England kuingilia utendaji wa timu ya Chelsea sio kosa kwa kanuni za FIFA?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,331
12,647
Wajuzi tuambieni kwanini shughuli za mchezo wa mpira England umeingiliwa na wanasiasa kutokana na vita ya Russia na Ukraine?
 
Ndio mjue hii dunia mabeberu ndio wana power, wanafanya wanavyojisikia, unachokisikia na kukiona wewe kwenye media ni wao wametaka wewe uone na kwa lengo lao.

Watu wameuwawa sehemi tofauti tofauti, dunia kwa % ikawa kimya, kwa ukraine watu wanashupaza shingo(siungi mkono nchi kuvamiwa wala mauwaji yoyote)

Fifa walikataza siasa kwenye michezo, ila wao sasa ndio wamekuwa kimbembele front katika hili..
Hilo linalofanyika pale lina baraka zote za FIFA, ukijiuliza chelsea inahusika vipi mpaka inyanyasike hivi hata huelewi.
 
England imemuwekea vikwazo Roman pamoja na mali zake na Chelsea ni mali yake. Kwa kifupi tu England haijachanganya siasa na mpira ndiyo maana pamoja na kufungiwa mmiliki wao wamepewa special license kuendelea kufanya kazi.
maajabu makubwa, huko sio kuingilia mambo ya mpira? huoni hata afya za wachezaji zitayumba kwa timu yao kuyumba? mpaka wachezaji wenye asili ya Urusi wananyanyaswa kama vile na wao ni sehemu ya urais wa Urusi. Hii sio sawa aloo, double standard
 
Safari hii FIFA wameruka sarakasi 🤸 huku wakiwa wamevaa taulo.
Chelsea imevurugwa sana na wanasiasa katikati ya msimu bila kosa lolote la kimpira kwa mmiliki, uongozi, benchi la ufundi wala wachezaji. Abramovich hakuna ushahidi kama yeye ndiye ameamuru uvamizi wala kugharamia vita, ni vipi FIFA ikae kimya kwenye hili?
 
Back
Top Bottom