Eid Vs Pasaka na X-mass

Eid Vs Pasaka na X-mass

Kwa Dar Iddi ni fungulia dog. Bar, hoteli, migahawa, gest wote wanaingiza mkwanja.
 
Unaenda Kagera uwambie leo sikukuu ya Idd watu watakushangaa! Kwa maeneo ya pwani sawa lakini kwinginrko ni big no!
Same to Pasaka, X mass kwa mikoa ya Pwani na kanda ya Kati, KIGOMA, TABORA, DOM, MORO huko Eid huwa na Vibe kutokana na Majority ya Waislam. Na karibu majiji Yote isipokuwa MBEYA.
Mikoa ambayo EID haina VIBE ni MBEYA, IRINGA, RUVUMA, NJOMBE, SHINYANGA, MARA na RUKWA.
 
Eid Mubarrak wana Jf,

licha ya utofauti wa kiimani baina ya islam na christian ila Watanzania tumekua ni watu wamoja. Na tumeunganishwa na utanzania wetu. Sikuu ya kiislam huwa ni sikukuu ya taifa zima na ya kikristo pia vivyo hivo, jambo la kumshukuru sana mungu.

Kwa upande wako sikukuu ipi huwa inabamba zaidi kati ya Eid, pasaka na xmass.

Kwa upande wangu mimi huwa inaanza Eid hii ya ramadhani Then Xmass. Na sio kwamba kwa sabab mim ni muislam ila nikiangalia hata mwamko tu wa wananchi, na sehemu za kufurahia katika hizi sikukuu zote hii siku huwa ina shamra nying mno.

Karibuni pilau
View attachment 2596292
Kuhusu ipi inafana zaidi inategemea na wapi unaishi na jamii inayokuzunguka ni watu wa mlengo upi.
Usitarajie matokeo utakayopata Mikoa kama Pwani, Tanga, na Lindi itaweza kufanana na Mikoa ya bara kama Mbeya, Mwanza na Arusha
 
Eid Mubarrak wana Jf,

licha ya utofauti wa kiimani baina ya islam na christian ila Watanzania tumekua ni watu wamoja. Na tumeunganishwa na utanzania wetu. Sikuu ya kiislam huwa ni sikukuu ya taifa zima na ya kikristo pia vivyo hivo, jambo la kumshukuru sana mungu.

Kwa upande wako sikukuu ipi huwa inabamba zaidi kati ya Eid, pasaka na xmass.

Kwa upande wangu mimi huwa inaanza Eid hii ya ramadhani Then Xmass. Na sio kwamba kwa sabab mim ni muislam ila nikiangalia hata mwamko tu wa wananchi, na sehemu za kufurahia katika hizi sikukuu zote hii siku huwa ina shamra nying mno.

Karibuni pilau
View attachment 2596292
kweli sikukuu ni za kitaifa lakini huwa zinabamba kulingana na maeneo.Mf sikukuu ya id maeneo ya zanzibar,dar,mtwara,lindi haifanani na mbinga au njombe hata mbeya,upo?
 
wanyakyusa huwaambi kitu kuhusu nane nane ni moja la sikukuu kwao yaaan mtoko haswaaaa wanapika mpka pilau na nguo mpya hizo nyingne zilizobaki zinawahusu nyie watu wa dar
 
Christmas ndio sikukuu pendwa duniani kote. Idd haifikii hata nusu ya inavyosherehekewa Christmas. Hapa Tanzania ndio kabisa kila kona ya nchi inakuwa na heka heka ya maandalizi. Na watu wengi wanaamua kwenda kusherehekea vijijini kwao
 
kweli sikukuu ni za kitaifa lakini huwa zinabamba kulingana na maeneo.Mf sikukuu ya id maeneo ya zanzibar,dar,mtwara,lindi haifanani na mbinga au njombe hata mbeya,upo?
Hapo nimekupata mkuu, kama Eid ya znz ni balaaa sijawah ona sikukuu kama ile.
 
Christmas ndio sikukuu pendwa duniani kote. Idd haifikii hata nusu ya inavyosherehekewa Christmas. Hapa Tanzania ndio kabisa kila kona ya nchi inakuwa na heka heka ya maandalizi. Na watu wengi wanaamua kwenda kusherehekea vijijini kwao
Maandalizi ya eid ni almost whole month of ramadhani, lakini nahisi ni kutokana na maeneo
 
Mkuu sikukuu za kikristo usifananishe na za kiislam.....za kikisristozinasheherekewa kwa ukubwa sana sana
Wapi huko? Vijijini lkn sio JIJINI DAR ES SALAAM.

DAR, X MASS + PASAKA ni sikukuu za Kawaida ukilinganisha na EID hasa hii ya ul Fitr.

X mass ni huko Mbeya kwa walima viazi.
 
Ndo nafika muda huu humu ndani, nauliza wale waslamu swala 5 hawajaja kukukaanga baada ya kusema unapeta fresh na sikukuu za kikristo
 
Inategemea na maeneo na ukanda pia,pasaka hufunika katika maeneo yaliyo na wakristu wengi,huwezi kwenda kusherekea sikuku ya pasaka zanzibar mana karibia robo tatu ya watu watakuwa katika mfungo wa ramadhan

Hata sikuku ya idi pia ina maeneo yake kwan si kila sehemu kuna waislam wa kutosha kuweza kuifanya iwe vibe.Nimekaa maeneo ya Zanzibar kwa mda wa miaka zaidi ya minne ,sikuu zote zimenikuta huko.

