Mie hapa nitamlinda Joyce kwa upande mmoja.
Joyce siku zote anakubali kukosolewa na mie nimekuwa nafuatilia vipindi vyake almost vyote.
Na wala uwezo wake wa taaluma haufichi,na maisha aliyopitia ndio yakafanya mpaka aanzishe kipindi hiki kwakuwa ana Experience ya kutosha kwenye maisha ya namna hiyo na ndio maana ameona haitoshi ameanzisha kipindi kingine Star Tv.
Mie nahisi tatizo sio kuponda ni kwamba faida ya vipindi vyake ki ujumla ni kubwa sana kwa jamii,ni bora asaidiwe ushauri kuliko kuponda kwa ujumla kwa kosa alilofanya jana.Nakiri kweli ni kosa kubwa sana ila pia tupime mambo mazuri sana aliyafanya na anayoendelea kuyafanya Dada huyu.Ukipima basi utakuta mazuri ni more than 99%.
Tusimhukum kosa hili na kuona hajafanya mazuri.
Hata Oprah hana shule ila ana Directors wakali sana kitaaluma na kiuzoefu.
KWA JOYCE:-
Maana yule binti alianza kuwa Mateka wa ngono akiwa na miaka 13,na kwa sheria za kimahakama na kama yule MAMA akishtakiwa ni kwamba atashtatiwa kuanzia kipindi hicho kwa kumteka mtoto kingono akiwa na miaka 13 .Kwahiyo hawatoangalia umri wake wa sasa wamiaka 25 in deep,bali alipoanza
Sasa ndio kama jana,yule pale ni kwamba amesimama kama Binti wa miaka 13 kwahiyo alitakiwakulindwa ili asije kutengwa na jamii,na hasa baada ya kuonekana kwamba ni muathirika wa HIV.Na ukizingatiwa ameishatengwa na Familia yake mwenyewe.
KWA DIRECTORS WAKE:
Haya ndio mambo ya mtu kuwa muandaaji kipindi na kubeba majukum mengi peke yako,mie naamini kama ana Director huyu ndio wakulaumiwa sana.Aangaliwe vyeti na experience.
KWA EATV:-
Hiki kipindi kimenunuliwa Airtime.
Mfano wasani wengi hurejeshewa kazi zao kwamba hazina viwango vya kuruka hewani,kama nyimbo,filam nk,ambapo wahusika huenda tena kufanyakazi upya ya kurekebisha makosa.
Sasa hapo tatizo kubwa pia ni kwa waandaji wa vipindi vya EAT,sasa sijui weledi upo wapi wa taaluma ya uandishi wa habari na tukio hili.Maana kipindi sio Live ni recorded.
Mfano mmoja ni kwamba mie hufuatilia sana kipindi cha Jiji letu,huwa kuna siku mtu haonyeshwi sura,tena mtumzima tu ili kulinda maadili nauhalisia wa tukio.Na wakati mwingine hata machangudoa pia hufichwa sura.Sasa inakuwaje kwa binti kamahuyu alielawitiwa kwa miaka zaidi ya kumi,kuambikizwa HIV aanikwe namna ile.Wakati kuna waathirka wengine wa HIV huwa wanazibwa uso ili wasitengwe na jamii itakuwa huyu aliekuwa mtumwa wa ngono kwa miaka zaidi ya 12?
Hapa ningeomba jamani tusimlaumu sana Joyce,maana yeye haishi mjini kwa ku act kama ni msomi na amekuwa akilisema sana hili,ila tatizo ni watu wanaosimamia kipindi ndio ilkuwa tatizo,na uongozi wa EAT nao tatizo pia,sijui waajiri muandaaji vipindi mkenya?maana sie tunalalamika tukipewa nafasi ndio madudu kama hayo.
Pia ningeomba sana kwa hivi mlivyomuanika huyu bindi basi naomba mumsaidie,na sie pia tupo pamoja.
Joyce hongera sana kwa kazi zako nzuri,hizi ndio changamoto za kazi,umevumilia mengi naimani na hili ni lamapito tu,naamini umejifunza kitu juu ya hili.
Bana sana hao Directors wako