Ngaramu
JF-Expert Member
- May 7, 2009
- 382
- 78
Hauna jipya kinachokusumbua ni frustration baada ya kujaribu njia zote kumchafua Lowassa mkashindwa! Hatutaki kusikia mbwembwe zenu na fitna tuko uwanjani tuangakie mpambano!
My Sister Tiba,, hapa sasa ndipo lazima uukubali ukweli mchungu, kuwa huyu ndie rais wako ajaye!. Ni kweli hao ngombea ndio utajiri wake pekee alioanza nao maisha ila kwa vile huyu ni mtu wa Mungu, hivyo ana upako fulani kama wa Midas, everything he touches turn to gold!. Alipokuwa mgurugenzi wa AICC neema ikamwangukia, akaanza kumiliki land Arusha, Mungu akamuangazia akapewa wizara ya Ardhi, enzi hizo viwanja vikitolewa bure tena prime areas!, akajenga zile nyumba akakodisha mabalozi faida akaitumia kama mtaji wa Alfa!. Mungu akamuangazia zaidi akapewa wizara ya Mifugo, Ranchi ya zaita zikauzwa kwa bei ya bure na yeye uwezo alikuwa nao hivyo akanunua!. Mungu akambariki zaidi na kumfanya akawa Waziri Mkuu wetu lakini katika maandalizi ya kumfanya awe rais wetu, Mungu akampitisha kwenye majaribu ya Richmond, ili iwe kama kawaida baada ya mateso na kifo, huja ufufuko na uzima wa milele, sasa hii ndio safari ya kukitwaa kile kiti alitayarishiwa na Mungu mwenyewe, au hukumsikia TB Joshua?!.
Kilichoanzisha Alfa ni mtaji kutokana na vitega uchumi vyake, hata hizo Nyumba London ni faida tuu kutoka vitega uchumi vyake!.
Kwa vile ni mtu wa Mungu na mwenye upako wa neema, hao marafiki zake wanaomchangia wamejikuta wanabarikiwa sana hivyo kuchanga zaidi na zaidi kama sadaka tuu makanisani, hawasubiri kuja kulipwa baadae ila kila ukitoa tuu unajikuta unazidishiwa mara sabaini fii sabaa!.
Hiyo the bottom you are very right, EL is not clean!, yae he is not, hata JK was not clean, but he was!, hata CCM is not clean, but it is!, hata YULE aliyekuja kuukomboa ulimwengu huu, aliisha sema hakuja kwa ajili ya wakamilifu!, alikuja kwa ajili ya hao hao ambao sio clean!. Na akasema "Wainuliwe wote wenye mizigo waje kwa YEYE wapumzishwe!", ndio maana hata lile zigo la Richmond, amelibeba tuu sio lake, na sasa anasubiri kuinuliwa ili apumzishwe kule juu!.
Kama JK amweza kuwa presidential material na ametutawala miaka hii kumi, EL ni 100 times better, ataiinua hii nchi kutoka huku kwenye vumbi na majajala na kutupeleka kwenye ile nchi ya ahadi, mabomba mchi nzima yatatoa maziwa na asali!.
Hata alipokuja YEYE, mwanzo alikataliwa hivi hivi mnavyotaka kumkataa huyu mtu!, hivyo sasa YEYE aliyemwandikisha atajidhihirisha utukufu wake kwenu, kwa "lile jiwe walilolikataa waashi, litafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni!",
Amesema "Huu ni mwamba na juu ya mwamba huu, nitalifa taifa langu!".
Just wait and see!.
Pasco
Mtajamba sana mwaka huu na hili JIZI lenu. Hata hamwelewani kauli.
Je, akiukwaa URAIS atajiuzia kitu gani tena jamani, UWIIII nchi yetu!!!