Hammaz
JF-Expert Member
- May 16, 2018
- 7,035
- 15,332
Uwe na amani ndugu yetu, tunakupenda vilevile kwa ajili ya Allah. Mapenzi baina yetu ni haki.Baarakallaahu fiykum.
Ninakupendeni kwa ajili ya Allaah.
Nyinyi ni ndugu zangu hasa!
Mungu wetu ni mmoja.
Mtume wetu ni mmoja.
Kitabu cheti (Quran ) ni kimoja.
Na kibla cheti ni kimoja.
Kupendana ni lazima hata kama tunapishana uelewa katika baadhi ya mambo.
Mimi bado sikukuu imenishughulisha lakini nataraji baadae nitapata nafasi ya kufafanua kwa yale ambayo hamjanielewa au mmenielewa tafauti na nilivyokusudia.
Jambo ambalo nasisitiza ni kwamba mwanzo wa uzi huu hapakuwa na nukta ya kuwakosoa wenye msimamo wa mwezi wa kitaifa.
Nilianza kujenga hoja kutetea msimamo wetu na kuonyesha dosari zilizopo katika msimamo wa wenzetu baada ya wachangiaji kuanza kukosoa msimamo wa wale walioswali Eid siku ya leo.
Pamoja na yote hayo hapajaharibika neno Bado nafasi ya kuendelea kuonyeshana hoja za kila upande ipo na haimaanishi kwamba ni ugomvi.
Kwasababu naona kuna baadhi ya maeneo nimeeleweka vibaya nitakapokuwa tayari nitaanza kuzungumzia msimamo wetu juu ya ikhtilafu za wanachuoni inshaa Allaah.
Eid Mubaarack.
تقبل الله منا ومنكم.
Ikiwa kama kuna sehemu yoyote kwenye mjadala nilikukwaza unisamehe. Kwa upande wangu hukunikwaza, hivyo natanguliza kuomba radhi kama niliteleza popote kwa bahati mbaya kama nilikukwaza ndugu yangu unisamehe.
Mungu wetu ni mmoja,
Mtume wetu ni mmoja,
Kitabu chetu ni kimoja,
Na kibla chetu ni kimoja.
Naam, umesema kweli, kupendana kwetu ni lazima hata kama tunatofautiana katika baadhi ya mambo.
Eid Mubaraka na kwako pia na kwa familia yako na kwa waislamu wote kwa ujumla ambao leo wanasheherekea sikukuu ya Eid.