Elimu ya Josephat Gwajima inatia mashaka

Elimu ya Josephat Gwajima inatia mashaka

Sifa za kuwa mbunge ya chini awe darasa la Saba ndio maana Tunduma mgombea ubunge wa Chadema Tunduma ambaye pia alikuwa mbunge wa chadema Jimbo Hilo ni darasa la Saba pure anaitwa Mwakanjoka
bila kumsahau yule mbunge wa CCM👹👹👾wa kandaile yakupenda madem weupe anaitwa MSUKUMA cjui yule hata ilo dalasa7 kwake nindoto
 
Sifa za kuwa mbunge ya chini awe darasa la Saba ndio maana Tunduma mgombea ubunge wa Chadema Tunduma ambaye pia alikuwa mbunge wa chadema Jimbo Hilo ni darasa la Saba pure anaitwa Mwakanjoka
Hahaha hivi uki fail form six ukapata zero unakuwa na elimu gani?! A-level au O-level?!

Gwajima O-level ali fail alipata daraja la nne lililo egemea zero, leo ana PhD.
CCM akili zenu mnazijua wenyewe.

Eti kasema anajua kaongea kijapani na kaandika vitabu vya kijapani, mara katuambia anatuletea Ambulance, !!!

Kampeni za hivyo angeenda Koromije.
Kawe Ambulance za nini tuna magari yetu, halafu sisi sio wagonjwa, au anagombea uganga wa zahanati?!
 
Vyuo vya dini vingi haviko Accredited na serikali sababu ya separation Kati ya dini na serikali .Hivyo sifa za kujiunga ziko tofauti na Hivyo vyuo accredited vya serikali.Sababu serikali hazina dini nyingi Huwezi mpelekea mtu asiye na dini akutengenezee syllabus ya dini hivyo vyuo vingi vya dini vigezo huwa tofauti kabisa

Ndio Maana waweza mkuta shehe ana PhD ya elimu ya kiislamu lakini alisoma madrasa tu hajawahi kanyaga hata shule ya msingi lakini kasoma madrasa na vyuo vya kiislamu Hadi kufikia ngazi ya PhD

Kwenye makanisa mengine mfano darasa la Saba aweza Soma vyuo vyao.Diploma na degee bila shida wao elimu wanayojikita nayo Ni ya dini Yao tu Sio mlundikano wa masomo mengi la hasha wanatengeneza msomi w dini Yao tu

Kuhusu PhD ya Gwajima hiyo alipewa na hicho chuo.kutokana na kazi yake anayofanya kwenye jamii walifanya assessment wakaona ni mtu kafanya kazi kubwa kwenye jamii kaandika vitabu 32 na vimetafsiriwa kwa lugha za ya 20 duniani na vinadomwa nchi tofauti za lugha tofauti na kutumia vyuoni vya dini ndio wakamtunuku hiyo PhD

Hiyo PhD hicho chuo waliotunukiwa nacho Ni pamoja na marehemu Dk Reginald Mengi yeye PhD yake Ni ya hicho chuo naye alitunukiwa kwa kazi yake kwenye jamii mwingine Ni Marehemu Dk Getrude Rwakatare pia PhD yake alipewa na hicho chuo
Japo umejitahidi kutaka kueleza kitu lakini ukweli ni kuwa umepotoka kabisa.

Shule za dini zina uwezo wa kutengeneza syllabus zao lakini unapofika kwenye Universities, haijalishi chuo hicho kinamilikiwa na dini au Serikali, ili kuweza kutambulika na kukubaliwa, katika kila nchi kuna board ya kuweka vigezo vya kukifanya chuo kutoa degree inayotambulika, na hizi board hufuata miongozi ya kimataifa ya elimu. Bodi hizi ndiyo hutoa ulinganifu wa credits za viwango vya elimu kwa mataifa mbalimbali.

Vyuo vikuu, bila ya kujali kama ni cha dini, serikali au taasisi binafsi, huwa ni taasisi huru ya kimasomo. Ndiyo maana leo hii ukitaka kwenda kusoma degree ya theology au divinity Kent University, UK, unapokelewa kwa kuangalia kiwango chako cha elimu na siyo dini yako. Hata kama huna dini yoyote utapokelewa kama kiwango chako cha elimu kimefikia entry qualifications.

Kwa kuangalia hiyo elimu ya Gwajima, kwa kweli huo ni utapeli mkubwa wa elimu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sifa za kuwa mbunge ya chini awe darasa la Saba ndio maana Tunduma mgombea ubunge wa Chadema Tunduma ambaye pia alikuwa mbunge wa chadema Jimbo Hilo ni darasa la Saba pure anaitwa Mwakanjoka
Hujaelewa hata kianachojadiliwa. Tuliza akili, uelewe hoja iliyopo badala kukurupuka kuandika kabla hata ya kuelewa hoja ni nini.

