Kutoka kwenye page ya fb ya Azam TV wameandika hivi kama inavyosomeka hapa chini, kumbe kuongeza sate sio kosa wanajamvi wenye utaalam na hii elimu ya Sate endeleeni na moyo huo huo wa kushare mlichonacho.-- Ph-25
""Wadau,
Tunawaletea software mpya kwenye visimbuzi vyenu vya Azam TV, makubwa utakayopata ni kama ifuatavyo;
Ongezeko la listi za chaneli;
(Haimaanishi tumeongeza chanel mpya,la hasha ila tumebadilisha mpangilio wa chaneli)
Hapo utaona kuna list kadhaa utakazopata kwa kubonyeza OK na kisha kubonyeza kitufe cha mshale wa kushoto au kulia ili kwenda kwenye chaneli mbalimbali.
List ya kwanza itakuwa na chaneli za package ya Azam,
na ya pili ni (Other TV Channels) itakupatia list ya chaneli nyinginezo ulizoweka kwenye kisimbuzi chako.
Kwa hiyo basi, ukiongeza satellite mpya na kuweka frequency zake kwenye kisimbuzi chako, chaneli zake zitakuwa kwenye list ya pili ya Other TV Channels.
Kupangilia chaneli kwenye mpangilio unaotaka wewe.
Sasa mdau utaweza kubadilisha nafasi ya chaneli unazozipenda(Favourite) kwenye list kama unavyotaka wewe. Hii itakupa nafasi ya kuweka mwanzo zile chaneli unazozipenda na kuziangalia kwa wingi kuliko nyingine kuliko kuanza kuitafuta kwa kubonyeza mshale wa kushusha.
Kama unapenda chaneli yoyote ianze juu kabisa kwenye list yako, nenda kwenye menu ubadilishe mpangilio wa chaneli zako kutokana na maelezo yatakayowiana na remoti yako ufatishe maelekezo kwa kutumia rimoti yako.
Uwezo wa kuweka au kuondoa subtitle kwenye chaneli.
Sasa unaweza kuondoa au kuongeza subtitle(Tafsiri) kwenye chaneli ambazo zina subtitle.
(Tafadhali kumbuka, kuna baadhi ya chaneli tayari zina substitle zimewekwa ambazo hazitaweza kutolewa.)Chaneli ya Colors imetengwa subtitle kwa maana unaweza kuangalia na subtitle ama laa.
Ongezeko la format za video zinazoweza kuchezwa kwenye kisimbuzi. Sasa unaweza kuweka USB flash yako na kuona filamu zilizo kwenye format mbalimbali.
Chakufanya:
Kama unaangalia Azam TV, Zima kisha washa, utapokea ujumbe,bonyeza ok.mwanzo itakuambia failed,usijali,itaendelea yenyewe ndani ya sekunde hiyo hiyo,iache iji update mpaka imalize,itachukua muda wa mpaka Dakika 5,ila inaweza kuwa chini ya hapo.
Kama Azam TV yako imezimwa,ukiwasha itakupa utaratibu huo huo, Tafadhali usizime Dekoda yako wakati zoezi hilo linaendelea,unaweza kuzima ikimaliza ku update.
Hii ni katika kuhakikisha tunawaletea ubora zaidi kila kukicha.
Usisite kuuliza pale popote utakapokwama, Tuko kwa ajili yako.
Azam TV Burudani kwa wote