Elimu ni cheti au ni ujuzi?

Elimu ni cheti au ni ujuzi?

Logic: Elimu ni ujuzi , cheti ni nyaraka ya kisheria kuthibitisha elimu = cheti ni nyaraka ya kisheria kuthibitisha ujuzi. Kwa hiyo, mwenye elimu lazima awe na ujuzi; kama hana ujuzi atakuwa hana elimu. Hapo nipo sahihi?
Ndio maana nikasema ni cheti cha kuthibitisha elimu kwenye mabano nikasema lakini sio ujuzi kwakuwa watu wanaweza kununua cheti cha elimu lakini sio ujuzi
 
Elimu ni ujuzi, cheti ni kama uthibitisho wa kinadharia kuwa tuna assume unao ujuzi hivyo ngoja upewe nafasi tuone kuwa kweli ujuzi upo?....Twende kibongo bongo sasa, bongo Elimu ni cheti Kwa asilimia kubwa, ndio maana kama huna cheti hupewi nafasi uoneshe ulichonacho maybe upitie chocho Kwa chocho ujikomboe mwenyewe bila kushikwa mkono na govt.

Hapa mm nimeongelea ujuzi wa kutatua changamoto Tu na siyo ujuzi kama wa mawasiliano na vinavyofanana na hivyo .
 
Elimu ni ujuzi, cheti ni kama uthibitisho wa kinadharia kuwa tuna assume unao ujuzi hivyo ngoja upewe nafasi tuone kuwa kweli ujuzi upo?....Twende kibongo bongo sasa, bongo Elimu ni cheti Kwa asilimia kubwa, ndio maana kama huna cheti hupewi nafasi uoneshe ulichonacho maybe upitie chocho Kwa chocho ujikomboe mwenyewe bila kushikwa mkono na govt.

Hapa mm nimeongelea ujuzi wa kutatua changamoto Tu na siyo ujuzi kama wa mawasiliano na vinavyofanana na hivyo .
Kama changamoto hazitatuliwi inatafsiri, hakuna ujuzi?
 
Hapa nilipo nina vyeti vingi kweli, vinakaribia kujaa begi, lakini sina uwezo wa kuvumbua chochote kile kwa kutumia elimu niliyoipata kutokea chekechea mpaka uprofeseri. Nazidiwa ata na mafundi majiko walioishia darasa la saba, wanaweza kutengeneza kitu. Yaani nisipo ajiriwa na huu wingi wa vyeti nilivyonavyo, sitaweza kuishi kabisa. Sasa najiuliza swali, elimu ni kupata ujuzi au ni kupata cheti tu? Kwa sababu, ata huku mashuleni na vyuoni tunajifunza namna ya kujibu maswali tu, na tunafaulu vizuri kwa alama A; ila kiuhalisia hatuvumbui vitu, tunategemea kuajiriwa tu.​
Kwa huku kwa kina makonda ni cheti hata kama hujui chochote kilichopo kwenye chati chako
 
Hapa nilipo nina vyeti vingi kweli, vinakaribia kujaa begi, lakini sina uwezo wa kuvumbua chochote kile kwa kutumia elimu niliyoipata kutokea chekechea mpaka uprofeseri. Nazidiwa ata na mafundi majiko walioishia darasa la saba, wanaweza kutengeneza kitu. Yaani nisipo ajiriwa na huu wingi wa vyeti nilivyonavyo, sitaweza kuishi kabisa. Sasa najiuliza swali, elimu ni kupata ujuzi au ni kupata cheti tu? Kwa sababu, ata huku mashuleni na vyuoni tunajifunza namna ya kujibu maswali tu, na tunafaulu vizuri kwa alama A; ila kiuhalisia hatuvumbui vitu, tunategemea kuajiriwa tu.​
Ulisomea vitu gani hasa mkuu
 
Cheti ni kwa ajili ya kuajiriwa tu. Unaweza kuwa na ujuzi bila cheti hautaajiriwa. Ni rahisi kupata ujuzi kuliko kupata cheti. Ujuzi unaupata hata ukiwa mitaani kwa kuiga wenye ujuzi waliousomea shuleni/chuoni
 
Kuna watu ni wajuzi wa fani na taaluma mbalimbali za kimaisha ila hawana cheti, hawaajiriwi ingawa waajiri wanawatamani sana kuwapata ila mifumo ya ajira haiwatambui
 
Cheti ni kwa ajili ya kuajiriwa tu. Unaweza kuwa na ujuzi bila cheti hautaajiriwa. Ni rahisi kupata ujuzi kuliko kupata cheti. Ujuzi unaupata hata ukiwa mitaani kwa kuiga wenye ujuzi waliousomea shuleni/chuoni
Kwa mtazamo huu, ni sawa na kusema tunaenda shule ili tupate vyeti na si kupata ujuzi ili tuajiriwe?
 
Kuna watu ni wajuzi wa fani na taaluma mbalimbali za kimaisha ila hawana cheti, hawaajiriwi ingawa waajiri wanawatamani sana kuwapata ila mifumo ya ajira haiwatambui
Je, na sekta binafsi inaangalia ujuzi au vyeti?
 
Kuna watu wamefika mpaka vyuoni kusomea fani na taaluma fulani wakaishia kutokutunikiwa cheti. Watu hawa wakirudi mitaani tayari wana ujuzi na maarifa ila hawakupata cheti huko chuoni kutokana na sababu mbalimbali. Basi hubaki na maarifa na ujuzi wao bila kutumika sehemu mahsusi. Angalau fani kama za ufundi, biashara na kilimo/ufugaji hizo mtu huweza kujiajiri mwenyewe na akatumia maarifa/ujuzi alioupata chuoni hata bila kupata cheti
 
Kuna watu wamefika mpaka vyuoni kusomea fani na taaluma fulani wakaishia kutokutunikiwa cheti. Watu hawa wakirudi mitaani tayari wana ujuzi na maarifa ila hawakupata cheti huko chuoni kutokana na sababu mbalimbali. Basi hubaki na maarifa na ujuzi wao bila kutumika sehemu mahsusi. Angalau fani kama za ufundi, biashara na kilimo/ufugaji hizo mtu huweza kujiajiri mwenyewe na akatumia maarifa/ujuzi alioupata chuoni hata bila kupata cheti
Kwa hiyo nikitumia njia za mkato nikapata cheti, nitakuwa tayari nina elimu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom