Eid Mubaarack. تقبل الله منا ومنكم

Eid Mubaarack. تقبل الله منا ومنكم

naona kunawatu wanataka kuleta harufu ya kisiasa hasa jamaa wa chadema

niwakumbushe eid haiwahusu kwa mtindo huyo wallah
 
Mufti ametangaza?
Kwa mujibu wa fiqihi au sharia ya kiislamu kazi ya mufti ni kutoa majibu ya maswali mbalimbali yanayowatatiza waislamu na sio kutangaza mwezi.
Ilivyokuwa taasisi kadhaa za kiislamu zinaongozwa na watu ambao hawana elimu ya kutosha kutoa majawabu ya maswali na kadhia mbalimbali zinazowahusu waislamu ndio wakajipachika majukumu mepesi sana ambayo hayalazimishi kuwa na elimu kama hayo ya kutangaza mwezi .
Kazi ya kutangaza mwezi unaweza fanywa na mwislamu yeyote hata kama hata alifu hajawahi kuisoma
( isipokuwa bubu tu ) kwa kuwa jambo la muhimu ni kujua kuzungumza kiswahili kwakuwa taarifa ya mwezi hutolewa kwa waswahili.
 
Kesho jumapili ya tarehe 30 march 2025 ni sikukuu ya Eid Al fitri kwa waislamu wote duniani.

Eid hii inakuja baada ya kuonekana mwezi wa shawwaal (mfungo Moshi ) ambao ni alama ya kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Taarifa za kuonekana mwezi wa shawwaali zimepatikana toka mataifa mbalimbali ya kiislamu ikiwa pamoja na Saudi Arabia, Qatar na Umoja wa Falme za kiarabu UAE.

Mtume Muhammad صلى الله عليه وسلم amesema: "fungeni kwa kuonekana mwezi, na fungueni kwa kuonekana mwezi, na mwezi ukifunikwa juu yenu(msiuone) kamilisheni siku thelathini)

Kunako majaliwa mimi nataraji kuswali swala ya Eid kesho asubuhi saa Moja na nusu katika uwanja wa Mandela mtaa wa Pasua manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro..

Namuomba Allaah azikubali ibada zetu za mwezi wa Ramadhani, na kwa rehema zake atupe uwezo na umri wa kuifikia Ramadhani ya mwaka ujao. Aammiyn.
Nyie watu hata hamueleweki, kama naniliu tu.... mnatuharibia sana ratiba zetu na hata sirikali kuna wakati haielewi
 
Je Bakwata watakubali
Sio lazima kukubali. Wao Wana wafuasi wao wanaotegemea taarifa zao ila waislamu wanaojitambua huwa hawategemei taarifa za bakwata kwakuwa hakuna mahala ambapo Allaah kawapa kibali bakwata kuwa wasemaji wa waislamu.
 

Attachments

  • IMG-20250329-WA0039.jpg
    IMG-20250329-WA0039.jpg
    53.5 KB · Views: 11
Hakuna miezi miwili duniani..
Ni swala la Elimu tuu. Hao wasoma dini ya kislam wengi hawataki kusoma na Elimu za sayansi hivyo akili zao zimekuwa zakukariri tu.
..
Mwezi unaweza kuonekana Dodoma ila Dar usionekane sio hakuwepo, laahasha, ila ni Swala la majira(Mwanga wa jua, mawingu, milima, humidity, n.k).

Nakumbuka mwaka flani nikiwa mdogo mkoani kilimanjaro kijiji nilichokuwepo tuliona mwezi ila hakukutangazwa kuwa ni Iddi kitaifa(hapa mfano utasemaje).

Ndo maana kamwe hutoona Nchi ambazo wameletea dini kama Saudia Arabia wanachangamoto hizi za Idd kwasababu ukiacha dini ila wanashirikisha na Sayansi

Pia kwa vile nchi yao ni jangwa hivyo kuandama kwa mwezi hunaonekana zaidi kwani hakuna mawingu jioni.

Mwezi ni mmoja mambo sijui eti uwepo kenya alafu Tz usiwepo ni ukosefu wa elimu tuu za sayansi na kubaki kuriri tu
Jielimishe kwanza hlf uje uandike tena
 
EID MUBARAK MY BELOVED MUSLIMS AND ALL NON MUSLIMS🕋🕋🌹💝💝💝💝💝💝💝💝💖💘💕💞♥️💌💜🎉
 
Jielimishe kwanza hlf uje uandike tena

Ungekuja kupangua hoja moja moja nione nina haja ya kujielimisha.

Mwezi ni mmoja hakuna miezi miwili. Nyie fata mkumbo ambap mmekariri kwa kuambia hamtaki kusoma ndo shida inapokuja.

Ukweli upo Asilimia 95 ya wasomi wa dini ya kislam elimu ya Sayansi au dunia ni sifuri
 
Mufti kashasema idd ni tar 31 au tar 1 hiyo ya idd ya kesho ni ya wavaa suruwale fupi na makobazi.
Hata hizo nchi zilizotangaza kuuona mwezi zina mamufti Tena wenye elimu kushinda hawa mashehe ubwabwa wa hapa Tanzania.
Mwezi umeonekana Saudi Arabia, Qatar na Umoja wa Falme za kiarabu.
Hapo kuna mamufti watatu wenye elimu za kutosha ambao wamethibitisha mwezi umeonekana , Sasa Mimi niache kuwasikiliza mamufti watatu wa nchi za kiislamu ningoje ngonjera za mufti wa bakwata ?!
 
Back
Top Bottom