Kampeni zimeshaisha, ulitaka aseme nini kila siku,?
Baada ya kampeni watu wanapumzika kabla ya kuanza hatua inayofuata.
Mapambano bado yanaendelea ya kumkomboa mtanzania kutoka kwa mkoloni ccm.
Lowasa yuko mioyoni kwa watanzania walio wengi, ndio maana pamoja na kupewa mapumziko ya kuapishwa kwa mnayemuita raisi, nchi iko kimya kama kuna msiba.
Wadau, amani iwe kwenu.
Ilikuwa ni jambo lililozoeleka kila unapotune radio ama kuangalia TV au kuperuzi gazeti na hata kuangalia mitandao ya kijamii kusikia ama kuona jina la Lowasa likitawala kwenye media hizo. Hali hiyo iliwaaminisha baadhi ya Watanzania kuwa hakuna mtu muhimu Tanzania kama Edward Lowasa. Tena wengine wanadiriki kusema kuwa eti Magufuli anakalia kiti ambacho si chake.
Cha kushangaza zaidi, tangu tarehe 1 Novemba, jina la Lowasa limepotea ghafla kwenye media nchini. Hii imekuja siku mbili tu baada ya Dr Magufuli kukabidhiwa cheti cha ushindi wa nafasi ya Urais, hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.
Kwa sasa ni jambo la kushangaza kuona hata zile media ambazo kila uchwao walikuwa wanatuaminisha kuwa Lowasa ndiye mkuu katika taifa hili wameacha kutangaza habari zake. Mathalan, ITV na Channel Ten, TV zilizokuwa zinatumiwa na Lowasa kama mdomo wake hawajaonesha taarifa yoyote ya Lowasa tangu juzi. Hii ni kusema kuwa TV hizi zimebadili gia angani na sasa wanatumia muda mwingi kutoa habari za Magufuli.
Bye Bye Lowasa.
Lumumba mnajitekenya na kucheka wenyewe
Lumumba mpo kazini,
Kitufe cha like ndio kilikuwa kinatumiwa na wale jamaa wa milimani city kupeleka trafic kubwa kwenye server ilikohostiwa JF kama njia ya kuhack kwenye kupitia layer 7 baada ya kupigwa pin layer 4 ndio maana ilipotea halafu unajifanya hujui mlichokuwa mnafanya cc Invisible Max meloHalafu JF siku hizi haina kitufe cha like. Sijui kimeenda wapi
Kumbe Sera ya mabadiliko haikuwa ya chadema ilikuwa ya lowasa hivyo ameondoka nayo.Ni wenye upeo na IQ kubwa tu ndo wanajua Alichowafanya Lowasa , Kutoka viti 74 vya upinzani ndani ya Bunge 2005 - 10 hadi zaidi ya viti 120 vikiwemo Viti Maalumu, Angalia Baadhi Miji Mikubwa mliyoitamani ikiwemo Dar es salaam (Nape kakiri ) Bakora za Lowasa zimewacharaza.
Mbegu ya mabadiliko Aliyoipanda Lowasa Ndani ya Mioyo ya watanzania wengi wakiwemo Vijana subirini Mavuno yake mtayaona miaka mitano ijayo, kwani ahadi alizoahidi Mh;Pombe Elimu Bure , Tanzania itakayojaa viwanda , Meli mbili kubwa ,Maji kutoka ziwa victoria Hazitekelezeki
Mkuu si unajua tena moto wa mabua,namnukuu JKWadau, amani iwe kwenu.
Ilikuwa ni jambo lililozoeleka kila unapotune radio ama kuangalia TV au kuperuzi gazeti na hata kuangalia mitandao ya kijamii kusikia ama kuona jina la Lowasa likitawala kwenye media hizo. Hali hiyo iliwaaminisha baadhi ya Watanzania kuwa hakuna mtu muhimu Tanzania kama Edward Lowasa. Tena wengine wanadiriki kusema kuwa eti Magufuli anakalia kiti ambacho si chake.
Cha kushangaza zaidi, tangu tarehe 1 Novemba, jina la Lowasa limepotea ghafla kwenye media nchini. Hii imekuja siku mbili tu baada ya Dr Magufuli kukabidhiwa cheti cha ushindi wa nafasi ya Urais, hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.
Kwa sasa ni jambo la kushangaza kuona hata zile media ambazo kila uchwao walikuwa wanatuaminisha kuwa Lowasa ndiye mkuu katika taifa hili wameacha kutangaza habari zake. Mathalan, ITV na Channel Ten, TV zilizokuwa zinatumiwa na Lowasa kama mdomo wake hawajaonesha taarifa yoyote ya Lowasa tangu juzi. Hii ni kusema kuwa TV hizi zimebadili gia angani na sasa wanatumia muda mwingi kutoa habari za Magufuli.
Bye Bye Lowasa.
Tena inapasuka wakati hata sherehe hazijaanza teh tehLizaboni ngoma ikivuma sana inapasuka