maroon7
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 11,341
- 15,834
Duuuh, jana nikasema ngoja niangalie BSS maana tangu ianze sijaangalia, nilichokutana nacho niliona aibu mwenyewe maana mtu unashangaa hawa washiriki wametolewa wapi,ni aibu tena kwa television inayoonekana duniani kote kuwa na washirki kama wale,ni bora wangesema mwaka huu hawajaona vipaji wakapotezea..washiriki wote ni kama wanalazimisha na hakuna hata anayeonekana anakipaji (maana kipaji huwa kinaonekana hata kama mtu hajapewa training ya kufukia makosa bado). Ushauri wangu kwa waandaaji wajaribu kwenda kutafuta vipaji sehemu ambazohawajawahi kufika kabisa kama bado washiriki hawaonekani kukidhi viwango,maana hii ya mwaka huu ni aibu tupu hata kwa majaji.