Ombeni sefue katumbua jipu zito ITV jamani
Kumbe ile kampuni iliyotupiga ikishirikiana na Stanbic bank wahusika ni Harry Kitilya aliyekuwa kamishina mkuu wa TRA na Mboya. Sasa ukitaka kujua dunia haramu +na yule miss utaelewa sasa na yeye aliingizwaje!!
Mh. Magufuli, kurudishiwa hela haisaidii tunataka walioohongwa wafungwe waende ndani.
SFO wametaja waliohusika ni mzee wetu H. Kitilya na Mboya. Kuweka nchi iwe na adabu wapelekwe mahakamani na kesi isikae mizezi 3.
Na kama wao wana ama walitumika kama middleman wasema top nani.
Taarifa ya SFO inasema wazi kuwa Harry Kitilya alikuwa kwenye timu maalum ya serikali ya Tanzania iliyokuwa inahusika kutafuta huo mkopo na wakati huo huo alikuwa ni 'wakala' wa Stanbic bank! Huu ni uhuni na utani uliopitiliza! Kamishna wa Internal Revenue (appointed by the President) anajigeuza kuwa agent wa Bank tena wakati anaongoza mazungumzo kati ya serikali na hiyo Bank? Sasa kwenye meza ya mazungumzo alikuwa anawakilisha upande gani? Serikali au wakala?
Lakini kuna kitu kingine hapa, Shose Sinare kama sikosei ni mtoto wa Dr Hawa Sinare. Huyo mama ni mjuzi wa 'double agent system'. Rex Attorneys ambako ndiko aliko huyo mama walifanya hivyo hivyo kwenye mgogoro wa Dowans na Tanesco, walikuwa wanawakilisha pande zote! Yote tisa, kumi, Dr Hawa Sinare aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa bodi ya Kahawa wakati huo akiwa anasimamia (kama wanasheria) uuzwaji wa mali za KNCU!. Na siku chache kabla ya uchaguzi akatangaza kujiondoa CCM na kumuunga Lowassa mkono. Sasa binti yake ndio hivyo yuko kwenye saga ya Stanbic. Shida.
Usaha ulimrukia mwenyewe usoni.kimyaaaa ana vimeo kama vitatu na vyote amezusha yeye
Uyo uyo kwenye uzi wake wa nan anastaili kuwa waziri wa fedha,jamaa kamsifia sana Kitilya,kumbe mpiga dil tu
Ni nani nchi hii msafi?? Hata huyo Magu mbona nae kaiba, ile Hotel kwani kajenga kwa pesa zake??
The Boss alikuwa anaongelea ujuzi na uzoefu wa Kitilya na angeisaidia vipi nchi kukuza Uchumi wetu..
Hivi hata wewe kila unakogeuka unaona wenzako wanaiba tu, hivi na wewe utaacha kufanya hivyo?? Si tunasemaga Samaki mmoja akioza au?? Hakukuwa na msafi yeyote kwenye serikali ya JK
Kwanza nampongeza Kitilya kufungua consultancy baada ya kustaafu na sio kwenda kulima au kufuga ngombe na kuku!, ili at such senior position, ukistaafu unaendelea kufanya kazi za brain power!.Pasco njoo huku
Shose ni Senare, binti wa Melckzedec Senare (RIP), mtangulizi wa Kitilya pale TRA!. Dr. Hawa ndio Sinare, mwanasheria nguli, na mwalimu wa kujitolea wa sheria UDSM!.Lakini kuna kitu kingine hapa, Shose Sinare kama sikosei ni mtoto wa Dr Hawa Sinare. Huyo mama ni mjuzi wa 'double agent system'. Rex Attorneys ambako ndiko aliko huyo mama walifanya hivyo hivyo kwenye mgogoro wa Dowans na Tanesco, walikuwa wanawakilisha pande zote! Yote tisa, kumi, Dr Hawa Sinare aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa bodi ya Kahawa wakati huo akiwa anasimamia (kama wanasheria) uuzwaji wa mali za KNCU!. Na siku chache kabla ya uchaguzi akatangaza kujiondoa CCM na kumuunga Lowassa mkono. Sasa binti yake ndio hivyo yuko kwenye saga ya Stanbic. Shida.
Ningeomba THE BOSS aje alisemehe ili maana anamkubal sana uyo KITILYA
Dah inasikitisha kuona uingereza inatusaidia kuibua madudu yetu, hivi hao mabalozi wanakazi gani huko abroad, nikweli hawajui maofisa wetu wanapokuja huko wanafanya madudu gani, ofisi zao huwa wapo waambata kibao mpaka maofisa usalama, ila nasikia wanalipwa mishahara duni, (but where is loyalty) hata hvyo nyie maofisa waandamizi, nyie wasomi wetu kwenye positions muhimu ni mbwembwe tu, majivuno, suti, magari na nyumba zakifahari, lakini ni aibu tu. Huwa mnajidai tu lakini hamna lolote. Yani mmeitia aibu nchi na raia wake. Hamna hata aibu, nasasa mnaumbuka.
Kwa jinsi Sefue anavyoongea je kama Ikulu ilishiriki wakati huo je yeye atapoma maana sasa hivi anajifanya mkali wakati kipindi kile alikuwa mstari wa mbele kutetea uovu wa Ikulu na hakuwa upande wa wananchi.Sefue ametumia lugha laini mno! Anasema kama kuna watu walihongwa! Kah!!! Waingereza wamesema wazi kuwa zile pesa zilitumika kuwahonga maafisa wa serikali Tanzania!
Sefue anataka kuweka credit kwa benki kuu Tanzania kitu ambacho Nina mashaka nacho, benki nao in watuhumiwa katika hili! Ningewaelewa kama wangekuwa wa kwanza kukamata hawa wezi na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola bila kusubiri hisani ya waingereza kutukamatia!
Kama waingereza wasingefuatilia sidhani kama hii pesa ingerudi! Inaonekana kabisa hapa kuna ubia wa uovu kati ya benki kuu na stanbic bank! Haiwezekani hii benki ikawa inatoa Fedha cash kwa mabilioni katika muda mfupi bila kuwa na hofu na benki kuu kama hawana ubia! Wakati wa sakata la escrow ni hawa hawa waliruhusu pesa zichukuliwe kwenye viroba kwa mabilioni na mpaka Leo "wamegoma" kutoa orodha ya wahusika na wanaendelea na biashara kama kawaida pamoja na bunge kupiga makelele!
Namwomba Magufuli awatembelee kwa kushtukiza na awaombe hiyo orodha ya escrow tuone kama naye watamgomea! Hilo jipu linamsubiri Magufuli maana watanzania wanalijua japo nasikia inasemekana limekaa pabaya!! Tukubali tuna matatizo makubwa ya uadilifu benki kuu, wanakubali kutumiwa na mafisadi!
huyo kamanda wako wakipuuzi aje tena aendelee na zile porojo zake kwenye serikali hii ya magufuli aone moto wake. maana alikuwa mzushi aliyepitiliza kwa kutuletea uongo humu.Kuna mmiliki mmoja wa Hiyo kampuni ni marehemu,kila nikiona SFO namkumbuka kamanda Yericko Nyerere alivyotumbua jipu la ? 1.5m
Mhh! Unamuamini Sefue? Ukali kaupata lini? Mbona akiwa na mkwere alikuwa paka mororo!