Elimu bure maigizo, Sekondari ya Maendeleo inawachangisha wazazi

Coloneli

Member
Aug 24, 2020
35
151
Salaam wakuu.

Kuna wimbo mmoja unaimbwa sana juu ya elimu bure katika utawala wa awamu ya tano wa Magufuli. Kama ni kweli elimu hiyo inatolewa bure, basi kuna watumishi wanamuhujumu. Shule ya Sekondari Maendeleo, iliyopo Kata ya Wazo wilaya ya Kinondoni inawatoza wazazi na kuwazuia wanafunzi ambao wazazi wao hawajalipa kuingia darasani.

Walimu wanatumia kigezo cha kutaka matokeo mazuri ya mitihani ya kidato cha pili na nne kwa kuwachangisha fedha hizo kwa kisingizio ya mitihani ya majaribio.

Pia wazazi wametakiwa kutoa shilingi elfu kumi kila mmoja ili shule inunue printa. Sasa cha kujiuliza, kama elimu bure imekuwa mzigo kwa Serikali, kwa nini haisemi hadharani watu tujue? Na hii ni shule iliyopo Dar, sijui zile za pembezoni hali ikoje, hii elimu bure ni kiinimacho na kutaka sifa kwa hii Serikali?
 
Acha wachangie, ili watoto wao wasome vizuri. Bila shaka wamekubaliana kwenye vikao vya wazazi. Angalia wanaosoma bure na wanaolipia nani wanafaulu sana?
 
Acha wachangie, ili watoto wao wasome vizuri.....bila shaka wamekubaliana kwenye vikao vya wazazi.......angalia wanaosoma bure na wanaolipia nani wanafaulu sana?
Kama lengo ni kuwafaulisha na then mnawazuia kuingia shule kwa sababu hawajatoa PESA si inakuwa ni ujinga.Nilifikiri kwamba wana akili.Huyo Mkuu wa shule anapaswa kutumbuliwa iwapo kweli anawarudisha wanafunzi nyumbani kwa sababu ya TZS 10,000.IDIOT.Kwa kawaida utaratibu ni mzazi anaitwa shule na sio mwanafunzi anarudishwa nyumbani.Sijui hii desturi imekaaje
 
Mkuu watanzania tu wajinga kwenye mikutano ya kampeni hatuulizi hizi hoja ila tunaambiwa TUMETEKELEZA na watu wanashangilia kana kwamba hajui maana ya elimu bure jambo la muhimu ni kuwaambia watanzania wote tupo kwenye hatua za UBEPARI ujamaa hauna nafasi .
 
Kwa hiyo arudishwe nyumbani mzazi ambaye hasomi?Mtoto anarudishwa nyumbani ili akamshinikize mzazi kutoa pesa kumbuka elimu bure haijakataza wazazi kuchangia maendeleo ya shule zetu.

Vikao halali vinafanyika kati ya shule na wazazi na wanakubaliana kuchangia mwisho wa siku wazazi wanashindwa kutekeleza wajibu wao.Pia kumbuka elimu bure ni mzigo mzito kwa shule zetu kwani haziwezi kujiendesha ipasavyo kwa kutegemea pesa ya serikali peke yake.
 
Ila hiyo elf 10 kwa printa wangeita wazazi pia wavidato vingine hiyo elf 10 ingepungua maana haitumiwi tu na kidato cha 2&4
 
Mkuu kwa uelewa wangu mdogo kila shule ina kamati ya shule ambayo ina jumuisha jopo la walimu na wazazi wa wanafunzi hapo shuleni. Hivyo basi sitaki kuamini wanafunzi wana changishwa hela kwa jili ya kuwa saidia wao kujianda na mitihani ya mwisho bila swala hilo kushirikisha wazazi.

Tatizo liko wapi? Tatizo naliona kuwa wazazi wengi wanapo itwa kwenda mashuleni kwenye vikao vya shule huwa wanajidai havina maana au kusema wapo busy na maisha matokeo yake wanao fika wa chache wana kwenda pitisha hizi agenda nyie mwanafunzi ana rudishwa huku mnalalamika wakati vikao hamuendi.

Kingine swala zima la bure jamani tuweni serious kuna michango mingine midgo mno elfu kumi ni hela ya kujikaza tu umpe mwanao aka lipie afanye majarbio hembu jiulize asipo fanya au unapo bisha bisha mwalimu ana kata tamaa jiulize mwanao anapo feli ni garama ngapi unakuja kuingia? ni shingi nagapi unatumia kwenye mabaa na starehe?

Tusisahau cha bure kina umiza siku zote. Sometime hizo garama kidogo unazo takiwa kuingia elewa au saidia wanao pata changamoto kutwa kupambana na hawa watoto siku hizi wana kwenda shule na smartphone ni walimu. so tunapo shindwa kuwapa hata za kubrush viatu nao wana kosa motisha.
 