Tatizo la Gwajima siyo kiwango cha Elimu bali uwongo katika utoaji wa taarifa ya elimu yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Japo umejitahidi kutaka kueleza kitu lakini ukweli ni kuwa umepotoka kabisa.

Shule za dini zina uwezo wa kutengeneza syllabus zao lakini unapofika kwenye Universities, haijalishi chuo hicho kinamilikiwa na dini au Serikali, ili kuweza kutambulika na kukubaliwa, katika kila nchi kuna board ya kuweka vigezo vya kukifanya chuo kutoa degree inayotambulika, na hizi board hufuata miongozi ya kimataifa ya elimu. Bodi hizi ndiyo hutoa ulinganifu wa credits za viwango vya elimu kwa mataifa mbalimbali.

Vyuo vikuu, bila ya kujali kama ni cha dini, serikali au taasisi binafsi, huwa ni taasisi huru ya kimasomo. Ndiyo maana leo hii ukitaka kwenda kusoma degree ya theology au divinity Kent University, UK, unapokelewa kwa kuangalia kiwango chako cha elimu na siyo dini yako. Hata kama huna dini yoyote utapokelewa kama kiwango chako cha elimu kimefikia entry qualifications.

Kwa kuangalia hiyo elimu ya Gwajima, kwa kweli huo ni utapeli mkubwa wa elimu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Asante kwa kutoa hilo darasa. Nilishindwa mjibu huyu mtu sababu niliona ana uelewa duni kwenye mambo haya. Kuhusu Gwajima, mimi nilikuwa napata shida sana kwani elimu yake na matamshi yake niliona haviendani. Nilidhani ni msomi. Sasa, nimejua ukweli hivyo nimekuwa huru na simlaumu tena atakapo sema lolote.
Nimebaki na shida moja tu, nayo ni elimu ya Jiwe. Uelewa wake hauendani na elimu yake.
 
Hii elimu ya Gwajima ni utapeli mkubwa. Sasa nimeelewa kwa nini amekuwa mtu wa kuropoka ovyo ovyo. Mara anafufua misukule, mara nitanunua treni, mara nitawapeleka wakazi wote wa Jimbo la Kawe Marekani - haya siyo maneno yanayoweza kutamkwa na mtu aliyeelimika au hata mwenye akili timamu yeyote, bila ya kujali huyo mtu ana elimu gani.

Ameshindwa kuwapeleka waaumini wake Marekani, halafu eti atawapeleka wajazi wote Marekani. Unawapeleka Marekani kufanya nini! Eti ana rafiki ambaye ni gavana, na anataka wabadilishane watu. Huyu ni mzima kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Separation ya serikali na dini kwenye elimu ndiko ni ndiko naongelea.Kwenye kugombea uongozi katiba ya Nchi inaruhurusu Kila mtu kugombea bila kubagua.Ha i separate

Anatumia Haki yake ya kikatiba.Hakuna popote katiba inatamka kuwa mgombea ubunge anatakiwa kuacha kazi yake ya kidini au ya private sector Ni serikalini tu
Kinachojadiliwa siyo haki ya kikatiba, ni uongo na sifa za bandia. Kumbuka mambo hayo yanaweza kuwa ni mwongozo wa tabia yake. Mbona Musukuma anajitambulisha kwa class 7 yake?
 
Sifa za kuwa mbunge ya chini awe darasa la Saba ndio maana Tunduma mgombea ubunge wa Chadema Tunduma ambaye pia alikuwa mbunge wa chadema Jimbo Hilo ni darasa la Saba pure anaitwa Mwakanjoka

wewe mbunge darasa la saba ni CCM (msukuma )
 
Tulieni octoba 28 kitaeleweka,mtafutueni kazi mbadala huyu mgombea wenu mdee
 
Hahaha hivi uki fail form six ukapata zero unakuwa na eliu gani?! A-level au O-level?!

Gwajima O-level ali fail alipata daraja la nne lililo egemea zero, leo ana PhD.
CCM akili zenu mnazijua wenyewe.

Eti kasema anajua kaongea kijapani na kaandika vitabu vya kijapani, mara katuambia anatuletea Ambulance, !!!

Kampeni za hivyo angeenda Koromije.
Kawe Ambulance za nini tuna magari yetu, halafu sisi sio wagonjwa, au anagombea uganga wa zahanati?!
Duh....!

Kawe wote mna magari?!
 
pia kupeleka watu marekani
Mkuu hakusema atapeleka watu tu marekani; amesema atapeleka watu "wote" wa Kawe marekani, na atabadilishana na wale watu wa kule marekani ili wao waje Kawe...Kawe yote itakuwa ni miondoko ya watsap niiiga yoyo yoyo, yu no waram seeeing
 
Hii elimu ya Gwajima ni utapeli mkubwa. Sasa nimeelewa kwa nini amekuwa mtu wa kuropoka ovyo ovyo. Mara anafufua misukule, mara nitanunua treni, mara nitawapeleka wakazi wote wa Jimbo la Kawe Marekani - haya siyo maneno yanayoweza kutamkwa na mtu aliyeelimika au hata mwenye akili timamu yeyote, bila ya kujali huyo mtu ana elimu gani.

