Eid Mubaarack. تقبل الله منا ومنكم

Eid Mubaarack. تقبل الله منا ومنكم

Kesho jumapili ya tarehe 30 march 2025 ni sikukuu ya Eid Al fitri kwa waislamu wote duniani.

Eid hii inakuja baada ya kuonekana mwezi wa shawwaal (mfungo Moshi ) ambao ni alama ya kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Taarifa za kuonekana mwezi wa shawwaali zimepatikana toka mataifa mbalimbali ya kiislamu ikiwa pamoja na Saudi Arabia, Qatar na Umoja wa Falme za kiarabu UAE.

Mtume Muhammad صلى الله عليه وسلم amesema: "fungeni kwa kuonekana mwezi, na fungueni kwa kuonekana mwezi, na mwezi ukifunikwa juu yenu(msiuone) kamilisheni siku thelathini)

Kunako majaliwa mimi nataraji kuswali swala ya Eid kesho asubuhi saa Moja na nusu katika uwanja wa Mandela mtaa wa Pasua manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro..

Namuomba Allaah azikubali ibada zetu za mwezi wa Ramadhani, na kwa rehema zake atupe uwezo na umri wa kuifikia Ramadhani ya mwaka ujao. Aammiyn.

View: https://www.youtube.com/live/WPPNis4ZaTU?si=UTqmAu3vMuU5KnkE
BILIONEA DAVIS MOSHA NA UPENDO WA SIKU 30 ZA IFTAR NYUMBANI KWAKE
 
bila shaka idd ni jumatatu.kesho lazma mwezi utaonekana mkubwa
kwanini uonekane mkubwa na leo umeonekana nch 3 tu Qatar, UAE na Saudi hizi nchi nyingine kwa nini haujaonekana? na kwanini ukionekana nchi izo ambazo leo haujaonekana kwanini uonekane mkubwa?

Huu mwezi unatuchonganishe ee? haiwezekanu uonekane nch 3 tu dunia nzima
 
Back
Top Bottom