Lizaboni
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 33,901
- 20,410
Wadau, amani iwe kwenu.
Ilikuwa ni jambo lililozoeleka kila unapotune radio ama kuangalia TV au kuperuzi gazeti na hata kuangalia mitandao ya kijamii kusikia ama kuona jina la Lowasa likitawala kwenye media hizo. Hali hiyo iliwaaminisha baadhi ya Watanzania kuwa hakuna mtu muhimu Tanzania kama Edward Lowasa. Tena wengine wanadiriki kusema kuwa eti Magufuli anakalia kiti ambacho si chake.
Cha kushangaza zaidi, tangu tarehe 1 Novemba, jina la Lowasa limepotea ghafla kwenye media nchini. Hii imekuja siku mbili tu baada ya Dr Magufuli kukabidhiwa cheti cha ushindi wa nafasi ya Urais, hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.
Kwa sasa ni jambo la kushangaza kuona hata zile media ambazo kila uchwao walikuwa wanatuaminisha kuwa Lowasa ndiye mkuu katika taifa hili wameacha kutangaza habari zake. Mathalan, ITV na Channel Ten, TV zilizokuwa zinatumiwa na Lowasa kama mdomo wake hawajaonesha taarifa yoyote ya Lowasa tangu juzi. Hii ni kusema kuwa TV hizi zimebadili gia angani na sasa wanatumia muda mwingi kutoa habari za Magufuli.
Bye Bye Lowasa.
Ilikuwa ni jambo lililozoeleka kila unapotune radio ama kuangalia TV au kuperuzi gazeti na hata kuangalia mitandao ya kijamii kusikia ama kuona jina la Lowasa likitawala kwenye media hizo. Hali hiyo iliwaaminisha baadhi ya Watanzania kuwa hakuna mtu muhimu Tanzania kama Edward Lowasa. Tena wengine wanadiriki kusema kuwa eti Magufuli anakalia kiti ambacho si chake.
Cha kushangaza zaidi, tangu tarehe 1 Novemba, jina la Lowasa limepotea ghafla kwenye media nchini. Hii imekuja siku mbili tu baada ya Dr Magufuli kukabidhiwa cheti cha ushindi wa nafasi ya Urais, hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.
Kwa sasa ni jambo la kushangaza kuona hata zile media ambazo kila uchwao walikuwa wanatuaminisha kuwa Lowasa ndiye mkuu katika taifa hili wameacha kutangaza habari zake. Mathalan, ITV na Channel Ten, TV zilizokuwa zinatumiwa na Lowasa kama mdomo wake hawajaonesha taarifa yoyote ya Lowasa tangu juzi. Hii ni kusema kuwa TV hizi zimebadili gia angani na sasa wanatumia muda mwingi kutoa habari za Magufuli.
Bye Bye Lowasa.