Acha kulinganisha urafiki na mambo haya ya msingi. Hili tamko la kuwahusishwa Warwanda ktk ICT si ajabu mkuu lilimjia akiwa pale anahutubia ikabidi aliseme.
Maana kikawaida huwezi kuajiri watu wasiowazalendo kwa nchi yako wadesign na/kuendesha mifumo wa ICT, umeme, miundimbinu ya reli, barabara, mawasiliano, anga, jeshi nk. Hivi ina maana hata jeshi letu halina kitengo imara cha ICT mpaka leo? Hivi ni kweli hatuna system designers, analysts, programmers and developers?
Hivi kuna kiwanda kinaendeshwa bila hawa watu?
Mifumo yote ya viwanda iko automated na computer scientists and engineers, software engineers ndo wanapaswa kuautomate hiyo mifumo. Nenda TANESCO unakuta limashine likubwa linaendeshwa na computer. Sasa nchi inaazima wataalamu wa ICT nje alafu tuna ndoto ya kuwa na viwanda?
Yaani uzalishe bidhaa mechanically uje kushindana na mchina anayezalisha bidhaa zake kwa information systems!?
Basi kama hali hivyo ikitokea vita na Rwanda watatusambaratisha ndani ya mwezi. Maana cha kwanza watakachofanya ni ku-hack system zetu walizotuundia. Tunabaki bila mawasikiano alafu wanatumaliza.
The morden world is more technological than mechanical.