Acha wachangie, ili watoto wao wasome vizuri.....bila shaka wamekubaliana kwenye vikao vya wazazi
Kama lengo ni kuwafaulisha na then mnawazuia kuingia shule kwa sababu hawajatoa PESA si inakuwa ni ujinga.Nilifikiri kwamba wana akili.Huyo Mkuu wa shule anapaswa kutumbuliwa iwapo kweli anawarudisha wanafunzi nyumbani kwa sababu ya TZS 10,000.IDIOT.Kwa kawaida utaratibu ni mzazi anaitwa shule na sio mwanafunzi anarudishwa nyumbani.Sijui hii desturi imekaaje
Unafhani headmaster pekee ndiye kaamua? Kama unamtoto hapo, vikao vya wazazi huwa unaenda? Duniani hapa hakuna cha bure tusidanganyane ukitaka kitu bora lazima ugharamie.....endeleeni kucheka na wanasiasa, watoto wao wenyewe hawasomi humo,elf 10 tu makelele kibao
 
Dar kuna wazazi waswahili sana . Acha wasurubiwe tu
Kama lengo ni kuwafaulisha na then mnawazuia kuingia shule kwa sababu hawajatoa PESA si inakuwa ni ujinga.Nilifikiri kwamba wana akili.Huyo Mkuu wa shule anapaswa kutumbuliwa iwapo kweli anawarudisha wanafunzi nyumbani kwa sababu ya TZS 10,000.IDIOT.Kwa kawaida utaratibu ni mzazi anaitwa shule na sio mwanafunzi anarudishwa nyumbani.Sijui hii desturi imekaaje
 
Acha wachangie, ili watoto wao wasome vizuri.....bila shaka wamekubaliana kwenye vikao vya wazazi

Unafhani headmaster pekee ndiye kaamua? Kama unamtoto hapo, vikao vya wazazi huwa unaenda? Duniani hapa hakuna cha bure tusidanganyane ukitaka kitu bora lazima ugharamie.....endeleeni kucheka na wanasiasa, watoto wao wenyewe hawasomi humo,elf 10 tu makelele kibao
ndio waache porojo za kisiasa kujilamba kuwa ccm inatoa elimu bure wakati elimu ya kulipia
 
Acha wachangie, ili watoto wao wasome vizuri.....bila shaka wamekubaliana kwenye vikao vya wazazi

Unafhani headmaster pekee ndiye kaamua? Kama unamtoto hapo, vikao vya wazazi huwa unaenda? Duniani hapa hakuna cha bure tusidanganyane ukitaka kitu bora lazima ugharamie.....endeleeni kucheka na wanasiasa, watoto wao wenyewe hawasomi humo,elf 10 tu makelele kibao
Mku swala sio 10k swala ni kumfukuza mwanafunzi shule kisa 10k.Haina maana yoyte.Nafikiri jukumu la kufuatilia ni la mzazi na mwalimu.Mwanafunzi aachwe asome kwa amani.Hutaelewa hili wewe kwa sababu unaweza kuwa unafikiri tofauti na mimi.
 
Salaam wakuu.

Kuna wimbo mmoja unaimbwa sana juu ya elimu bure katika utawala wa awamu ya tano wa Magufuli. Kama ni kweli elimu hiyo inatolewa bure, basi kuna watumishi wanamuhujumu. Shule ya Sekondari Maendeleo, iliyopo Kata ya Wazo wilaya ya Kinondoni inawatoza wazazi na kuwazuia wanafunzi ambao wazazi wao hawajalipa kuingia darasani.

Walimu wanatumia kigezo cha kutaka matokeo mazuri ya mitihani ya kidato cha pili na nne kwa kuwachangisha fedha hizo kwa kisingizio ya mitihani ya majaribio.

Pia wazazi wametakiwa kutoa shilingi elfu kumi kila mmoja ili shule inunue printa. Sasa cha kujiuliza, kama elimu bure imekuwa mzigo kwa Serikali, kwa nini haisemi hadharani watu tujue? Na hii ni shule iliyopo Dar, sijui zile za pembezoni hali ikoje, hii elimu bure ni kiinimacho na kutaka sifa kwa hii Serikali?
Ujinga wa wazazi ndio unafanya mchangishwe mimi kuna shule naijua mkuu wa shule yuko vizuri sana wazazi wanachangia chakula tu hayo mengine ni yaserekali jamaa yangu serekali ilishatoa muongozo kuhusu elimu bure ni kazi yetu wananchi kuifuata au kuicha
 
Mku swala sio 10k swala ni kumfukuza mwanafunzi shule kisa 10k.Haina maana yoyte.Nafikiri jukumu la kufuatilia ni la mzazi na mwalimu.Mwanafunzi aachwe asome kwa amani.Hutaelewa hili wewe kwa sababu unaweza kuwa unafikiri tofauti na mimi.
Kwamtazamo huo nimekuelewa na kumfukuza mtoto si sawa japo ni mbinu ya kumshitua mzazi
 
Mkuu fuatilia wazazi walichokubaliana kwenye kikao halafu lete mrejesho, vinginevyo ruzuku haitoshi, na kill mzazi anataka mtoto afaulu.
Bado Safari ya elimu ni ndefu, akifika advance au chuo lazima kulipa michango zaidi ya elfu kumi.
 
Back
Top Bottom