Joyce Kiria Wanawake Live EAT: kisa cha kusikitisha

Joyce Kiria Wanawake Live EAT: kisa cha kusikitisha

ngoshwe

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2009
Posts
4,141
Reaction score
951
Wanawake Live EATV Leo tarred 29.04.14. Kuna binti anaitwa Christina Frank anahojiwa na Joyce Kiria anaelezea stori ya kusikitisha ya kuajiria na Wanawake wenzake kwa mama mmoja hapa Dar ambapo kwa KAI za Nyangi lakini baadae kutumikishwa Kwa biashara ya kuuza mwili. Ameingiliwa kinyume na maumbile, kabakwa na kuondolewa kizazi kwa kupasuliwa na mwanaume ambae alikuja kutaka huduma kwenye danguro ambae mama aliyemwajiri alimleta kama Mteja. Anasema Alikuwa akilazimisha kutoa uroda, ameingiliwa kishenzi kinyume na maumbile na kubanwa na bisibisi ili asipige kelele...

Binti huyo ameathirika kutokana na kubakwa na sasa Hali Yale si Nzuri. Alipata hela aliyochangiwa na wasamaria alipopeleka nyumbani kwao Moshi, mama yake mdogo alimnyanga'anya hela zote na hakamfukuza. Akapata msaada wa kuelekezwa kwa Joyce Kiria. Kwa ujumla habari yake inasikitisha sana.. kaharibiwa maisha kwa ujumla.
 
Hivi ukibakwa ndio kizazi kinatoka..??! au alifanyiwa operesheni pori..?
Pole sana dada.., Mungu yu nawe..
 
Huyo mama anaejihusisha na hayo mambo nadhan anastahili awekwe ndani na pia elimu ianze kutolewa vijijini kua mtu akija kutafuta msichana wa kazi mjini,wawe wanawazuia mana nadhani ndicho kinacho wacost watu wa vijijin mana wakisikia kazi mjini wanaamin ni kazi nzuri kumbe wanadhalilishwa na kuharbiwa utu wao
 
Sijafahamu mipaka ya ile sheria yakusafirisha Binadamu (Human Trafficking).Miaka ya karibuni kumeibuka ka mtindo ka kina mama kufanya biashara ya mabinti kwa malipo manono kwa kisingizio wanawasaidia kupata kazi za majumbani.(ndani). Turekebishe huu utaratibu.

Tungeanzia huko.Wizara husika Ustawi wa Jamii na ile za Ajira zitekeleze majukumu yake kikamilifu.Watoto wetu wanapotea kupitia watanzania wenzetu wasio na ubinadamu. Huyu binti anadai wapo wengi sana kwenye hilo Danguro wanauzwa na mama anaewamiliki.Haya ni mambo ya Pataya Thailand tuyapige vita kali watanzania. Binti wa watu kaathirika kisa alikuja jijini kutafuta maisha...Inauma sana!. Stori itaendelea ...
 
Nyinyi mnashangaa wanawake wanaouza vibinti,china kuna vibint mpaka vya 15 years toka Tanzania,wamepelekwa na maboss ladies kwa kuaidiwa kazi za saloon,lakini wakifika huko wanaishia kuliwa uroda na watu mpaka 5 kwa siku.hapa dar maeneo ya sinza kuna mtaa unaitwa mtaa wa dhambi....kuna vibinti vimefugwa na wanawake wenzao(wanawaita mama) hao ndo wana panga bei na kupokea hela za kuuza miili ya hao watoto.
 
uyo binti ana miaka 23. ameeleza sana.ameshaathirika. ilo jumba lililoko oysterbay lilishasemwa sana, tena linasafirisha watoto wengine kwenda congo. watoto wengine walishaenda hadi congo kupitia jumba hilo.wadau tuambieni humu, nani mwenye jumba hilo?oysterbay...
 
kwani wapo wangapi mkuu?


Story inasikitisha kwa kweli, wahusika wachukuliwa sheria maana nchi inaongozwa kwa sheria,.
Nchi hii ilivyooza nani wa kuchukua sheria? Kwenye hiki kisa msichana alienda kuripoti polisi lakini polisi badala
ya kumsaidia wakamla uroda na kukaa upande wa mama mwenye danguro. Eti nchi ina serikali! My foot!
 
Pia kama kuna anaemfahamu huyo mama aanikwe hadharani na ahukumiwe na kufungwa jela ya wanaume,hili jumba lipo wapi????
 
Haya majumba yanajulikana,naukisema tu unabambikiwa kesi.Na wakubwa wanajau hili.
Hii nchi ni ya amani ila nasema siku kikinuka basi ni balaa.
Maana uchafu wote huu unajulikana.Hiii Biashara ni sawa na ya wauza Unga.
Hembu chukua mfano wa Biashara ya Unga:
Hivi kweli unafikiria wauzaji Serikali haiwajui?
Mfano:Wewe chukua Laki moja mpe Teja,atakutajia mtu anaefuata,yule anaefuata mpe milioni mbili atakutajia mtu wa kati,nae mpe milioni kumi atakutajia dealer au boss.Very simple.
Ila jaribu uone.
Hata hivyo Joyce shujaa sana kwa hili ila hata yeye anaogopa,maana huyo binti hilo Jumba analijua na wahusika wote anawaju,sasa bado anaogopa kujitosa kama anavyojitosa kwa wengine mpaka kuwafuata mikoni kama ilviyo kwenye baadhi ya vipindi,ila hii ni Dar tena Oysterbay lakini kangia mitini kufuatilia hilo jumba.

We ukisikliza yule Dada anakuambia Polisi wa Osyerbay walisema kwamba hawezi kushindana na mwenye pesa,na baadhi yao ni wateja wa yule Mama,mwishoe wakamzingua akasepeshwa.Pesa ndio kila kitu nchi hii
 
Hakika hawa wanawake mashankube wa mujini wanatakuwa waswekwe magereza. Hivi polisi na usalama hawajui madanguro haya? au niseme kuna rushwa cash and in kind au ni sehemu ya wateja?
 
Back
Top Bottom