Sikuku ya pasaka ukiwa Zanzibar shamla zake hutaziona labda uende kanisani wakati wa usiku au asubui ya pasaka ,kisha ukale pilau lako then uende viwanja huko utapata vibe.kwenye bar vibe lipo na sijui kama wanywaji wana sikuku maalum mana huwa wapo tu.

Miaka ya nyuma mimi kama mkristu kwenye familia yetu tulikuwa hatusherekei kabisa sikukuu zisizo za kikristu.
Yani unaweza kukuta ni siku ya idi lakini tunaenda shamba kulima na hakuna mshituko au mwamko wowote ,miaka ya 90s huko hasa maeneo ya mikoani na sehemu zilizo na wakristu.

lakini sikuku kama pasaka,x-mas na mwaka mpya watu walikuwa hawalali,ilikuwa ni kukesha hadi asubui,

Miaka imeenda baadae mchanganyiko wa watu ukaongezeka,hapa muislam hapa mkristu,lakini sikukuu zilikuwa na vibe la hatari ,watu waliburudika wakubwa kwa wadogo,pilau lilipikwa kila kona ya mji,watu walinunua nguo mpya na zawadi za kutosha.Pilau ilisikika katika pande zote nne za dunia
Nyumba zilikuwa zinafungwa ,watu wote wanatoka nyumban kwenda viwanja,hiyo siku mtu asiye toka nyumban atatoka.wasio pika pilau kwao watapika ,wasio kula nyama watakula

Miaka ya 1990 hadi 2005 kulikuwa na vibe sana kwenye sikukuu ,uchumi ulikuwa sio haba ,wenye kulima walivuna,wafanyakazi mishahara kidogo lakini ilikizi mana tozo zilikuwa sio za kuumizana kama leo hii,bei ya vyakula ilikuwa chini,bei ya bia ilikuwa chini ,sodo bei poa .
Kiukweli uchumi haukuwa wa kutesana sana,mana hata asiye kuwa na pesa chakula alikuwa nacho,hivyo uhakika wa kupika ubwabwa maharage ulikuwepo

Siku zimeenda mara mikesha ikazuiliwa,watu kuwepo mtaani mwisho saa sita,marufuku kuwasha mioto wala kulipua fataki hadi kibali maalumu.
Marufuku kupiga mziki hadi kibali maalumu.
Mtaani kusherekea sikukuu mwisho saa sita ,ukikutana na wazee usiku zaidi ya saa sita lazima wakunyanyase tu,ikawa kukimbizana na polisi licha ya kutambua wazi kuwa watu wanasherekea sikukuu lakin walikomaa tu na saa sita yao eti watu walale na wakati ndo mwanzo vibe linapamba moto.

Maisha yakaenda,uchumi ukawa una dolala kwa mtu mmoja mmojatozo zikapamba moto,mvua hazinyeshi,mtu analima lakini havuni,mfanya kazi ndo angalau ,lakini vitu bei ipo juu,ukishika hela inapotea utazani kuna chuma ulete

Ikafika mahali hata polisi hawasumbuki na kufukuza mtu mtaani,ikifika saa tatu unajirudiaha tu nyumbani mwenyewe,mana hela huna utaenda wapi sasa! Na ukafanye nini!

Watu wakawa wanaenda makanisani usiku wakitoka huko wanaelekea kulala tu,hakuna vibe la mkesha tena,upepo wa kiuchumi haupo poa,kila mmoja mnyonge yani hakuna mwamko wa kisherekea kabisa .
Kesho yake watu wanapika kilo mbili za pilau wanakula wanamaliza ,hata hela ya soda wengine walikosa je ya kwenda viwanja itapatikana?

Watu wakawa wapole,siku ya sikukuu , saa tutu tu za usiku mitaani panakuwa peupeee ,watu hakuna kila mmoja yupo makwao kulala.Disco zinapogwa ila watu ni wakuhesabu na ni wale wanao jiweza kidogo tu.

Ikafika mahali mwenye pesa yake ndo mwenye sikukuu kama huna pesa wewe huna sikukuu ,watu wakazoea mwishowe sikuu imekuwa ya kawaida na watu wanaichukulia poa tu
Yani ni bora uzima ,bora tumefika,bora tumeuona mwaka ,mengine majaaliwa.

Sikukuu ina vibe,sikukuu ni furaha ,sikukuu ni amani ya dunia sikukuu ndo uzima wa mwanadamu ,sikukuu ndo kila kitu katika maisha ya duniani ,mana tupo kwa furaha ,siku zetu ni chache za kuishi na uwepo wetu haujirudii .

Tufarahini inapobidi na tufahi kwa amani ,hata kama huna kitu we furahi tu ila sikukuu zilikuwa na vibe sana zamani kuliko sasa.
Duh hii post imeakisi jina
 
Back
Top Bottom