Ameshindwa kuwapeleka waaumini wake Marekani, halafu eti atawapeleka wajazi wote Marekani. Unawapeleka Marekani kufanya nini! Eti ana rafiki ambaye ni gavana, na anataka wabadilishane watu. Huyu ni mzima kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app
Lawama ziko kwa CCM na maamuzi yao. Walishindwa kuelewa maana ya nafasi ya ubunge. Gwajima alistahili kuangaliwa kwa ubora wake na hata waumini wake. Ubora wake uko chini na hata waumini wake ni wa aina hiyo hiyo! Hili ni tatizo kwa vyma vyote lakini kwa CCM ni kubwa kutokana na ukongwe wao. Ndo maana Bunge linageuka kuwa ni kikao cha watu wabovu na rais anaamua kujipangia matumizi yeye mwenyewe.

Ni kweli haikuwa ajabu mtu anayejiita askofu kujipiga picha akifanya ngono? Bila kujali sababu ya kitendo hicho, hakutakiwa hata kusikilizwa kwenye kura za maoni. Ni mtu mchafu tu! Tamaa ya CCM ni ile ile; kuwa na wabunge wengi bila kujali ubora wao.
 
Nimekuwa napata shida sana kutokana na elimu ya Gwajima . Tokea kipindi akitangazia umma na akiliamsha dude pale Kanisani kwake, basi ,nikawa napata shida kutokana na matamshi yake.

Kila kazi ina miiko yake. Askofu hatakiwi kutoa siri za muumini wake hata kama huyo muumini amelihama kanisa lake. Hapa niliona kwenye YouTube Gwajima akisema mambo ya siri ya mke wa Dkt. Slaa.

Leo nimeangalia tovuti ya kanisa la Gwajima. Katika hii tovuti ambayo ameandaa yeye mwenyewe nimeona mambo yafuatayo:
  • Gwajima amezaliwa mwaka 1970
  • Amemaliza shule ya msingi mwaka 1985
  • Amemaliza shule ya sekondari Olevel mwaka 1993. Alichelewa kumaliza secondary sababu ya maradhi.
  • Alimaliza Advanced Diploma in Bible and Theology mwaka 1994 mjini Nairobi Kenya. Hapa ndo pana ufisadi wa elimu. Yaani alisoma stashahada ya juu kwa mwaka mmoja tena baada ya kumaliza olevel. Kwa maoni yangu, huyu alichosoma ni level ya certificate. Matatizo ya Gwajima it yanaanzia hapa.
  • Baada ya hiyo Advanced Diploma yake ambayo ni magumashi, alijiunga na chuo kinaiitwa Japan Bible Institute na kusomea Master’s degree in Christian Missions June 2006 mpaka February 2008. Hapa nilitaka kujua ni kwanini hiyo institute ilikubali kumpa admission mwanafunzi ambaye ambaye ana only post secondary study ya mwaka mmoja tu, nikakuta hiyo institute yenyewe nayo ni ya kimagumashi. Hiyo institute haina hata physical address . Ni Chuo cha kwenye mtandao na pia kinatoa degree by experience. Yaani waweza pewa hata degree kwa kuwa una uzoefu. Hii masters degree yake kumbe ni utata mtupu na achilia mbali kwamba hana sifa za kujoin hata kozi ya degree ya kwanza.
  • Mwaka 2015 alipewa PhD na chuo cha kidini cha Afrika ya Kusini kinaitwa Omega Global University. Kwenye tovuti ya chuo hiki pana maelezo kwamba kinatoa honorary PhD. Gwajima haoneshi kwenye tovuti yake ni mwaka gani alijoin hiki chuo wala lini alimaliza. Pia, hiyo miaka, Gwajima alishakuwa na kanisa la misukule huko Ubungo na baadae kuhahmia Kawe. Tena ni mwaka ambao alikuwa mshenga wa kumleta Lowassa Chadema na baadaye kututobolea siri ya vyeti vya mkuu wa mkoa aitwaye Bashite. Hivyo basi, PhD hii ni ya heshima.
  • Mwisho, kwa maoni yangu, elimu ya Gwajima ambayo haina mashaka kabisa ni ile ya form four mwaka 1993.
References
Mwamposa alipewa PhD baada ya kuua watu kule Moshi ndio hiyo hiyo ya akina gwaji.
 
"...Separation ya dini na serikali..." na sasa mtu huyo huyo anaingia serikalini huku akiwa bado kiongozi kwenye mambo ya kidini.
Usisahau kuteuliwa kugombea ubunge, kigezo kikubwa ni kujua kusoma na kuandika tu... huko mbele kama mtu ana elimu ya majini, katekisimu etc kwao si ishu... cha kuniuliza, JE! ANAJUA KUSOMA NA KUANDIKA..!?
 
Back
Top Bottom