni full kujiachia ikifika saa kumi wanafunzi wengine wanawahi kuamka kuja kukusanya kilichobaki. hatukuwahi kamatwa.