KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,149
Badiliko hili wala halina TIJA kwa CCM. Ni mjinga tu atakayeacha UBUNGE akagombee U-NEC wa CCM. Ni moja ya mabadiliko ambayo yanahanikizwa na nguvu nyingi walizonazo baadhi ya watu kuliko CCM na vikao vyake. Subiri tu kuonyeshana nguvu kutakakojitokeza ya MNEC wa CCM na Mbunge wa CCM.
Atakufa lowassa wako ccm palepale mzee....Don't waste ur time Man, CCM ni chama ambacho kimeshakufa kinachofanyika sasa ni postmortem ya kuhalalisha sababu ya kifo cha marehemu.
Hakuna dini inayohubiri Umaskini!!
KIM K, hoja zako huwa hazina mashiko kutokana na CHUKI na UDINI
Ezekiel huyo katibu wa uvccm jimboni kwa mamvi ni darasa la saba
bora wewe umeuliza.
Jibu - ndiko walikoanzia wakati wanaingia mjini!
Ulikuwa hujui hilo?
Kweli mkuu kwanini Matola hajiamini?Kaka Matola usiwe na wasi wasi juu ya uwepo wangu hapa. Ni kweli mimi ni mzoefu hapa jukwaani na kwa kuwa huu ni wakati wa kujivua gamba na langu pia nimelivua ili kusogea hatua moja mbele katika mapambano.
Usifunge milango kwa watu kujivua gamba mkuu, kuna haja ya kuibadili jamii forum ili tukutane ana kwa ana kama walivyo akina Zitto Kabwe, Slaa, Mwigulu, Nape, Mnyika na n.k. .Vile vile si lazima ama haijalishi kumpata Matola halisi ama nick name hapa jamvini ila uzito wa hoja mkuu.
Kuhusu kutokuonekana kwenye sehemu nyingine nadhani hapa hujawa sahihi, kila mtu ana jukwaa lake kama ambaye anapenda kuwa jukwaa la "mapenzi", "udaku" ndivyo hivyo na sisi wengine tunapatikana hapa Mkuu.
Acha uwongo . Lowassa siyo mjinga kiasi hicho yaani badala ya kutumia wapambe yeye mwenyewe ndo atume msg ? Hujanishawishi bado we utakuwa umetumwa . Hajafikia kufanya ujinga mraisi kama huo.
NabiiRafiki zangu wa karibu sana Mheshimiwa Pasco & Matola,
Niliwaambia Lowassa alishapotezwa siku nyingi wakanibishia sijui mpaka leo na baada ya kusoma kisa hiki bado wana amini Lowassa is next President ?.
Kitendo cha Lowassa kumuumbua Mwenyekiti wake ndani ya kikao cha Halmashauri kuu ya taifa kwamba alijua kila kitu katika ule mradi tata wa RICHMOND & DOWANS na kwamba alipelekewa jina la Rostam Aziz na kulikubali wakati mwenyekiti alishajitetea hamjui mmliki wa RICHMOND & DOWANS alikuwa akitengeneza jeneza lake kwa mikono yake mwenyewe.Lowassa alikwenda mbali sana alipohakikisha mazungumzo yake yanawafikia wahariri wa magazeti kupitia simu za kiganjani ndani ya kikao cha Halmashauri kuu !.