Media zimepiga hela zake za ufisadi vya kutosha....kwa sasa wamemtupa kama toilet paper. Hana ishu tena.
Halafu JF siku hizi haina kitufe cha like. Sijui kimeenda wapi
Wadau, amani iwe kwenu.
Ilikuwa ni jambo lililozoeleka kila unapotune radio ama kuangalia TV au kuperuzi gazeti na hata kuangalia mitandao ya kijamii kusikia ama kuona jina la Lowasa likitawala kwenye media hizo. Hali hiyo iliwaaminisha baadhi ya Watanzania kuwa hakuna mtu muhimu Tanzania kama Edward Lowasa. Tena wengine wanadiriki kusema kuwa eti Magufuli anakalia kiti ambacho si chake.
Cha kushangaza zaidi, tangu tarehe 1 Novemba, jina la Lowasa limepotea ghafla kwenye media nchini. Hii imekuja siku mbili tu baada ya Dr Magufuli kukabidhiwa cheti cha ushindi wa nafasi ya Urais, hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.
Kwa sasa ni jambo la kushangaza kuona hata zile media ambazo kila uchwao walikuwa wanatuaminisha kuwa Lowasa ndiye mkuu katika taifa hili wameacha kutangaza habari zake. Mathalan, ITV na Channel Ten, TV zilizokuwa zinatumiwa na Lowasa kama mdomo wake hawajaonesha taarifa yoyote ya Lowasa tangu juzi. Hii ni kusema kuwa TV hizi zimebadili gia angani na sasa wanatumia muda mwingi kutoa habari za Magufuli.
Bye Bye Lowasa.
Kampeni zimeshaisha, ulitaka aseme nini kila siku,?
Baada ya kampeni watu wanapumzika kabla ya kuanza hatua inayofuata.
Mapambano bado yanaendelea ya kumkomboa mtanzania kutoka kwa mkoloni ccm.
Lowasa yuko mioyoni kwa watanzania walio wengi, ndio maana pamoja na kupewa mapumziko ya kuapishwa kwa mnayemuita raisi, nchi iko kimya kama kuna msiba.
Nitakuwa mchoyo wa fadhira kama nisipo mshukuru Lowassa kwa kuniwezesha kipesa pia. Wengi mlikuwa mnapoteza muda kumshangilia ila hela yake tumeila sisi. Tangu kutangaza nia Arusha hadi kutafuta wadhamini ndani ya CCM. Mzee Lowassa sitakusahau, kwa kuchoma pesa wewe ni noma sana.
Mwenzio Yule Mwandishi Bingwa Wa Kujipendekeza Kwake Jamila Omary Wa Channel Ten Arusha Sasa Anamalizia Kujenga HEKALU Lake Huku Vogue Lake Likiwa Baharini Sasa Linakuja Dar. Kweli Lowassa ULIINGIZWA MKENGE Na Utajuta Sana KUPOTEZA MIHELA Yako Kwa Kukosea au Kusahau Kwamba Hakuna Bingwa Wa UNAFIKI Dunia Nzima Kama WATANZANIA Sisi Sisi. MAFURIKO Yako Sasa YAMEKUTIA HASARA Na Sijui Utawalipaje Akina TSN, Big Bon Na Mzee Bakhressa Bila Kumsahau Hanspoppe.